angalia root
Uliposema unyanyasaji wa kimtandao ulikuwa na maana gani?
Nani wa kulaumiwa? mzazi wake alieweka video yake youtube au wewe na mimi tunaoiangalia?Picha kama hii kuwekwa kwenye mtandao ina mnyanyasa mtoto hasa hizo sexual movement zinazokuwa potrayed, hii ni kama dirty dancin, huoni kama tukimpa miaka mingingine kumi na tano hawezi kukubali picha hizi ziwe public?
Nani wa kulaumiwa? mzazi wake alieweka video yake youtube au wewe na mimi tunaoiangalia?
Hii inaonekana ni Disco Toto, maana sauti na wanaonekana hapo wote ni watoto. Wandaaji wa Disco Toto kuweni macho na yanayotendeka kwenye hizo disco.
Wala sioni kama kuna haja ya kuanza kutafuta mchawi, issue ni kuangalia structures zinazoweza kuwakinga watoto wetu na haya maendeleo hapo baadaye. Nchi za wenzetu zimeweka sheria kali sana kuwalinda watoto na unyanyasaji huu, lakini sijui kama Tanzania imejipanga kwenye hili.