Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,505
- 51,101
Mikutano yenu huwa mnaianza kwa sala. Hilo ni jambo zuri sana. Maana mnamtanguliza Mwenyezi Mungu mbele.
Lakini wakati mkianza kwa sala, Wale ambao huwa mnawaita kufanya sala kwa niaba ya Wakiristo huwa ni watu ambao kwa namna moja huwa ni watu wenye authority katika taasisi zao za imani, wanaelewa protokali za maombi, yaani ni profeshno. Huwa ama ni wachungaji, mapadri au hata maaskofu.
Lakini inapokuja katika Kuomba dua kwa niaba ya waislamu, huwa ni kama hamjajiandaa kwa nukta hiyo ya mkutano, huwa mnakurupuka na kuita yeyote bora liende.
Matokeo yake, Huyo mtu anakuja kuomba vitu ambavyo kwa mujibu wa Imani ya kiislamu ni makosa makubwa sana, tena makosa yanayokulazimu kutubu baada ya kufanya hayo.
Kwa mfano Juzi katika mkutano wenu pale Bulyaga, mlimuita Askofu Mwamakula kuombea mkutano. Huyo ni profeshno , ana hekima zake, na anajua aombe nini.
Ilipokuja muda wa Muislamu kuomba dua, Mkajichukulia kamanda tu aliyevaa kombati za chama, Dua yake anachanganya maombi, Wakati mwingine anamuomba Mungu na wakati huohuo anamuomba Mtume. Kwenye Uislamu kumuomba Mtume ni kosa kubwa sana. Anayepaswa kuombwa ni Mwenyezi Mungu tu.
Na pia mambo anayoomba mengine ni mabaya, yamekaa kisiasa, hayaendani na hekima za maombi ya Waislamu yaliyofundishwa na mtume.
Sasa vitu kama hivi vinafanya Waislamu waone chama chenu ni Insensitive kwa Imani yao. Kwamba chama hakichukui muda kuwapa heshima stahiki kama ambavyo kinafanya kwa wakiristo. Na hivyo bila kujua kujikuta kinaingia katika mtego wa Propaganda kinaotengenezewa na mahasimu wao wa kisiasa yaani CCM.
Nafahamu, CHADEMA ni taasisi ya kisiasa na si kidini. Ila pale mtakapoamua kuinvolve watu wa dini basi pelekeni watu wanaostahiki kutoka pande hizo.Siyo upande mmoja unamleta baba mchungaji aombe dua, halafu upande wa pili unafanya zimamoto ilimradi bora liende.
Hili tatizo nimelishuhudia katika mikutano yenu mingi huko mikoani, Hamjajiandaa vizuri kwenye nukta ya waomba dua kwa niaba ya Waislamu. Huwa mnafanya tia maji tia maji. Sasa hii inawaput off Waislamu vibaya sana.
Rekebisheni hii kitu, mnaweza kudhani siyo issue ila nakuhakikishieni ni issue kubwa kwa waislamu nchini wanaofuatilia mikutano yenu.
Lakini wakati mkianza kwa sala, Wale ambao huwa mnawaita kufanya sala kwa niaba ya Wakiristo huwa ni watu ambao kwa namna moja huwa ni watu wenye authority katika taasisi zao za imani, wanaelewa protokali za maombi, yaani ni profeshno. Huwa ama ni wachungaji, mapadri au hata maaskofu.
Lakini inapokuja katika Kuomba dua kwa niaba ya waislamu, huwa ni kama hamjajiandaa kwa nukta hiyo ya mkutano, huwa mnakurupuka na kuita yeyote bora liende.
Matokeo yake, Huyo mtu anakuja kuomba vitu ambavyo kwa mujibu wa Imani ya kiislamu ni makosa makubwa sana, tena makosa yanayokulazimu kutubu baada ya kufanya hayo.
Kwa mfano Juzi katika mkutano wenu pale Bulyaga, mlimuita Askofu Mwamakula kuombea mkutano. Huyo ni profeshno , ana hekima zake, na anajua aombe nini.
Ilipokuja muda wa Muislamu kuomba dua, Mkajichukulia kamanda tu aliyevaa kombati za chama, Dua yake anachanganya maombi, Wakati mwingine anamuomba Mungu na wakati huohuo anamuomba Mtume. Kwenye Uislamu kumuomba Mtume ni kosa kubwa sana. Anayepaswa kuombwa ni Mwenyezi Mungu tu.
Na pia mambo anayoomba mengine ni mabaya, yamekaa kisiasa, hayaendani na hekima za maombi ya Waislamu yaliyofundishwa na mtume.
Sasa vitu kama hivi vinafanya Waislamu waone chama chenu ni Insensitive kwa Imani yao. Kwamba chama hakichukui muda kuwapa heshima stahiki kama ambavyo kinafanya kwa wakiristo. Na hivyo bila kujua kujikuta kinaingia katika mtego wa Propaganda kinaotengenezewa na mahasimu wao wa kisiasa yaani CCM.
Nafahamu, CHADEMA ni taasisi ya kisiasa na si kidini. Ila pale mtakapoamua kuinvolve watu wa dini basi pelekeni watu wanaostahiki kutoka pande hizo.Siyo upande mmoja unamleta baba mchungaji aombe dua, halafu upande wa pili unafanya zimamoto ilimradi bora liende.
Hili tatizo nimelishuhudia katika mikutano yenu mingi huko mikoani, Hamjajiandaa vizuri kwenye nukta ya waomba dua kwa niaba ya Waislamu. Huwa mnafanya tia maji tia maji. Sasa hii inawaput off Waislamu vibaya sana.
Rekebisheni hii kitu, mnaweza kudhani siyo issue ila nakuhakikishieni ni issue kubwa kwa waislamu nchini wanaofuatilia mikutano yenu.