CCM wajiandaa kujibu kauli ya Anne Kilango kuhusu kuogopa mafisadi

WAKATI tayari baadhi ya vigogo wakiwemo mawaziri wa zamani wanaburuzwa mahakamani kwa tuhuma za ufisadi na kutumia vibaya madaraka, Rais Jakaya Kikwete, amesisitiza mbele ya jumuiya ya kimataifa kwamba, vita bado ni mbichi.

Kauli ya Rais imekuja wakati Watanzania wakisubiri kuona watuhumiwa zaidi wakiwemo wenye tuhuma mbalimbali za ufisadi, wakiburuzwa mahakamani huku serikali ya awamu ya nne ikisifiwa hadi katika anga za kimataifa kutokana na kuimarisha utawala bora.

Akijibu swali la mmoja wa waandishi kutoka nje mara baada ya maazimio ya Mkutano kati ya Afrika na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), aliyetaka kujua mchakato wa vita dhidi ya rushwa, Rais Kikwete alisema bado unaendelea.

"Vita dhidi ya rushwa inaendelea, ni kweli tumekuwa tukipambana na tatizo hilo, lakini bado tunaendelea," alisisitiza juu ya msimamo huo mbele ya Mkurugenzi Mkuu wa IMF Dominique Strauss-Kahn.

Rais kwa ufafanuzi zaidi, alisema vita dhidi ya rushwa ni wajibu wa serikali kuhakikisha inadhibitiwa.

"Vita dhidi ya rushwa ni wajibu wetu, tunapaswa kupambana na rushwa, tumekuwa tukipambana na bado tunapambana," aliongeza Rais.

Tayari vita dhidi ya ufisadi imeonyesha mafanikio kwa kuwafikisha mahakamani baadhi viongozi wakiwemo aliyekuwa Waziri wa Fedha Basil Mramba, Nishati na Madini Daniel Yona na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi, Grey Mgonja

Mbali ya hao, pia tayari watuhumiwa wengine akiwemo mfanyabiashara maarufu nchini Jeetu Patel na wengine wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Fedha za Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT).

Pia tayari, aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa BoT, Amatus Liyumba, amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuishauri serikali vibaya na kuingizia hasara ya zaidi ya sh 200 bilioni katika mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo.

Katika hatua nyingine, Rais alisema serikali imejipanga kupunguza utegemezi wa misaada kutoka kwa nchi wahisani.

Akijibu swali la pili la mwandishi huyo wa kigeni aliyetaka kujua kikomo cha Tanzania kutegemea misaada ya wahisani, Rais alisema ni vigumu kueleza kikomo, lakini nia ni nchi kujitegemea.

"Unauliza kikomo, nasema tumekuwa tukijitahidi kupunguza utegemezi wa nchi wahisani, lengo ni kuweza kujitegemea zaidi katika bajeti yetu," alifafanua Rais.

Alisema serikali imekuwa ijjitahidi kutumia rasilimali za ndani, kuhakikisha inaweza kujijengea uwezo zaidi wa kujitegemea.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mkuu Mfuko wa Kuuza Mazao Nje (CFC) Balozi Ali Mchumo, alisema pamoja na nia nzuri ya IMF na jumuiya ya kimataifa kuisaidia Afrika, ni vema sasa ikatangaza namna bora ya kuhakikisha inakuwa na mipango ya dharura kuzisadia nchi za Afrika.

Kwa mujibu wa Mchumo ambaye alikuwa mmoja wa wageni waliohudhuria mkutano kati ya Afrika na IMF, kujadili namna ya kujinusuru na mgogoro wa kifedha duniani, alisema nchi za magharibi zimekuwa zikitoa fedha kuokoa taasisi zao.

Balozi Mchumo alifafanua kwamba, iwapo hakutakuwa na mipango hiyo na ikatokea taasisi za fedha katika nchi za Afrika zikaanguka, Wizara za Fedha hazitaweza kutoa fedha kuzinusuru kama inavyofanya mataifa ya magharibi.

