Chadema hawana cha kujifunza kutoka CUF, kwani hata CCM sasa wanahangahika ili wapate watu makini na wenye uchungu na nchi yetu kama walioko CHADEMA. Fanya tu utafiti uliomdogo kabisa utagundua kwamba wote wenye ueelewa mzuri wako CHADEMA na kwa wale ambao bado wapo CCM ni kwasababu wanapigania matumbo-maslahi yao. Ili uwe na uhakika angalia hata matokeo ya Uchaguzi mwaka jana. Sehemu zote wenye watu makini waliipigia kura CHADEMA. CCM walipata kura vijijini ambapo ni rahisi kuwarubuni watu kwa vitu vidogovidogo kama Khanga, kofia , 2000 na VITISHO. Hakika CHADEMA wana watu makini sana, jpo mimi siyo mwanachama wao, lkn hilo haliwezi kunifanya nisiseme ukweli kwamba CHADEMA wana watu makini kuliko sisi japo tuna wanachama wengi na resource nyingi kuliko wao.