CHADEMA waanzishe na kumiliki News Media zao

Chesty

JF-Expert Member
Aug 30, 2009
5,777
2,720
Ni jambo lililo wazi kuwa watanzania tumebadilika sana kimitazamo na kuwa forums zilizopo na hasa TV na radio kwa mtazamo wangu zinashindwa kukidhi kiwango cha upevu wa kimawazo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Ukiangalia TV karibu zote TZ na hata radio zetu nyingi zina muelekeo wa entertainment zaidi na kama ni siasa basi ni za kiwango cha uelewa wa chini sana na au ushabiki ambao unakosa uhalisia wa mambo hivyo kutengeneza ombwe katika nyanja hii.

Ukiangalia kwa mfano radio zetu za FM ambazo nilitegemea zingekuwa na coverage kubwa sana ya siasa na uchumi, nyingi zina vijana ambao elimu na uelewa wao ni wa chini sana (si nia yangu kudharau) na hivyo hata mazungumzo ni ya level ya chini sana.

Kenya kwa mfano FM radio stations kama Capital FM, zina vijana waliosoma degree ya Mass Communication na hata vyuo vikuu vingine na hivyo kuwa na mijadala yenye mantiki, ya kisomi na yenye kuvutia hasa.

Sasa ili tuweze kukidhi haja ya wasikilizaji wengi wanaopenda indepth discussions katika nyanya muhimu nashauri CHADEMA tuwe na mkakati wa kuongeza visibility yetu na pia kushiriki katika kuwapa elimu ya uraia wananchi wetu kwa kuanzisha TV station na Radio.

Nna imani vijana wengi wasomi watapata ajira na wengi tutapata nafasi ya kushiriki, kusikiliza na kuangalia vipindi vyenye mitazamo ya kimaendeleo kuliko ilivyo sasa.

Naomba kuwasilisha.

========
Oktoba 05, 2011
Ndugu wana JF

Wote mnajua kuwa CDM inakubalika mijini zaidi kwa sababu zifuatazo:
1. Mjini kuna wasomi wengi ambao ni wepesi wa kuchambua mambo
2. Upatikanaji wa Vyombo vya habari vingi
3. Kampeni nyingi huwa zinaishia mijini hasa kwa sababu ya ufinyu wa budget

Ili CDM iweze kuchukua dola 2015 in wazi kuwa ni lazima iweke mkakati wa kwenda vijijini kwa muda huu ili kiweze kuweka mizizi huko kama ilivyo kwa CCM. Kazi hii ni ngumu na inaitaji fedha nyingi.

Napendekeza uongozi wa CHADEMA waanzishe mfuko maalumu ambao wanachama na watanzania wote wenye mapenzi mema na wanaopenda kulikomboa taifa hill 2015 wachangie ili kufanikisha CHADEMA kuenea vijijini. Pia mfuko huo uwezeshe CHADEMA kuanzisha TV na Radio yake ili kiweze kunadi sera zake zaidi. Katika kurahisisha uchangiaji utaratibu wa M-Pesa, Tigo pesa nk, etc utakua mzuri sana kutumika.

Nawasilisha
Agosti 27, 2012
Ndg wana JF napata taabu kuona CHADEMA chama kikuu cha upinzani nchini, chama tarajiwa kuongoza serikali mwaka 2015, chama chenye mikakati ya uhakika na viongozi makini na shupavu lakini hakina hata chombo kimoja cha habari ktk kurahisisha upatikanaji wa habari za chama na taarifa mbalimali.

Hivi ktk vuguvugu hili la M4C vyombo vya habari kama gazeti, radio au hata televion si ingetufaa kabisa! Nguvu ya umma tuko tayari kuchangia ktk kuanzisha na kuendesha vyombo hivyo au labda kama TCRA watakuwa wametunyima vibari kwa maelekezo ya CCM.

Naomba kufahamishwa kwanini hatuweki nguvu ktk kumiliki vyombo vya habari sie kama chama?

Naomba kuwasilisha.
Oktoba 11, 2012
Wakuu, nadhani kila mtu anaelewa na kutambua umuhimu wa CHADEMA kuwa na television na radio yake hasa katika kipindi hiki cha kuelekea 2015.

Tunajua namna vyombo vya habari vya CCM vinavyoeneza propaganda chafu dhidi ya vyama vya upinzani hususani CHADEMA.

Uwepo wa CHADEMA TV na Radio utarahisisha sana kueneza sera na taarifa mbalimbali zinazoihusu CHADEMA kwa wananchi hususani wale waliopo vijijini ambapo chama hakijaenea sana. Naamini kabisa muda unaofaa kuanzishwa kwa vyombo hivi ni sasa na wala sio kesho.