"Nafikiri dhamira ya IMF na mashirika mengine ni nzuri tu, lakini wangekuwa na mpango wa dharura kama ambavyo Rais Kikwete ameamua kuunda Task Force (Kikosi Kazi), kuangalia athari hizo," alisema Balozi Mchumo na kuongeza

" Kwa maana, kule ulaya na Marekani tunasikia wao wanatoa mabilioni kuokoa mabenki yao, huku kwetu Afrika ikifikia hali hiyo Wizara zetu za Fedha hazitaweza kufanya hivyo,".

Mkutano huo ambao ulihudhuriwa na washiriki zaidi ya 300, wakiwemo mawaziri na magavana wa nchi za Afrika na viongozi wengine maarufu akiwemo Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa (UN) Dk Kofi Annan na mfanyabiashara maarufu Mo Ibrahim, ulimalizika jana baada ya kujadili mambo mbalimbali kuhusu namna Afrika inavyoweza kujinasua na anguko la uchumi wa dunia.

Source: Mwananchi
 
mwache huyu mpayukwaji anatapatapa hapo alipo hajui hata analofanya, keshaanza kigugumizi hata 2010, bado anafkiri watu wata sahau, na waje 2010 watueleze walivyotupora waone,"makofi matupu".
 
mwache huyu mpayukwaji anatapatapa hapo alipo hajui hata analofanya, keshaanza kigugumizi hata 2010, bado anafkiri watu wata sahau, na waje 2010 watueleze walivyotupora waone,"makofi matupu".

Cha ajabu kuna baadhi ndani ya CCM wakiwemo Wabunge ambao wameshasema kwamba Makamba aondolewe kwenye nafasi ya ukatibu Mkuu kwa sababu amekuwa ni liability kubwa ndani na nje ya chama, lakini bado anaendelea kuachiwa abwabwaje tu.
 
Je ni kweli sera ya kupambana na mafisadi ndio imeshatoka ? Kwa mujibu wa Makimba kuwa vita vya mafisadi vimeshapitwa na wakati..! .
Hayo matusi yako ya reja reja kwa CCM naona sasa yanazidi! Nimejaribu kuangalia herufi A na I kwenye key board zipo mbali mbali! Hivyo usisingizie kukosea kuchapa!
 
Wanabodi,
KAULI ya Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango kuwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaogopa kupambana na ufisadi kwa kuwa mafisadi ni viongozi wenzao, inaonekana kukikera chama hicho na sasa kinaandaa taarifa maalum kujibu mapigo.
Maneno ya mama Kilango ni mazito sana na ukiyapima utakuja gundua kwamba Tatizo la nchi yetu ni mfumo mzima wa Utawala wa nchi yteu.

Kama nchi yetu ingelikuwa ni nchi yenye Demokrasia ya kweli na nchi ambayo imeacha mfumo wa chama kimoja nyuma, swala hili lisinge subiri CCM kupambana na Ufisadi..Au kwa lugha nyingine lawama hizi hazitakiwi kupitia CCM badala ya serikali kwani Ufisadi ni crime!..na sii jukumu la chama kilichopo madarakani kupambana na criminals..

Sasa basi ikiwa CCM ndio serikali na serikali ndio CCM naelewa vizuri maneno ya Mama Kilango kwani unapotazama list ya Viongozi wa CCM ndio hao hao viongozi wa serikali, hivyo basi tafsiri kamili ya maneno ya mama Kilango kwamba Viongozi wa CCM wanaogopa kupambana na Ufisadi kwa sababu Mafisadi ni viongozi wenzao..
Ina maana, Kikwete, Malecela na.... wanaogopa kupambana na Ufisadi kwa sababu mafisadi ni (viongozi wenzake) kina Mkapa...

Endelezeni list ya Mafisadi ktk Uongozi wa CCM.
 
FMES Sauti ya umeme yupo Easter anapombeka siasa kwaweka kando!

- Yeah! Yeah! Mazee Masa, you got it right wazee vipi vipi hapa? Unajua nilikuwa ma-trip kidogo na pia kutoa nafasi ya heshima kwa Mwenyezi Mungu, unajua tena yeye ndio mambo yote, okay sasa ngoja kwanza nipitie pitie threads nione tulikoachia na tulipo,

- Otherwise, safari ilikuwa njema sana na kama kawaida tumekutana na ma-JF, unajua siku zote I am a proud member of JF na huwa ninawatafuta kwanza member wa JF popote pale ugenini, ninawashukuru wote tulionana jana na leo asubuhi, na sasa nice to be home tena, home sweet home.

