CHADEMA, tumsamehe Zitto tusonge mbele; awe mtu asiye na madhara kama Shibuda!

Tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokkuwa vikitoke kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema kitu wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yagu naona hata Zitto asamehewe hata kabla hajawaza kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kauwa sidhani kama atakuwa tayari kuomba msamaha, Tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.


Mkuu hili sio sahihi mfano mdogo tu.

1. Kikwete nimewasamehe wezi wa rada - wezi wa kuku wanafungwa

2. CCM magamba hayajavuliwa wamesameheana kimya kimya

Maswali

1. kama zito atasamehewa nini itakuwa tofauti ya cdm na ccm

2. Kama zito atasamehewa je nini nafasi ya wale akina shonza na wenzake

3. Je kumsamehe zito kunaashiria nini hapo baadae?

a. uwezo wa kufanya maamuzi magumu na kuyasimamia

b. Ubutu na udhaifu wa kufanya maamuzi magumu na kutoweza yasimamia?

Zito lazima afukuzwe na kunyang'anywa uanachama kabisa ilikujenga discpline, na kufanya maamuzi ambayo

watanzania wengi wanayataraji kwa afya ya Taifa kwa ujumla wake. Kugeuka nyuma cdm itakuwa jiwe la chumnvi
 
Huwezi ukamsamehe mtu ambae anajiona kuwa hana kosa lolote Pia huwezi kumufananisha Zitto na Shibuda.Zitto ni mwanachama wa CHADEMA tofauti na Shibuda ambae hakuwa mwanachama wa CHADEMA bali aliitumia CHADEMA kama mbeleko ili aweze kupata ubunge wala hana shida yoyote na CHADEMA na hana madhara yoyote kwenye chama.
 
Nope mkuu, we need to carry each others burdens sometimes! We forgive him, but set him pending so that he can realize what he has done! it will be a big lesson for the rest of us!

Zzk hasameheki na wala hasafishiki, jinsi alivyokuwa mtu smart na alivyokuwa mpiganaji hodari kwa ajili ya wanyonge na masikini wa nchi hii, alijijengea heshima kubwa sana nje na ndani ya cdm, alikuwa askari wa mstari wa mbele kabisa wa kuwapigania maskini wa nchi hii na hata tulijua yeye ni mmoja wa watu walikuwa wakombozi wa kweli wachache sana waliohai leo hii amegeuka na kuwa msaliti wa wanyonge tena anatusaliti kama yuda alivyofanya kwa Yesu, anatuuza kwa vipande thelathini vya fedha na kisha anakuja kutusaliti kwa kutupiga busu kama anatupenda hivi kumbe anawaonyesha adui zetu njia ya kutuua kabisa!!!!! Mwenzake yuda alienda kujinyonga kwenye shamba alilolinunua kwa fedha aliyokuwa anaiba kwenye mfuko wa Yesu na wanafunzi wake huyu naye anapaswa kufanya hivyo hivyo. Hasameheki wala hasafishiki, ni uchungu sana kumpoteza kijana kama huyu niliyemtegemea sana na kumwamini sana, alikuwa kioo changu kwa maswala ya kisiasa. Lakini hakuna jinsi nenda Zzk, nenda ktk njia yako uliyoichaguwa mwenyewe, nenda kwa amani Zzk, tunajifunza kwa makosa yako!!! Tutakukumbuka daima!!!!!!!
 
Tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokkuwa vikitoke kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema kitu wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yagu naona hata Zitto asamehewe hata kabla hajawaza kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kauwa sidhani kama atakuwa tayari kuomba msamaha, Tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.

Usilinganishe Shibuda na Zito. Shibuda ni muhamiaji wakti Zito ni mzawa; Shibuda ni hananyazifa kubwa chamani, wakti Zito ni alipewa dhamana kubwa ya uongozi.

Hivyo basi, Zito kama kiongozi alitarajiwa kuvuta kamba pamoja na wenzake, kukijenga chama badala ya umaarufu wake binafsi akitumia mgongo wa chama. Nadhani hili ndilo jambo gumu kwake
 
mkuu sijaona sharti lolote gumu kwa ndugu zzk...huwezi kumsamehe mtu kosa asilolijuwa..na pia kukiri kuwa kakosea na kuahidi kutorudia makosa.

Mfano wa john ccm shibuda ni case tofauti kabsaaa na kijana zzk..john ni mtoto wa jirani alikuja kuomba kuishi kwetu pia tunaamini alitumwa aje kuishi kwetu ili tukimkataa jirani apate la kutusemea duniani...sie wabaguzi mara chama cha wachaga..ila zzk ni mwanetu wa damu ni wajibu wa mzazi kumlea na kumrejesha kwenye mstari kila anapoonekana kukosea na hasa anapotambua kuwa kakosea....

