bullet proof
Member
- Sep 19, 2012
- 57
- 35
Wakati ambapo ni dhahiri CHADEMA kimedhamiria kuharibu amani na utulivu, ambavyotumekuwa tukijivunia tangu historia ya nchi hii na kupigiwa mfano kwa nchi jirani, chama cha mapinduzi (CCM) kimesema daima kitahubiri amani na mshikamano wa watanzania.
"Kulazimisha kuingia madarakani kwa gharama za damu na maisha ya watanzania ni uchu wa madaraka ambao lazima watanzania waukatae", alisema kiongozi mmoja wa CCM kata ya Bangwe, Kigoma.
Wakati huo huo baadhi ya vijana, waliojitambulisha kama wanachadema, wameongeza kuwa licha ya kuwa maendeleo yanakuja taratibu sana nchini lazima amani ilindwe kwani ndio msingi wa maendeleo.
Vijana hao wamewataka wanasiasa kujifunza siasa za kiungwana na kumtaja mh ZITTO (chadema) kama mfano wa wanasiasa waungwan.
"Kulazimisha kuingia madarakani kwa gharama za damu na maisha ya watanzania ni uchu wa madaraka ambao lazima watanzania waukatae", alisema kiongozi mmoja wa CCM kata ya Bangwe, Kigoma.
Wakati huo huo baadhi ya vijana, waliojitambulisha kama wanachadema, wameongeza kuwa licha ya kuwa maendeleo yanakuja taratibu sana nchini lazima amani ilindwe kwani ndio msingi wa maendeleo.
Vijana hao wamewataka wanasiasa kujifunza siasa za kiungwana na kumtaja mh ZITTO (chadema) kama mfano wa wanasiasa waungwan.