Wana JF wenzangu napenda kukishukuru CDM kwa chachu kiliyoleta ndani ya Bunge na serikali iliyo likizo ya CCM, Lakini ninakuwa na hofu juu ya utendaji ama uwajibikaji wa baadhi ya wabunge wetu majimboni, tunaenda mwaka wa pili sasa lakini kwenye majimbo hali bado ni tete sio kwa wananchi kupewa zawadi, michango au misaada ya mtu mmoja mmoja, ila katika kuwapanga wananchi kutumia japo raslimali kidogo zilizopo kwenye maeneo yao. Juzi niliwasikia vijana wasukuma matoroli yenye bendera ya CDM wakiuza maji wakisema mbunge wao ni mbunge wa Taifa, kwamba yuko makini sana kwenye mambo ya kitaifa ila jimboni anakuja kusalimia ndugu zake. Je kama hali ndo inaanza kuaw hivi Taswira ya chama na imani yake kwa umma wa maskini wa kitanzania itabaki wapi?