Wakulu wote ninatumaini kwamba tulikuwa na Pasaka njema sana, sasa ni wakati wa kurudi tena kwenye ishus na taifa mbele.

Respect.

FMES!
 
Mzee Makamba anadai kuongelea ufisadi ni kupitwa na wakati, je ina maana tufumbie macho, kaza mguu twende tuvumilie kuhujumiwa?

Je hilo ndilo tamko rasmi la CCM kwa Watanzania kuwa kuongelea Ufisadi na kufunua maovu ni kupitwa na wakati? Hata kama atadai ndivyo ndani ya CCM, haoni kuwa ni kudanganya umma wa Wanachama wa CCM milioni tano ambao wengi wao anaishi katika umasikini wa hali ya juu kutokana na matumizi mabaya ya hazin yaliyotokana na Ufisadi?

Tusipoligangamalia suala la Ufisadi kama tulivyogangamalia Ukoloni mpaka ukaondoka, je CCM na Mzee Makamba hawaoni kuwa tutaendelea kunyonywa na kutawaliwa na mafisadi daima?
 
Mzee Makamba wangekuwa wamemsaidia kwa kiasi kikubwa kama wangemuacha kwenye level ileile ya ukuu wa mkoa.Ana matatizo sana katika kuchagua maneno azungumzapo.Lakini maadam wameamua kumbeba,na waendelee maana hawachelewi kusema 'pilipili ya shamba...'.Ila ukweli utabaki kuwa viatu alivyovaa ni vikubwa sana kwake.Period
 

"Nchini Marekani mtu aliyetaka kurithi nafasi ya useneta wa Obama alitanguliza rushwa ili kuwashawishi wajumbe, jambo ambalo liliwafanya Wamarekani kusimama imara na kuzungumza ukweli kuhusu kashfa hiyo," alisema Kilango ambaye alipata tuzo ya ‘Mwanamke Jasiri' aliyopewa na Serikali ya Marekani hivi karibuni.
Ha hahhaaaaaaaaaa.....Mama Kilango usitake kunivunja mbavu zangu we Mama we hahahaa aaaaha

Nani aliyetaka kurithi kiti cha ubunge cha Obama aliyetanguliza rushwa?

Yuko wapi sasa hivi huyo mtu, bungeni au jela? Bub bub bwa ha hahaaa aaaaaaaaaaaa
 
Ha hahhaaaaaaaaaa.....Mama Kilango usitake kunivunja mbavu zangu we Mama we hahahaa aaaaha

Nani aliyetaka kurithi kiti cha ubunge cha Obama aliyetanguliza rushwa?

Yuko wapi sasa hivi huyo mtu, bungeni au jela? Bub bub bwa ha hahaaa aaaaaaaaaaaa


- Bwana Buriss alitanguliza hongo na sasa anatakiwa ajitoe kwenye kiti hicho cha Obama, mkuu unachekesha sana BW!! ha! ah! mama kabla hajaongea huwa anafanya homework.

Respect.

FMES
 
- Dilunga soma hii chini acha kukurupuka mkuu, mama hufanya homwork kwanza unaona aibu yako hapa sasa omba radhi kwa forums:-



The Monumentally Egomaniacal Senator from Illinois

Roland Burris, what are you thinking?


Terence Samuel | February 20, 2009 | web only



If we were talking about anyone else, I'd say that by the time President Obama goes before the Congress on Tuesday to deliver a speech in lieu of the State of the Union, the man appointed to replace him in the Senate will have resigned, deciding, in the best interests of his state, his party, and his country, to return to the obscurity of his private life.

But since we are talking about the monumentally egomaniacal Roland Burris, the chance of this development is close to zero. Burris, who rode into the Senate on the strength of one of the most cynical, race-based political ploys of all time, is having a hard time seeing the trouble he's in. Accusations of lying to a state impeachment panel about his contacts with disgraced former Gov. Rod Blagojevich have sparked an investigation by the Senate Ethics Committee to go along with state probes back in Illinois. But Burris is as desperate to keep the title of senator before his name as he was to get it there in the first place. The likely result is that for weeks to come, we will be hearing more gory details about how deeply entangled Burris was in the pay-for-play schemes that led to the arrest of Blagojevich on corruption charges.

