BUBE
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 846
- 253
Kwani CDM ni hao tuuu? Wakitoka itakufa ama itaendelea?
Niliwahi kumnukuu Stephen M. Wassira akisema kuwa chadema ni cha msimu na kitakufa kabla ya 2015. Nilimwona huyu mzee amechanganyikiwa na anatapatapa kama mfamaji. Sasa naweza sema nakubaliana na Wassira na pengine kwa kauli yake hiyo alijua kinachofanyika kati ya CCM na baadhi ya wasaliti ndani ya chadema. Tangu leo tujue kuwa msaliti ndani ya cdm si zitto na shibuda tu bali kuna orodha ndefu ambayo kila kukicha inaongezeka. Inaandaliwa na ccm kwa umakini mkubwa na baadhi yao wameanza kuonesha utii kwa ccm kwa kutoa siri za chadema kwa ccm. Hivi juzi, niwaibie siri(kama si kweli Slaa aikanushe.) Slaa alihojiwa incamera na wazee wa system baada ya kupatikana kwa traces zinazomwonesha Slaa akiwa Italy mwezi Agost 2012 akizungumza na Italy Mafia Mob (ITAMM) ili iwafundishie snipers na sharpshooters kwaajili ya uchaguzi mkuu 2015. Mwanzoni alikataa japo alikuja kukubali baada ya kuoneshwa mkanda wa video Dr Slaa akiwa airport Dar, akiwa mapokezi uwanja wa ndege Rome na akiwa Foret de Mafia Italiano akizungumza na master wa Mafia d'Italiano. Slaa anadaiwa kuikataa sauti na kudai kuwa video ni fabricated. Hata hivyo Slaa anadaiwa kumlaumu askofu mmoja mwanza kuwa ndiye aliyevjisha siri hiyo kupitia kwa Halima mdee ambaye anadaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na kigogo mmoja wa system. Inadaiwa askofu huyo haelewani na Slaa tangu akiwa katibu wa TEC hivyo amefanya hivyo kumkomoa Slaa baada ya Slaa kumtuhumu kuwa alihamishiwa hapo
ili kuisaidia ccm. Katika Mazingira hayo ni wazi kuwa Wassira anajua jinsi watakavyoimaliza chadema, ana uhakika asilimia 100. Zaidi ya Zitto ambaye ndiye anaonekana msaliti, yeye ni kiongozi tu lakini nyuma yake kuna shibuda, shushushu mabere marando, halima mdee, sugu, wenje, mbunge ester, kasulumbai, selasini na vicent nyerere. Mkubali msikubali ukweli ndo huo ingawa ni mchungu.