Je CHADEMA hawalitambui hili?
 
Kwa hili nami naunga mkono na mguu, lakini tusissahau kuwa na mtandao pia wa Chadema zaidi ya ile iliyopo Face book na penginepo.
Lakini radio na TV is very important.

Ikiwezekana hata utaratibu wa kuchangia uanze mapema watu wenye nia nzuri waanze ili kukikuza chama kabla ya mwaka 2015
CCM lazima ing'oke na chekbobu wake wote
 
Mimi pamoja na wengi tupo tayari kuchangia pesa ili hili lifanikiwe. Ni very important kwa kweli.
 
Mimi pamoja na wengi tupo tayari kuchangia pesa ili hili lifanikiwe. Ni very important kwa kweli.
kIMSINGI hizi ni hoja zenye maana sana kwa taifa hili. Kumbukeni redio Tanzania ilianzishwa na watu kama hawa. Leo kuna Uhuru japo imeliwa na mafisadi.
Sasa hili hata mimi nitacahngia!!!! ili mradi means za kuchangia ziwe zile za kawaida i.e. Mpesa, Tigo pesa na Benk pia au hata Msg zile iliwatu wengi zaidi wachangie.

zaidi sana Chadema ifungue matawi mengi zaidi ili vitu mbalimbali viwepo kununuliwa huko as a means ya kuchangia pia.
 
Mimi nasapoti na pia nipo tayari kuchangia tv na redio kwa sababu bado watanzania wengi bado wamelala hasa kisiasa and specifically vijijini.
 
Chesty

You have nailed it. Fully supported.

Ikiwezekana na CUF nao waanzishe TV na redio ili wananchi wapate taarifa tofauti na huu ujinga wa amani, utulivu na mshikamano chini ya umaskini, ujinga na maradhi vilivyokithiri. Hizi TV na radio zilizopo zote ni za walamba viatu vya viongozi na haziwezi kamwe kutoa fair coverage kwa wapinzani kama wanavyotoa kwa CCM. Ushahidi tumeuona wakati wa kampeni.
 
Last edited by a moderator:
Chesty

Naunga mkono hoja. Pia nashauri CHADEMA ianzishe gazeti lake kwa lengo hilo hilo la kuelimisha umma wa watanzania. Kwa kufanya hivyo CHADEMA itafahamika kwa wananchi wengi ambao baadhi yao watakiunga mkono katika kuleta mabadiliko ya kisiasa na hatimaye katika nyanja mbalimbali.

Hata hivyo hayo pekee hayatakidhi ili kufikia malengo ya chama. Ni muhimu kuimarisha uongozi wa chama katika Wilaya zote nchini.
 
Last edited by a moderator:
Muhimu ni kampeni ya kuandikisha wapiga kura wengi zaidina wanachama wapya nilwahi kumsihi sana MNYIKA kuhusu hili.Ile mikutano ilijaza sana watu ni muhimu watu wale tuwasajili....kwa kutoa kadi bure
 
Pia utakuwa ni mkakati mzuri sana wa 2010, watu watajua upande wa pili wa shilingi. Sio siri kwa watu ambao bado hawajafunguka vizuri TBC1 inazidi kuwapa upofu kabisa.

They need opinions ambazo zitawaondoa kwenye giza hilo.

Nna uhakika mawazo mbadala yatavutia wengi kusikiliza na kuangalia matangazo hayo.
 
Haya mawazo muafaka kabisa, tuliwahi kujadili huko nyuma lakini nafikiri hayakupata muda wa kufanyiwa kazi.

Nashauri wale wataalamu wa nyanja hizi waanze kututayarishia estimates badala ya kusubiri kila kitu kuwa initiated na viongozi wa chadema. Kwa kuwa chadema ni chama cha wasomi napendekeza tununue shares ili tuweze kutoa michango ya maana kutimiza lengo mapema. Can anybody volunteer to take a leading role.