John ccm shibuda ni sawa na mtu mwenye shari na hila kwa hiyo tunamwangalia afanye afanyavyo ila hatutomgusa wala kumsemesha na ndio maana hutokaa usikie shibuda kupewa hata ujumbe wa nyumba 5 za chadema...

Ila kumbuka zzk ni naibu katibu mkuu...nchi kama china kwa haya anayoshutumiwa kuyafanya alikuwa keshanyongwa zamaniiii... We ni mwendawazimu. Kwan we nan had utoe mashart hayo? Acha kimbelembele kama bao la kwanza.
 
mkuu sijaona sharti lolote gumu kwa ndugu zzk...huwezi kumsamehe mtu kosa asilolijuwa..na pia kukiri kuwa kakosea na kuahidi kutorudia makosa.

Mfano wa john ccm shibuda ni case tofauti kabsaaa na kijana zzk..john ni mtoto wa jirani alikuja kuomba kuishi kwetu pia tunaamini alitumwa aje kuishi kwetu ili tukimkataa jirani apate la kutusemea duniani...sie wabaguzi mara chama cha wachaga..ila zzk ni mwanetu wa damu ni wajibu wa mzazi kumlea na kumrejesha kwenye mstari kila anapoonekana kukosea na hasa anapotambua kuwa kakosea....

John ccm shibuda ni sawa na mtu mwenye shari na hila kwa hiyo tunamwangalia afanye afanyavyo ila hatutomgusa wala kumsemesha na ndio maana hutokaa usikie shibuda kupewa hata ujumbe wa nyumba 5 za chadema...

Ila kumbuka zzk ni naibu katibu mkuu...nchi kama china kwa haya anayoshutumiwa kuyafanya alikuwa keshanyongwa zamaniiii... We ni mwendawazm. Kwan we ni nan had utoe mashart hayo? Acha kimbelembele kama bao la kwanza.
 
zitto ndio anatakiwa kuwasamehe watu kama nyinyi sio kinyume chake!
 
Zzk hasameheki na wala hasafishiki, jinsi alivyokuwa mtu smart na alivyokuwa mpiganaji hodari kwa ajili ya wanyonge na masikini wa nchi hii, alijijengea heshima kubwa sana nje na ndani ya cdm, alikuwa askari wa mstari wa mbele kabisa wa kuwapigania maskini wa nchi hii na hata tulijua yeye ni mmoja wa watu walikuwa wakombozi wa kweli wachache sana waliohai leo hii amegeuka na kuwa msaliti wa wanyonge tena anatusaliti kama yuda alivyofanya kwa Yesu, anatuuza kwa vipande thelathini vya fedha na kisha anakuja kutusaliti kwa kutupiga busu kama anatupenda hivi kumbe anawaonyesha adui zetu njia ya kutuua kabisa!!!!! Mwenzake yuda alienda kujinyonga kwenye shamba alilolinunua kwa fedha aliyokuwa anaiba kwenye mfuko wa Yesu na wanafunzi wake huyu naye anapaswa kufanya hivyo hivyo. Hasameheki wala hasafishiki, ni uchungu sana kumpoteza kijana kama huyu niliyemtegemea sana na kumwamini sana, alikuwa kioo changu kwa maswala ya kisiasa. Lakini hakuna jinsi nenda Zzk, nenda ktk njia yako uliyoichaguwa mwenyewe, nenda kwa amani Zzk, tunajifunza kwa makosa yako!!! Tutakukumbuka daima!!!!!!!

Mkuu kama uliyaona yote hayo iwe ndio source haswa ya kumsamehe Zitto! Ni kijana na sometimes vijana ni vema kuwapa muda!
 
zitto ndio anatakiwa kuwasamehe watu kama nyinyi sio kinyume chake!

Yeye ana makosa, jumuia kubwa imetambua kuwa ana makosa, kama yeye anahisi kakosewa naye awe wazi kuelezea not otherwise!
 
Wewe kuna vitu huelewi na havijawekwa wazi kwa manufaa ya chama, usiwe mshabiki kipofu kama hivyo!

1. Kuchukua hela toka kwa mahasimu
2. Kuwa na mashabiki wa kutoka yanga wakati wewe uko simba
3. Kuandaliwa vikao na viongozi wa Yanga wakati wewe uko simba
4. Kuchukua vijisenti toka taasisi ambazo inabidi uzisimamie n.k

Haa! wewe unalinganisha mambo muhimu ya Mustakbali wa taifa letu na ushabiki wa Simba na yanga?.

