Njowepo
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 9,710
- 2,226
Viongozi kitaifa wakacha kumbukumbu Butiama
na Sitta Tumma, Butiama
MAADHIMISHO ya miaka 11 ya kifo cha hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jana yaliingia doa baada ya kiongozi wa kitaifa hata mmoja kutoonekana nyumbani kwake, kijijini Butiama kwa ajili ya kuungana na familia yake.
Kitendo cha kiongozi wa kitaifa hata mmoja kutofika Butiama kilionekana kuwashtua wakazi wa kijiji hicho ambao walihudhuria misa iliyofanyika Kanisa Katoliki Butiama kabla ya maandamano ya kuelekea nyumbani kwake eneo la Mwitongo.
Hali hiyo, iliibua minongono mingi kwa baadhi ya wananchi waliohudhuria kumbukumbu hiyo, huku Mhashamu Baba Askofu wa Jimbo Kuu la Musoma, Marco Msonganzila, akilaani kitendo hicho.
Katika misa ya maombezi, iliyohudhuriwa na Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, ambaye kwa namna moja au nyingine ni ndugu wa karibu.
Wengine waliohudhuria ni baadhi ya viongozi wa ngazi za chini mkoani humo; baadhi ya watu walieleza kuwa kitendo cha viongozi wa serikali ngazi ya kitaifa kutohudhuria maadhimisho hayo ni ishara ya kuasi mambo mema na muhimu yaliyofanywa na mwasisi huyo wakati wa uhai wake.
Akitoa nasaha wakati wa mahubiri, Askofu Msonganzila alisema siasa chafu na uchu wa madaraka zimeanza kuhatarisha amani ya nchi.
Alisema inasikitisha kuona baadhi ya vyama kuanza kutamba kwa kusema ushindi ni lazima.
Hivi sasa nchi yetu imeingiliwa na siasa chafu zenye tamaa, uchu wa madaraka, fitna na ubinafsi kinyume na alivyotaka Nyerere?! alishangaa askofu huyo.
Kutokana na hali hiyo, Askofu Msonganzila alisema ghasia na vurugu za kisiasa zinazojitokeza sasa zimelenga kuleta machafuko ya kivita iwapo hazitadhibitiwa.
MY TAKE
Naona wamedhamilia kuzika kila kilicho cha Mwalimu kuanzia vitu mpka fikra zake no wonder wameshaanza mwaga damu uku Tarime na Hai kwa kutumia green guard
na Sitta Tumma, Butiama
Kitendo cha kiongozi wa kitaifa hata mmoja kutofika Butiama kilionekana kuwashtua wakazi wa kijiji hicho ambao walihudhuria misa iliyofanyika Kanisa Katoliki Butiama kabla ya maandamano ya kuelekea nyumbani kwake eneo la Mwitongo.
Hali hiyo, iliibua minongono mingi kwa baadhi ya wananchi waliohudhuria kumbukumbu hiyo, huku Mhashamu Baba Askofu wa Jimbo Kuu la Musoma, Marco Msonganzila, akilaani kitendo hicho.
Katika misa ya maombezi, iliyohudhuriwa na Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, ambaye kwa namna moja au nyingine ni ndugu wa karibu.
Wengine waliohudhuria ni baadhi ya viongozi wa ngazi za chini mkoani humo; baadhi ya watu walieleza kuwa kitendo cha viongozi wa serikali ngazi ya kitaifa kutohudhuria maadhimisho hayo ni ishara ya kuasi mambo mema na muhimu yaliyofanywa na mwasisi huyo wakati wa uhai wake.
Akitoa nasaha wakati wa mahubiri, Askofu Msonganzila alisema siasa chafu na uchu wa madaraka zimeanza kuhatarisha amani ya nchi.
Alisema inasikitisha kuona baadhi ya vyama kuanza kutamba kwa kusema ushindi ni lazima.
Hivi sasa nchi yetu imeingiliwa na siasa chafu zenye tamaa, uchu wa madaraka, fitna na ubinafsi kinyume na alivyotaka Nyerere?! alishangaa askofu huyo.
Kutokana na hali hiyo, Askofu Msonganzila alisema ghasia na vurugu za kisiasa zinazojitokeza sasa zimelenga kuleta machafuko ya kivita iwapo hazitadhibitiwa.
MY TAKE
Naona wamedhamilia kuzika kila kilicho cha Mwalimu kuanzia vitu mpka fikra zake no wonder wameshaanza mwaga damu uku Tarime na Hai kwa kutumia green guard