Elections 2010 Chadema, CUF kupambana kwenye mdahalo

Ujengelele

JF-Expert Member
Jan 14, 2008
1,253
22
Imeandikwa na Theopista Nsanzugwanko;
Tarehe: 22nd September 2010

BAADA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukataa kushiriki midahalo ya wazi, mdahalo mwingine umeandaliwa ukilenga baadhi ya wagombea vijana kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) na Chama Cha Wananchi (CUF).

Baadhi ya wagombea ambao watakuwa katika mdahalo huo, ni pamoja na Mbunge wa Kuteuliwa anayemaliza muda wake, Ismail Jussa Ladhu, anayegombea uwakilishi wa Mji Mkongwe kupitia CUF.


Wengine ni mgombea ubunge wa Chadema Ubungo, John Mnyika na mgombea ubunge wa CUF katika jimbo hilo, Julius Mtatiro, mgombea wa Chadema Kilombero, Regia Mtema na wa Chadema Vunjo, John Mrema.


Mdahalo huo maalumu kwa wagombea vijana, utarushwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha ITV keshokutwa saa moja usiku na utahudhuriwa na waalikwa 200.


Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa Mdahalo huo, Rosemary Mwakitwange, alisema kaulimbiu ya mdahalo huo ni ‘Tanzania Tunayoitaka' na Mwenyekiti wake atakuwa mwanaharakati na mwandishi aliyebobea, Jenerali Ulimwengu.


Alisema mdahalo huo ulioandaliwa na taasisi za East African Business and Media Training na Vox Media Center Limited, ulikuwa na nia ya kushirikisha vijana wa vyama vitatu vilivyokuwa na wabunge katika awamu iliyopita, ikiwamo CCM, lakini walipowasiliana na Kamati ya Kampeni ya Chama hicho tawala, ilikataa kushiriki.


Akizungumzia vyama vingine vyenye wagombea, alisema imekuwa vigumu kushirikisha wagombea wote, kwa sababu ya muda , kwani wangezungumza kwa muda mfupi huku wengine wakikosa muda huo hivyo walitaka vyama vishiriki kutoa idadi ndogo ya wagombea.


Alisema, lengo la mdahalo huo ni kutoa nafasi kwa wapiga kura kuwafahamu na kusikiliza hoja za vijana wanaoomba ridhaa ya kuingia bungeni kwa miaka mitano ijayo, huku wakiwahamasisha vijana wengine kwa kuwapa ujasiri wa kushiriki siasa.


"Mdahalo huu umemlenga kijana anayetafuta ridhaa ya wapiga kura ya kuingia katika chombo cha kutunga sheria zitakazowaathiri Watanzania wote, hata wasiokuwa ndani ya jimbo lake au chama.


"Utatoa nafasi kwa wapiga kura kuwaona ili kupima matarajio ya Watanzania ndani ya miaka mitano na zaidi, kwani vijana wa sasa wanaweza kukaa ndani ya Bunge kwa muda mrefu," alisema Mwakitwange.


Alisema, mdahalo huo hautagusa maisha binafsi ya wagombea kwa lengo la kuwadhalilisha au kuwachafua, hautatoka nje ya majadiliano yenye malengo ya kutoa majibu kwa wananchi na wapiga kura juu ya mustakabali wa Taifa.


"Utazingatia ujenzi wa demokrasia kuliko itikadi za vyama, ingawa washiriki wana nafasi ya kurejea hadidu kadhaa za ilani za vyama vyao katika kujenga hoja," alisema.
 
Safi sana ITV, Vox Media, Jenerali Ulimwengu na wote waliohusika kuja na wazo hili. Nadhani huu hautakuwa mdahalo wa mwisho, CCM watajuta kukurupuka kuwakataza wagombea wao kushiriki midahalo na hii yote inatokana na wao kutokuwa na mgombea imara wa ngazi ya urais. Kwa hiyo ilikusudi waweze kujitetea kwa mgombea wa urais kutoshiriki mdahalo wamewazuia wagombea wote ili wajifiche nyuma ya pazia la msimamo wa chama
 
Wanagoma kuongea na wananchi muda huu wa kuomba KUR/LA. Tukiwachagua tutawaona kweli au ndio watahamia hotelini mpaka 2015?
 

Attachments

  • mdahalo.pdf
    677.1 KB · Views: 71
Kesho kutwa nini maanake?
tupe tarehe na muda wa kipindi bana tafadhali.

naona jamaa kaweka habari ya gazetiI guess sasa tofanye homework kujua kesho kutwa ni lini ,muda ni saa moja jioni chanel ni ITV.

Kwa uelewa wangu kwakuwa habari ni ya tarehe 22 basi kesho kutwa ni tarehe 24mwezi huu ,usiulize mwezi huu mwezi gani plse,I'll slap u
 
CHADEMA NA CUF..tumieni nafasi hiyo kuibomoa ccm , manake nchi nzima mtakuwa mnasikika na CCM hawatakuwa na mtetezi..!

MUNGU AWAPE NINI...?
 
Back
Top Bottom