CDM Naomba mtusaidie kwa hili.

GAGL

JF-Expert Member
Aug 5, 2010
390
395
Nimeamua kuwaomba CDM japokuwa mimi ni CCM damu kwa kuwa wabunge wetu wa CCM wamekuwa ni watu wa kutetea chama ili kulinda nafasi zao wakati si ccm iliyowapeleka hapo bali ni wapiga kura wao ambao ndo sisi, kwa maana hiyo aidha hawajui wajibu wao au wamesahau wajibu wao kwamba kazi yao ni kuishinikiza serikali kutatua kero za wananchi. Ombi langu ni kama ifuatavyo, tunaiomba CDM kuitisha maandamano ya amani mapema kabla ya bajeti mpya ya 2011- 2012 haijapitishwa, kuishinikiza serikali itenge fungu kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo hasa wanaohitimu vyuo na wenye mawazo ya kijasiriamali kama mimi ili waweze kukopeshwa na kuanzisha au kuendeleza miradi waliyobuni. Naona hili linawezekana kwa kuwa mwaka jana mhe. Rais aliipatia TWB, Tanzania Women Bank shilingi bilioni mbili kuiwezesha, na hii ilikuwa nje ya bajeti ya 2010 - 2011. Sasa kwa mtazamo wangu nadhani kwamba TWB si zaidi ya tatizo la ukosefu wa ajira na mitaji kwa wajasiriamali wanaohitimu vyuo au mafunzo yoyote. Tunaombeni mtusaidie ili sauti yetu ya kinyonge isikike, tutajitokeza kwa wingi katika hili.
 
ombi zuri. Pia usichelewe, vuta kadi na endelea kuhamasisha watu wenye mapemzi mema na nchi yetu maana saa ya ukombozi wa kweli ni sasa-kupitia CDM pekeeeeeeee
 
Nimeamua kuwaomba CDM japokuwa mimi ni CCM damu kwa kuwa wabunge wetu wa CCM wamekuwa ni watu wa kutetea chama ili kulinda nafasi zao wakati si ccm iliyowapeleka hapo bali ni wapiga kura wao ambao ndo sisi, kwa maana hiyo aidha hawajui wajibu wao au wamesahau wajibu wao kwamba kazi yao ni kuishinikiza serikali kutatua kero za wananchi. Ombi langu ni kama ifuatavyo, tunaiomba CDM kuitisha maandamano ya amani mapema kabla ya bajeti mpya ya 2011- 2012 haijapitishwa, kuishinikiza serikali itenge fungu kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo hasa wanaohitimu vyuo na wenye mawazo ya kijasiriamali kama mimi ili waweze kukopeshwa na kuanzisha au kuendeleza miradi waliyobuni. Naona hili linawezekana kwa kuwa mwaka jana mhe. Rais aliipatia TWB, Tanzania Women Bank shilingi bilioni mbili kuiwezesha, na hii ilikuwa nje ya bajeti ya 2010 - 2011. Sasa kwa mtazamo wangu nadhani kwamba TWB si zaidi ya tatizo la ukosefu wa ajira na mitaji kwa wajasiriamali wanaohitimu vyuo au mafunzo yoyote. Tunaombeni mtusaidie ili sauti yetu ya kinyonge isikike, tutajitokeza kwa wingi katika hili.

1. ccm damu maana yake nini?

2. unawezaje kukiunga mkono chama kimoja na ukaamini kuwa unaweza kuhudumiwa na chama kingine?
3. huko ccm umepigwa pingu au kabali kiasi kwamba huwezi kuponyoka?
4. hizo fedha zikitengwa na kusimamaiwa na mafisadi wewe unadhani utafikiwa na sh ngapi?
5. yale mabilioni ya mwanzo ya kikwete binafsi zilikufikia sh ngapi?
6. je, hayo maandamano yakiitishwa, utakuwa tayari kushiriki?
7. vipi kama serilaki ya chama unachokiunga mkono (kilicho kwenye damu yako) kikisema hayo maandamano yanahatarisha amani na yanalenga kumuondoa mwenyekiti wa chama chako madarakani, bado utakuwa radhi kushiriki?

binafsi naomba unisaidie hayo tu

asante mpendwa
 
1. ccm damu maana yake nini?

2. unawezaje kukiunga mkono chama kimoja na ukaamini kuwa unaweza kuhudumiwa na chama kingine?
3. huko ccm umepigwa pingu au kabali kiasi kwamba huwezi kuponyoka?
4. hizo fedha zikitengwa na kusimamaiwa na mafisadi wewe unadhani utafikiwa na sh ngapi?
5. yale mabilioni ya mwanzo ya kikwete binafsi zilikufikia sh ngapi?
6. je, hayo maandamano yakiitishwa, utakuwa tayari kushiriki?
7. vipi kama serilaki ya chama unachokiunga mkono (kilicho kwenye damu yako) kikisema hayo maandamano yanahatarisha amani na yanalenga kumuondoa mwenyekiti wa chama chako madarakani, bado utakuwa radhi kushiriki?

binafsi naomba unisaidie hayo tu

asante mpendwa

ndugu kuwa mwanachama wa chama fulani hakunizuii mimi kushabikia cha kingine hasa kinachoonesha kuwa upande wa wananchi, mimi ninachoangalia ni maendeleo ya taifa na watu wake. Nina uhuru wa kushabikia chama chochote, sijameza hirizi za ccm ndugu yangu, na ccm si sakrament ya ndoa kwamba huwezi kuitema.
 
