CCM tupo katika mwanguko mkubwa

Burigi

Member
Jan 11, 2011
45
81
Watanzania wenzangu wana CCM wenzangu leo hii napenda kutoa ukweli mchungu ambao wenzetu hawataki kuusema aidha kwa makusudi ili liwalo na liwe, au kwa woga wa madaraka,au kuogopa kuwaudhi wakubwa au kwa faida ya matumbo yao wasiharibu nafasi na vyeo vyao hivyo wote tupo kimya kila mtu anamtazame mwenzake asijue lakufanya tupo katika mwanguko mkubwa wa chama chetu cha CCM.

Wana ccm wenzangu leo hii chama chetu hakina mkubwa wala mdogo wote tumekuwa kambale huu ni mwanguko mkubwa mfano ni bungeni wabunge wetu ndiyo wamekuwa wakijibu tuhuma za serikali badala ya kuibana serikali huu ni mwanguko ulio dhahiri.

Wana ccm wenzangu leo wabunge wetu wameamua kuwaachia vijana mahiri wa upinzani kuwasemea wananchi na wao wamebaki kupiga kelele za ndiyo na kutetea uovu wa serikali huu ni mwanguko mkubwa kwa chama chetu cha ccm.

Chama chetu bungeni huwezi kumtofautisha mbunge na waziri wote wamekuwa watetezi wa maovu ya serikali hili ni mwanguko mkubwa wana ccm wenzangu.

Vijana wetu mahiri wengine kama wachumi nambari moja kina Mwigulu mchemba yeye akisimama ananza kutukana ,CHADEMA, DR slaa ambaye hata bungeni hayupo ,MBOWE na wapinzani wakati vijana wa upinzani wanaogelea kwenye hoja na matatizo makubwa ya wananchi wana CCM wenzangu hili ni anguko kubwa ni mwanguko mkubwa

Wana CCM wenzangu mawaziri wetu wamefikia hawana hata uwezo wakujibu maswali kuanzia waziri mkuu na mawaziri wake hivi sasa wanatumia asilimia 90 ya mda wao kuwa attack wapinzani badala ya kujibu hoja murua na maridadi za wapinzani huu ni mwanguko mkubwa wana ccm wenzangu .

Wana CCM wenzangu spika na naibu wake wanasaidia kukiua chama chetu kwa kuwawekea kinga wajibu maswali ya umma hasa mawaziri kwa kuruhusu majibu yasiyokidhi haja ya wauliza maswali huu ni mwanguko mkubwa kwa chama chetu.

Wana ccm wenzangu spika wetu kupendelea chama chetu kwa wazi kabisa na naibu spika kuonyesha waziwazi hawapendi upinzani huko ni kuwapa wapinzani nguvu na mashabiki wengi nje ya uwanja na kutudhoofisha chama chetu huu ni mwanguko mkubwa wana ccm wenzangu.

Wana ccm wenzangu wabunge wetu hawawezi kujenga hoja tena kazi yao ni kupiga makofi na kuitikia ndiyoooooooooo.... HUU NI MWANGUKO MKUBWA WANA CCM WENZANGU.

Hata pale spika anapopunguza nguvu za upinzani kwa kuwapa adhabu eti kwa kuomba muongozo lakini wabunge wetu na mawaziri wetu bado hawawezi kukabili na kujibu hoja za wapinzani wanne tu kama ilivyokuwa alhamisi hoja ya wizara ya utawala bora ya waziri wassira na Kombani, mawaziri karibu sita mwanasheria mkuu na wabunge wote wa CCM walishindwa kujibu hoja za msingi kabisa toka kwa vijana mahiri wa upinzani mh.Mkosamali, HAlima Mdee, Mnyika na mzee wao professor Kahigi kwa walioshuhudia chama chetu kilishindwa kujibu hoja za msingi wabunge wetu na mawaziri wetu walishinda hoja ile kwa kura za ndiyoooo huo ni Mwanguko mkubwa wana CCM.

Wana CCM wenzangu ninaona mwanguko wa chama chetu ni kama UNIP ya mzee wetu KAUNDA au KANU ya mzee wetu MOI Tupo katika mwanguko mkubwa.

Wana ccm wenzangu chama chetu kinapowatetea watumishi waandamizi kabisa wa UMMA wa vyombo vya usalama wametuhumiwa katika kashfa kubwa kabisa na kuwaachia waendelee na kazi wakiwa katika kashfa nzito namna hiyo huo ni mwanguko mkubwa wa chama chetu na serkali yetu pia.