Kukusaidia tu, hata kwenye Simba na Yanga mchezaji akiwa timu ya taifa na akafunga magoli, hushangiliwa na Wote isipokuwa wale wanazi wachache!. Zitto Kabwe ni mbunge wa kitaifa, anaibua hoja zenye Maslahi kwa raia wote , kwa hiyo kupendwa kwake na Wanachadema au CCM ni kawaida sana!.

Hata mwalimu Nyerere alikuwa akipendwa na Wanachadema japo alikuwa CCM.
 
Tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokkuwa vikitoke kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema kitu wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yagu naona hata Zitto asamehewe hata kabla hajawaza kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kauwa sidhani kama atakuwa tayari kuomba msamaha, Tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.

Nimefarijika na maneno yako ya busara ndg yangu! Hakika tunahitaji kumsamehe na Chama kisonge mbele. Hatuhitaji marumbano tena tunacho hitaji ni kulikomba Taifa letu kutoka mikononi mwa wahaini Ccm!
 
Haa! wewe unalinganisha mambo muhimu ya Mustakbali wa taifa letu na ushabiki wa Simba na yanga?.

Kukusaidia tu, hata kwenye Simba na Yanga mchezaji akiwa timu ya taifa na akafunga magoli, hushangiliwa na Wote isipokuwa wale wanazi wachache!. Zitto Kabwe ni mbunge wa kitaifa, anaibua hoja zenye Maslahi kwa raia wote , kwa hiyo kupendwa kwake na Wanachadema au CCM ni kawaida sana!.

Hata mwalimu Nyerere alikuwa akipendwa na Wanachadema japo alikuwa CCM.

Inaelekea kuna vitu huelewi mkuu, nimetoa mfano wa impossibilities, kuna vitu mtu akifanya jamii inayomzunguka inamshangaa! ni pamoja na mambo niliyoyaandika kwa kutumia mfano wa hizo timu!

Huwezi ukawa una mashabiki wengii wa yanga wakati wewe uko simba, watu wa yanga watakuwa wanakuona bora lakini udhaifu wako ndio unakuwa issue zaidi ya ubora wako! Sasa kwa case ya Zitto maCCM wataona strengths zake nyingi zaidi ya weaknesses! Sijui kama unanielewa!

Anaweza akawa bora, lakini ubora wake ungetakiwa uwe dhahili kwa wana CDM not otherwise, Harafu hivi inaclick akilini kwa nini viongozi wa CCM waandae mkutano wa press ya Zitto? Huoni kama hao viongozi wa CCM hamnazo? Hatakama wanahusika na mgogoro CDM walitakiwa wawe sidelined kinamna, Hapo majibu yanatoka, kwakuwa most CCMs huwa hawatafakali and wanajihisi kama wana upeo mkubwa na wanajihisi kuwa ati wana nguvu kubwa za ushawishi doubtfull events hawazizingatii! Zinazidi kumdhalilisha Zitto kwa jamii!
 
Nimefarijika na maneno yako ya busara ndg yangu! Hakika tunahitaji kumsamehe na Chama kisonge mbele. Hatuhitaji marumbano tena tunacho hitaji ni kulikomba Taifa letu kutoka mikononi mwa wahaini Ccm!

Chukua like kwangu ndugu yangu!
 
Ndugu usaliti ni dhambi mbaya sana. Heri ya mchawi kuliko msaliti. Yuda Iskariote alivyosaliti Bwana Yesu,alilaaniwa"Ni heri asingelizaliwa". Msaliti hana faida katika jamii,ni mwuaji,ni heri asingezaliwa.
 
Ndugu usaliti ni dhambi mbaya sana. Heri ya mchawi kuliko msaliti. Yuda Iskariote alivyosaliti Bwana Yesu,alilaaniwa"Ni heri asingelizaliwa". Msaliti hana faida katika jamii,ni mwuaji,ni heri asingezaliwa.

Mkuu una hasira kali, punguza kidogo ukali wa maneno, hahaha!
 
Yeye ana makosa, jumuia kubwa imetambua kuwa ana makosa, kama yeye anahisi kakosewa naye awe wazi kuelezea not otherwise!

Ni ngumu kuishi na Shibuda wawili ndani ya Chama. Ni sawa na kuongeza adui mwingine wa Tano wa Taifa letu, yakiwemo Umasikini, Ujinga, Maradhi na CCM.
Yuda Iskariote baada ya kumsaliti Yesu aliondolewa duniani kwa kifo. Alijinyonga.
Ni kosa kubwa kumsamehe Zitto Kabwe.
 
Ndugu Kasimba B huyo Zito mtu hatari saana hafai!! Ni ndumila kuwili ili chama kiwe na Afya ni lazima Zito aondoke ni muharibifu hafai kabisa!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom