Elections 2010 CHADEMA Haijawafikia wapiga Kura

Mbogela

JF-Expert Member
Jan 28, 2008
1,384
257
Slaa_Musoma.JPG chadema4.jpg wananchama.JPG Nikilinganisha kwa muonekano wa picha za mikutano kati ya CCM na CHADEMA naona kuna kundi kubwa la wapiga kura nalikosa kwenye picha za CHADEMA, si waongeaji sana lakini ndio huamua nani awe kiongozi kutokana na nguvu yao ya kujitoa, uvumilivu na uwingi wao. Kwa waliofika kwenye mikutano labda kamera huwa haziwaoni, Je wapo wapiga kura hawa?
 
mwaka huu ni zamu yenu kulinganisha umati kwenye mikutano, mmesahau dharau yenu wakati wa mikutano ya mrema.
 
Chadema watapata kura kibao toka hapa JF....! Lakini sio huko kwenye wapigaji wa kura halisi.
 
Chadema watapata kura kibao toka hapa JF....! Lakini sio huko kwenye wapigaji wa kura halisi.
Wewe umerudi kuja kupata aibu yako hapa?
Ulikimbia sasa wakati wa kampaini mtani wangu naona umerudi. Karibu lakini pigo lako liko njiani maana nimejichimbia huku kijijini nafanya kampeni achaguliwe Dr silaha ili mpate cha mtema kuni.
 
mwaka huu ni zamu yenu kulinganisha umati kwenye mikutano, mmesahau dharau yenu wakati wa mikutano ya mrema.
Sidhani kama la msingi ni Idadi ya umati wanaofika kwenye mikutano, mimi wasi wasi wangu je wale wanaotumia wino kwenye kikaratasi cha kupigia kura, wale watakao weka Vema kwenye hilo karatasi na kulitumbukiza kwenye box la tume ya Uchaguzi wamefikiwa, maana wanaokuja mikutanoni wamo na wasio kuwemo. Ukiangalia hizo picha hapo mimi naona utofauti wa wazi kabisa.
 
Wewe umerudi kuja kupata aibu yako hapa?
Ulikimbia sasa wakati wa kampaini mtani wangu naona umerudi. Karibu lakini pigo lako liko njiani maana nimejichimbia huku kijijini nafanya kampeni achaguliwe Dr silaha ili mpate cha mtema kuni.
Nipo Mkuu, kushuhudia ndoto za mchana za Chadema.... by the way huyo jamaa yenu ni silaha ya aina gani?
 
Mkuu Mbogela umeona mbali, asante sana ....kwa kuwakumbusha, CHADEMA wanatakiwa wawafikie wapiga kura wa kada zote, wakumbuke biashara ni Matangazo.
Wakumbuke pia kuwaambia wapiga kura kwamba kuchagua upinzani siyo kuchagua vita, maana chama cha mafisadi ndo mtaji wao kudanganya wananchi amani amani huku wanakwapua rasrimali zetu kwa nguvu zote bila huruma, na wenye mali wanaishi kwenye umaskini wa kupindukia. Safari hii tunasema hatudanganyikiiiii!!!!!!!
Semeni tuu Chadema watapata kura hapa JF, hivi kweli mtu na akili zake timamu (kama sio mbinafisi asiyejua shida, asiyejua kuna watu wanakufa kwa sababu tu alikumywa maji machafu, kuna watu hawajui kesho atakula nini, aliyelewa na matunda/matokeo ya ufisadi) anashabikia CCM?? lol, Ndugu yangu tumia akili yako iko siku utajuta, maana yana mwisho! Chini ya jua hakuna kinachoshindikana. Mungu ni wetu sote!!!
 
Chadema watapata kura kibao toka hapa JF....! Lakini sio huko kwenye wapigaji wa kura halisi.

Kibunago ndio maana majimbo ya kwenye miji mikubwa yako nyuma kwa mageuzi, yapo nyuma kwasababu wapiga kura wake sio wavumilivu kwenye karaha zinazoambatana na zoezi la kupiga kura, kwa mfano watu wa dar, wazee wa mishe mishe, wakati wa kuhakiki daftari la kupiga kura hawawezi kuvumilia kukaa kwenye mstari na jua kali au mvua kukamilisha zoezi, maana kwenye diary zao kuna appointment kibao. Lakini ukiangalia kwenye picha kuna kundi maalum la wapiga kura(utofauti wa wazi) ambalo naamini lina uvumilivu na linadetermine nani aongoze nchi hii, Kundi hili limefikiwa?
 