Wana ccm wenzangu inapofikia chama hakiwezi kufanya mkutano bila kuwahonga wanachama wetu kwa kanga kofia na kuwanunulia vyakula huo ni mwanguko mkubwa tena mwanguko mbaya sana.

Wana ccm wenzangu inapofikia ili kufanya mikutano inabidi tu import watu kwa maroli kuwaleta sehemu ya mkutano ili tujaze uwanja au ukumbi huku ni kujidanganya na hili ni anguko ni anguko kubwa sana huu ni mwanaguko ulio dhahiri.

Wana ccm wenzangu inapofikia hoja ya mbunge mmoja wa upinzani inajibiwa na mawaziri na wabunge wote wa chama chetu na bado haijitoshelezi hilo ni anguko ni mwanguko mkubwa.

Wana ccm wenzangu tupo katika mwanguko mkubwa mwanguko mkubwa mwanguko mkubwa sana....

Wana ccm wenzangu hatuna wabunge wawakilishi wa wananchi na nchi tuna makada ambao kazi yao ni kuwajibu wapinzani hata katika zile hoja za msingi kabisa na za wazi wabunge wetu wao kazi ni kuwajibia mawaziri huwezi kujua mbunge wa chama chetu ni yupi na waziri we serikali ni yupi wote wamekuwa wakiijibia serikali hili ni anguko huu ni mwanguko mkubwa na 2015 utakuwa ni mwanguko mkubwa sababu wananchi watataka kupeleka wabunge watetezi wao na si watetezi wa dola.

Wana ccm wenzangu huu ni mwanguko mkubwa chama kubakia na wabunge wawili tu wawakilishi wa wananchi chama kuwakilishwa na Deo filikunjombe na Kange lugola pekee yao hili ni anguko ni anguko kubwa huu ni mwanguko wote tu mashahidi wa mashujaa wetu hawa wanavyotetea maslahi ya umma na siyo watu wa nddiyooo .

Tupo katika mwanguko wana ccm wenzangu chama chetu kinaangushwa kwa maslahi ya kwao tumekubali kuangushwa huu ni mwanguko mkubwa.

wana CCM wenzangu wabunge wetu wamechanganyikiwa kabisa husimama kwa kuponda hoja zilizotolewa na upinzani tena zile zenye maslahi kwa Taifa, hapo hapo anaunga mkono hoja kwa asilimia mia moja 100% lakini hapo hapo huitoa kasoro na kuonyesha mapungufu ya hoja hiyo wana ccm wenzangu kama kitu kina kasoro kinaweza kuungwa mkono mia kwa mia huu ni mwanguko mkubwa kwa chama chetu.

Wana ccm wenzangu kuwanyima wapinzani viwanja vya kusemea kuwazuia mikutano yao bila sababu huku ni kuwaunganisha zaidi wapinzani na wananchi na huku ni kujihujumu wenyewe wanaofanya hivyo wanasaidia huu mwanguko na wamedhamilia kutuangusha.

Wana ccm wenzangu huko mawilayani kuwatumia ma RPC,OCD ,RC's na maDCkuzuia mikutano ya wapinzani kunajaza sana mori wananchi kuhisi wanahitaji ukombozi wa kuwatimua hao wakoloni weusi na kufanya chama chetu kizidi kuchukiwa hawa watu hawatusaidii ni sehemu ya mwanguko wetu.

Wana ccm wenzangu viongozi wetu wamekuwa ni kundi la kulindana hata inapotakiwa mmojawapo kuwajibika kwa heshima ya chama na serikali yetu hawako tayari kufanya na watatea kwa nguvu zote huu ni mwanguko tena mwanguko mkubwa.

Inapofikia waziri mkuu anatumia 90%ya mda wake kumsema tu mbowe na chadema badala yakueleza serikali imefanya na itafanya nini huo ni mwanguko tena ni mwanguko mkubwa na kama waziri mkuu ameanguka basi ndiyo wote tumeanguka tupo katika mwanguko.

Wana ccm wenzangu Kama naibu katibu mkuu wetu amekuwa akihusika kama inavyosemekana kuhonga na kununua wapinzani akifikiri ndiyo silaha ya ushindi wetu huko mbele hili ni anguko ni anguko dhahiri ni anguko lililo kubwa na kama tunataka kujenga taswira ya chama chetu kuepusha huu mwanguko basi tumpatie kazi nyingine sababu hana heshima tena mbele ya wananchi huu ni mwanguko.