1. ccm damu maana yake nini?

2. unawezaje kukiunga mkono chama kimoja na ukaamini kuwa unaweza kuhudumiwa na chama kingine?
3. huko ccm umepigwa pingu au kabali kiasi kwamba huwezi kuponyoka?
4. hizo fedha zikitengwa na kusimamaiwa na mafisadi wewe unadhani utafikiwa na sh ngapi?
5. yale mabilioni ya mwanzo ya kikwete binafsi zilikufikia sh ngapi?
6. je, hayo maandamano yakiitishwa, utakuwa tayari kushiriki?
7. vipi kama serilaki ya chama unachokiunga mkono (kilicho kwenye damu yako) kikisema hayo maandamano yanahatarisha amani na yanalenga kumuondoa mwenyekiti wa chama chako madarakani, bado utakuwa radhi kushiriki?

binafsi naomba unisaidie hayo tu

asante mpendwa

Judi, kwa namna nyingine Chadema ni kama nyumba ndogo, unaifikiria ukiwa na mahitaji fulani tu na wala siyo kama familia.
Amini kuwa kati ya wapenzi 100 wa Chadema utakaowaona kwenye tv kati yao kuna wanaccm damu na iko kwenye akili zao kuwa chadema na uongozi wa nchi ni kama maji na mafuta au mbingu na ardhi.
Hivi umewahi kujiuliza kwa nini Saboda hachukui kadi ya Chadema?!!
 
ndugu kuwa mwanachama wa chama fulani hakunizuii mimi kushabikia cha kingine hasa kinachoonesha kuwa upande wa wananchi, mimi ninachoangalia ni maendeleo ya taifa na watu wake. Nina uhuru wa kushabikia chama chochote, sijameza hirizi za ccm ndugu yangu, na ccm si sakrament ya ndoa kwamba huwezi kuitema.

Judi, kwa namna nyingine Chadema ni kama nyumba ndogo, unaifikiria ukiwa na mahitaji fulani tu na wala siyo kama familia.
Amini kuwa kati ya wapenzi 100 wa Chadema utakaowaona kwenye tv kati yao kuna wanaccm damu na iko kwenye akili zao kuwa chadema na uongozi wa nchi ni kama maji na mafuta au mbingu na ardhi.
Hivi umewahi kujiuliza kwa nini Saboda hachukui kadi ya Chadema?!!

mimi pia si mwanchadema wala mwanasiasa kwa kiwango chochote, lakini nadiriki kusema kuwa, watu kama nyie akiwamo huyo role model wenu sabodo (nataka-sitaki) ndio manochelewasha ufanisi wa nguvu ya umma

unapenda chadema waandamane, lakini wakiitisha maandamano hutoki ndani, ukisikia yale ya ccm yameitishwa, huyoooo na shati lako la kijani! ukitaka hela za mikopo (baada ya kupigwa bao na wenye visu kikali huko ccm na wewe kuishia kushangilia tu bila kuambulia hata senti), unaigeukia chadema ikusaidie kupata mkopo! wala huulizi mabilioni yale ya JK yaliisjia wapi, unataka chadema wakuulizie kupitia maandamano, huku wewe ukiandamana upande wa ccm!

kuna kitu hapo sio bure!
 
Unajua hata mm kwa kweli nawashangaa sana wabunge wa mcc maana juzi watu wanatoa point za maana mwangalie Tundu Lisu alivyokua anauchambua vizuri ule mfuko wa mahakama sasa ikifika mahali wamuunge mkono kwa ndioooo unasikia siooo sasa hapo kabisa unaona wabunge hawapo kitaifa wapo kichama zaidi.inakera sana
 
ndugu kuwa mwanachama wa chama fulani hakunizuii mimi kushabikia cha kingine hasa kinachoonesha kuwa upande wa wananchi, mimi ninachoangalia ni maendeleo ya taifa na watu wake. Nina uhuru wa kushabikia chama chochote, sijameza hirizi za ccm ndugu yangu, na ccm si sakrament ya ndoa kwamba huwezi kuitema.




ha ha ha hah hayo maneno nimeyapenda na yamenifurahisha sana........
 
Hao wabunge wako wa sisi em wenyewe wanawaza matumbo tu na kukashifu cdm hawana hoja wala mashiko! Hata miswaada muhimu wachangiaji wakuu ni chadema.....mimi nazani chaguzi zijazo cdm ipewe nchi
 
Back
Top Bottom