Semeni tuu Chadema watapata kura hapa JF, hivi kweli mtu na akili zake timamu (kama sio mbinafisi asiyejua shida, asiyejua kuna watu wanakufa kwa sababu tu alikumywa maji machafu, kuna watu hawajui kesho atakula nini, aliyelewa na matunda/matokeo ya ufisadi) anashabikia CCM?? lol, Ndugu yangu tumia akili yako iko siku utajuta, maana yana mwisho! Chini ya jua hakuna kinachoshindikana. Mungu ni wetu sote!!!
Leta mifano hai ya haya madai yako, yametokea wapi na lini na yamesababishwa na nini na kwa vipi yameweza kutokea?
 
Kibunago ndio maana majimbo ya kwenye miji mikubwa yako nyuma kwa mageuzi, yapo nyuma kwasababu wapiga kura wake sio wavumilivu kwenye karaha zinazoambatana na zoezi la kupiga kura, kwa mfano watu wa dar, wazee wa mishe mishe, wakati wa kuhakiki daftari la kupiga kura hawawezi kuvumilia kukaa kwenye mstari na jua kali au mvua kukamilisha zoezi, maana kwenye diary zao kuna appointment kibao. Lakini ukiangalia kwenye picha kuna kundi maalum la wapiga kura(utofauti wa wazi) ambalo naamini lina uvumilivu na linadetermine nani aongoze nchi hii, Kundi hili limefikiwa?
Nimekusoma mkuu, moja ya sababu ya kuwepo na ushindani wa hali ja juu katika chaguzi za Tanzania Visiwani, ni kwa vyama kujua wapiga kura wao. Kwa mfano Diwani katika wadi yake anauwezo wa kujua zaidi ya asilimia 90 ya watu watakaompigia kura siku ya uchaguzi. Hivyo kuanzia siku za kampeni huweza kuwa nao sambamba na siku ya kupiga kura huhakikisha kuwa asilimia yate anayoijua kumpigia kura inafanya hivyo. Hii ni pamoja na hata wagonjwa waliolazwa sipitali.

Hali hii ni pamoja kwa Wawakilishi na Wabunge. Uhamamishaji wa kupiga kura upo kwa kiwango cha hali ya juu sana, kuanzia kwa vijana wa miaka 18 hadi kwa wazee wa miaka zaidi ya 90.
 
Leta mifano hai ya haya madai yako, yametokea wapi na lini na yamesababishwa na nini na kwa vipi yameweza kutokea?
unataka mifano hai kama huishi tanzania unataka uonyeshwe matatizo hadi tarehe.......wewe kweli si kunywa maji ya bendera tu bali umelewa.
 
unataka mifano hai kama huishi tanzania unataka uonyeshwe matatizo hadi tarehe.......wewe kweli si kunywa maji ya bendera tu bali umelewa.
Simply, hakuna Mtanzania anayekufa kwa njaa, labda yatokee maafa kama tunavyoona leo huko Pakstani na China.
 
Hali hii ni pamoja kwa Wawakilishi na Wabunge. Uhamamishaji wa kupiga kura upo kwa kiwango cha hali ya juu sana, kuanzia kwa vijana wa miaka 18 hadi kwa wazee wa miaka zaidi ya 90.
Uko sahihi kabisa, lakini nadhani ni muhimu kutambua makundi ambayo hujitokeza kwa wingi kupiga kura, angalia hizo picha mbili, Moja imechukuliwa leo wakati JK akishukuru wananchi baada ya kurudisha form na nyingine Dr. Slaa akihutubia jangwani, angalia mitari miwili mitatu ya watu waliokaa mbele, alafu angalia uwiano huo mpaka nyuma ya picha zote mbili. Kuna kundi wanaweza kushawishiwa kuuza karatasi yake ya kupigia kura kirahisi na kuna kundi haliwezi kushawishika na vishawishi kuuza karatasi, kuna kundi kubwa kwenye mikutano, kwenye makanisa hawa huwa wengi kuliko wengine, nadhani wakipata meseji, na ujumbe unaowagusa ni rahisi kugusika mioyo yao na huwa wepesi wa kuona huruma, waambiwe ukweli juu ya wapi nchi inaenda nadhani hawa hawajafikiwa, WANAWAKE. Kuwe na mkakati makusudi wa kutafuta kura za wanawake, ni kundi muhimu sana kijamii, wanaweza wasiwe na ushawishi mkubwa lakini ni watu walio wengi.
 
Wakuu, wala tusimshambulie kibunango....

ndani ya hizi siku chache nimebahatika kupita Dar, pwani, morogor, dodoma, manyara, tanga, na arusha... jioni hii nimeiona moshi [hadi sasa]... ukipita dar moro to dodoma, utaona ccm iko kila kona [nimetumia bendera vijiweni, pikipiki zenye nembo au bendera na mavazi]... it is the same situation ukipitadodoma arusha, arusha tanga na tanga dar

tusipende kuwa wabishi pale ambapo hatuna facs au at least some viashirishi vya hali halisi

NIJUAVYO MIMI [I MAY BE WRONG] MAGEUZI MENGI HUANZIA MIJINI... JE CHADEMA HALI IKOJE DAR, MWANZA, GEITA, DODOMA, ARUSHA, MBEYA, TANGA NA SHINYANGA?