These are the kind of approaches that need to be brought forward
in the struggle for constitutional changes and major reforms to our electoral commission.
 
muhimu ni kampeni ya kuandikisha wapiga kura wengi zaidina wanachama wapya nilwahi kumsihi sana mnyika kuhusu hili.ile mikutano ilijaza sana watu ni muhimu watu wale tuwasajili....kwa kutoa kadi bure

ccm walipoanza kukosa mweleko na dira walianza na waliondoa mafunzo kwa wananchama kama zamani, wakaanza kutoa kadi bure n.k. That is cheap popularity. Ukimpa kadi bure then next day akaenda kumrejeshea kiongozi wa ccm ndio umeafanya nini? Sisi ndio badala ya kuishia kupiga balaha blaha humu tunatakiwa kila mmoja aende kwa wananchi kuomba kujiunga na chama, kura n.k

chama cha siasa hata siku moja hakiwezi kuendeshwa kwa jamii forum pekee
 
haya mawzo muafaka kabisa tuliwahi kujadili huko nyuma lakini nafikiri hayakupata muda wa kufanyiwa kazi. Nashauri wale wataalamu wa nyanja hizi waanze kututayarishia estimates badala ya kusubiri kila kitu kuwa initiated na viongozi wa chadema. Kwa kuwa chadema ni chama cha wasomi napendekeza tununue shares ili tuweze kutoa michango ya maana kutimiza lengo mapema. Can anybody volunteer to take a leading role.

These are the kind of approaches that need to be brought forward
in the struggle for constitutional changes and major reforms to our electoral commission.

Wenzetu wataalam wa media you can take charge, sisi tupo tayari kuchanga na kuchangisha. Tunataka come 2015 Tanzania yote imeamka.
 
Jatropha

Sasa kwa vile CCM walishindwa basi CHADEMA wasitekeleze? ni muhimu kuwa na database kubwa ya wanachama na kuhakikisha kuwa kila mwanachama amejiandikisha kupiga kura kuliko kujaza mikutano watui ambao hawapigi kura...

MAMBO HAYA MAWILI YAFANYIKE KWA PAMOJA....kusajili wanachama wapya na kuhakikisha kuwa wanajiandikisha kupiga kura....sijui kama CHADEMA wana kitengo cha uanachama...

Chama chochote kile kinaendeshwa na WANACHAMA na sio mashabiki tu...wakati CCM wnakazaia kupanga matokeo kama mkakati CHADEMA ijiimarishe kwa wanachama
 
Last edited by a moderator:
Chesty

Nafikiri pia gazeti. Ili kuwa na coverage kubwa nchini ni vizuri kuanzisha kwa kanda na majina tofauti na usajili tofauti maanake sheria ya utangazaji inaweza kufanya Chadema wasisikike sehemu kubwa ya nchi.
 
Last edited by a moderator:
Lakini umakini unatakiwa pia sababu CCM wanaweza kuhujumu hata hatua za awali za usajili,si unakumbuka ile redio ya dini ya kule mwanza iliyokuwa inatoa elimu ya urai ilivyoletewa zengwe...

Sometimes mlimani tv inakatika mitambo(yaani haipatikani),..this is not accidental..unajua mlimani tv ni ya wasomi hivyo CCM hawaipendi.

Ushauri wangu ni kufikiria zaidi jinsi ya kukubiliana na hujuma za ccm sababu najua itafika point watafikria kuvifungia vituo hivyo...kama waliweza kumzuia shibuda kufanya kampeni,..these crooks are cpable of anything....bravo good idea nilishawahi kuifikiria..u ready my mind...
 
Chesty

Hii ni opportunity ya kumfanya mtu kuwa tycoon. Ni opportunity ambayo unaweza ku-ipursue wewe na marafiki wengine.. Kuwa na media group ambayo inalenga kujadili masuala ya uchumi, siasa za ndani na nje na ku-focus kujaza ombwe iliyopo kwenye soko sasa.

Mwanzilishi wa BET alianzisha empire yake kutoka kwenye mkutano na mtu aliyekuwa anataka kuanzisha TV kwa ajiri ya wazee, akaanzisha ya kwake ya watu weusi.

Nimeattach success story yake it may inspire a person to fill this gap
 
Last edited by a moderator:
Chesty,
Hii ni opportunity ya kumfanya mtu kuwa tycoon. Ni opportunity ambayo unaweza ku-ipursue wewe na marafiki wengine.. Kuwa na media group ambayo inalenga kujadili masuala ya uchumi, siasa za ndani na nje na ku-focus kujaza ombwe iliyopo kwenye soko sasa. Mwanzilishi wa BET alianzisha empire yake kutoka kwenye mkutano na mtu aliyekuwa anataka kuanzisha TV kwa ajiri ya wazee, akaanzisha ya kwake ya watu weusi.
Nimeattach success story yake it may inspire a person to fill this gap

Nilisahau ku-attach
 

Attachments

  • The Billion Dollar Brains Behind BET.doc
    53.5 KB · Views: 87
Back
Top Bottom