After insisting that there were never any discussions between him and Blagojevich about political favors in exchange for the Senate seat, Burris, in recent days, has amended and extended his response to those questions to admit that, well, there were some. First, the governor's brother asked him for a contribution to Blagojevich's re-election campaign, and then, Burris admitted, he did try to raise money for the governor, all the while making sure that his interest in the Senate seat was known.

It is tawdry enough that his hometown newspaper is leading a charge calling for Burris to resign, but the senator, whose narcissism is notable even in political circles, will see it as an act of courage to defy those calls. And it'll get tawdrier and tawdrier. I suspect that at some point, the president will have to distance himself from his old Senate seat. It's difficult to imagine any scenario in which Burris simply steps down. It may take direct urgings from the White House to get Burris to go.

Democrats desperately need that seat and that vote, as the roll call on the stimulus package showed, but Burris is becoming a larger embarrassment everyday.

Ironically, these recent developments are ultimately helpful to the Democrats -- whatever happens in the short term, Burris is out of the 2010 equation. While there may still be a heated primary, the Burris implosion will allow Democrats to wage a battle for the seat without having to worry about how to handle a problematic incumbent.

Burris, 71, had pledged to seek re-election next year, which worried many Democrats who believed that he couldn't win. But they were concerned, fairly, about the political risk involved if they are perceived to be throwing an incumbent senator, and the only African American in the Senate, under the bus.

The same political discomfort that complicated the debate about whether to seat Burris in the Senate after he was appointed by the tainted Blagojevich was likely to reappear in the re-election fight, and there was no guarantee that Burris would handle it any better then he did a month ago. Burris' actions will relieve some of that pressure. Even if he survives and remains in the Senate through the end of next year, he will have no chance of mounting a viable campaign for re-election. He will have no money and no natural base.

The tragedy of Roland is that he cheaply ruined his chance to live out his dream of being in high office -- he ran for governor twice -- and to quietly add some sheen to an otherwise ordinary political career. Ego alone made him one of the few, maybe the only person, who would have accepted an appointment from Blagojevich under the circumstances. Blagojevich decided to play the race card against a Senate leadership who said it would not seat anyone he appointed, and it worked, because he had Burris to play along.

As I noted back then, the story was never really about Burris; it was about Blagojevich and Harry Reid and his all-white Senate. Against that backdrop, there was no reason for Burris to lie about his relationship with Blagojevich. Now that he has, the story is about him, and like Blagojevich, he is not likely to survive it.
 
baada ya kupewa tuzo anna kilango malecela kaamua kupambana na mafisadi wa usa? anna atakuwa amechanganyikiwa huyu. buriss na blugoyevish wanahusika na nini bongo? anna kilango malecela kwanze ajitangaze yeye kwa ufisadi wa kuiba fedha za gulf airways.
 
baada ya kupewa tuzo anna kilango malecela kaamua kupambana na mafisadi wa usa? anna atakuwa amechanganyikiwa huyu. buriss na blugoyevish wanahusika na nini bongo? anna kilango malecela kwanze ajitangaze yeye kwa ufisadi wa kuiba fedha za gulf airways.

Kumbe ilikuwa inaitwa gulf airways, i thought ni Gulf Air.......Acha vijembe kwa mama, ile ilikuwa ni kazi ndogo, tu-support harakati sio kuingiza visivyohusika.
 
Huu mtindo wa kujificha kwenye mwamvuli wa kupiga vita ufisadi utaisha lini?nina hakika hata maana halisi ya neno "Fisadi" haijulikani na wengi.Ni nchi za kinyonge kama bongo ambazo unaweza kuwahadaa wananchi kwa patriotism za aina hiyo.Huyu mama na wengine wana hofu ya kutetea viti vyao vya ubunge tu, na tutasikia mengi tuu.Muulize kafanya nini jimboni kwake?atatoa kope kama fundi saa aliyepoteza mshale wa sekunde.
 
kupombeka ndo nini tena? ok kwa jinsi ninavyoona wote tumeshapombeshwa na ccm, manake utadhani hakuna njia mbadala katika kukomboa nchi yetu bila ccm
 
Back
Top Bottom