LOOKING DEEP DOWN, THER IS SOMETHING MISSING KWENYE OPPOSITION, NA CHA KWANZA NI HAWANA COMMON ENEMY... THAT IS BENEFICIAL KWA CCM

HUO NDIO UKWELI, NA MUDA NI MDOGO, CHA MAANA NI KUWASAIDIA KIMAWAZO WAPINZANI WAUNGANE

JIONI HII NASKIA BAADHI YA MAJIMBO KUNA WAPINZAI WANNE AU WATANO... THIS IS GREAT NEWS TO CCM


UPINZANI SI CHADEMA PEKEE...
 
kumbuka chadema hawatumii fedha za mafisadi kueneza chama na kuhonga watu waweke bendera kwenye nyumba na magari watu wanaoipenda chadema ni wale wenye mapenzi ya dhati hawafuati kofia,chumvi kam a wana ccm ambao wengi wao akili zao ziko tumboni
kumbuka watu wakijiunga na vyama vya upinza ccm kupitia polisi huwaonea na kama ni mfanyabiashara huweza kufilisiwa ndio maana hatuweki bendera, pia kumbuka watendaji wa vijiji ni wana ccm hivyo hufuata maelezo ya wakubwa wao ccm
 
kumbuka chadema hawatumii fedha za mafisadi kueneza chama na kuhonga watu waweke bendera kwenye nyumba na magari watu wanaoipenda chadema ni wale wenye mapenzi ya dhati hawafuati kofia,chumvi kam a wana ccm ambao wengi wao akili zao ziko tumboni
kumbuka watu wakijiunga na vyama vya upinza ccm kupitia polisi huwaonea na kama ni mfanyabiashara huweza kufilisiwa ndio maana hatuweki bendera, pia kumbuka watendaji wa vijiji ni wana ccm hivyo hufuata maelezo ya wakubwa wao ccm
If you want me to take your words [mia kwa mia]... Then vita iliyo mbele ni kubwa kuliko uwezo, na basi tuache tu!!!

Kauli yako bado haijanionyesha nini kifanyike, bali imenikumbusha nini kilichopo
 
kumbuka watu wakijiunga na vyama vya upinza ccm kupitia polisi huwaonea pia kumbuka watendaji wa vijiji ni wana ccm hivyo hufuata maelezo ya wakubwa wao ccm
Asante kwa kubainisha wazi kundi moja la watu muhimu sana kwa mageuzi, hao watu badala ya kuwaona adui labda tubadirishe mtazamo, tuwaone ni watanzania ambao wapo hapo kwa ajili ya kupata riziki halali kama mtanzania mwingine anayefanya kazi nyingine, sasa basi wabaki kule kwenye upolisi wao au Utendaji kimwili, lakini imani yao na nia zao ziletwe kwenye mageuzi, siku ya kupiga kura wapigie Mageuzi ya kweli, Tumaini la kweli.
 
Acid
Hivyo vibendera kwenye vibanda na maduka visikutishe. Hata mimi kwenye genge ninalomiliki ipo bendera ya CCM. Wala haihusiani na mapenzi kwa chama hicho. Ila CCM wanapandikiza hofu fulani kwamba ukiweka hiyo bendera, wewe uko kwenye safe side.

NB: Ni wananchi wenye nguvu na uwezo wa kuchagua chama wanachokitaka.
 
Simply, hakuna Mtanzania anayekufa kwa njaa, labda yatokee maafa kama tunavyoona leo huko Pakstani na China.

Watu mkinyweshwa maji ya bendera ya kijani na njano huwa hata macho yenu hayaoni wala masikio yenu hayasikii tena. Wewe hujaona wala hujasikia madhara makubwa ambayo wameyapata watu kutokana na mgodi wa North mara ambako CCM iliwathamini zaidi wazungu kuliko wakazi wa huko? Fuata link hii uone: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/56294-hatari-mgodini-north-mara-chukua-hatua-5.html. Pia unataka kusema kwamba hukumbuki manyanyaso na mauaji yaliyofanywa na CCM kule Bulyanihulu ambako CCM ilizika watanzania wakiwa hai ili kumpa madini yetu mzungu bure. Nyie CCM kuna wakati mnakera sana, hasa pale mnapojifanya hamjui uovu wenu ilihali upo obvious.
 
Back
Top Bottom