Wana ccm viomgozi wetu hivi sasa hawana uwezo wa kushawishi wanachama wapya badala ya kurudisha imanai na kuendeleza misingi ya chama wao sasa hivi ni kurubuni wapinzani na kuwahonga viongozi wa upinzani na kitembea mbele uetu na makapi ya viongozi waliofukukuzwa na vyama vingine hii ni kuonyesha tumefika mwisho tupo katika mwanguko mwanguko ulio dhahiri huu ni mwanguko.

Wana ccm wenzangu tupo wengi tunaona mwanguko huu lakini tunapotoa ushauri hausikilizwi sababu chama kimekuwa genge la watu fulani hawataki mawazo nje huu ni mwanguko mwanguko uliodhahiri.

Wana ccm wenzangu tunajenga chama saa ngapi tunajibu kero za wananchi na kuzitatua saa ngapi kama kila ziara za chama utasikia inatajwa chadema na viongozi wakati chama kina mambo ya msingi hayajatekelezwa kwa miaka 50 sasa na hayana majibu sisi kila siku ni kuimba chadema, DR slaa ,mbowe nk huu ni mwanguko wana ccm wenzangu.

Wana ccm wenzangu pimeni wenyewe uelewa wa wabunge wa upinzani hotuba zao, hoja zao linganisha na wabunge wetu na mawaziri wetu mtajua kama kweli tupo katika mwanguko.

Wana ccm wenzangu wapinzani wana sema mbunge wao mmoja ni sawa na wabunge wa ccm 40 mimi ni mwana ccm mwandamizi nathubutu kusema wabunge wetu 40 na mawaziri watano ndiyo sawa na mbunge mmoja wa upinzani mwenye kubisha aangalie bunge kwa uangalifu na apime hoja za pande mbili atagundua tupo katika mwanguko.

Wana ccm wenzangu Maneno haya yatawakera wengi hasa wale wenzetu wanafiki wenye kuogopa ukweli kwa maslahi yao huu ni mkweli mchungu na lazima usemwe na wenye uchungu sababu tupo katika mwanguko mbaya.

Wana ccm wenzangu leo chama chetu kinazunguka nchi nzima kinasema CHADEMA ni chama cha kidini na kikabila wakati chama hiki kina wabunge toka mbeya, iringa , biharamulo, Mwanza, kigoma, maswa,dar es salaam kina wabunge dini zote kutuaminisha uongo wa dhahiri na kutufanya wanachama sisi ni ndondocha huu ni mwanguko mwanguko uliodhahiri.

Wana ccm wenzangu mwanguko huu hautazuiwa na polisi, wala vyombo vya usalama kama hatutakubari ukweli huu ni mwanguko mwanguko ulio dhahiri.

Watanzania wenzangu naombeni tujadili mwanguko huu katika hali ya utulivu bila kashfa sababu huu ni mwanguko mkubwa uliodhahiri namalizia kwa kusema tupo katika mwanguko.

Karibuni tujadili.
 
Kijana umena kila kitu tena kwa uchungu mkali,

ama kweli mkuu kama ni utafitiumeufanya tena wa kina ila tu ukweli ni kwamba CCMya siku hizi hakishauriki hata kwa sala na sujuda; kwa kifupi kila mmoja mle madaraka imewapanda kichwani hawasikii cha mtu na wakosoaji kutafsiriwa wa uadui wa kila nama.

Pongezi sana mkuu kwa ujasiri wote huu na kuwa mpenzi na msimamo wa kusimamia ukweli na ukweli mtupu hata iweje.
 
asante kwa kukumbushana haya mambo muhimu.

Chama cha Mwalimu Nyerere na Rashidi Kawawa, chama cha Bi Titi Mohamed na akina John Rupia, chama cha Sykes na wazee wote waliokwisha tangulia.
Sikutegemea kama mbunge wake angetamka neno 'f...y you' na spika aliye kwenye chama hicho hicho akaridhia na kusema "endelea mkuu". Wengi wetu hatukutegemea kuyashuhudia haya katika uhai wetu!
 
Sawa inabidi tukubaliane kihivo hivo tu na nyie watani zetu kwa kuwa huo ndio mkondo mpya wa demokrasia bungeni.

Lakini sasa kosa la wabunge watano kwa kambi ya upinzani ndio sasa iwe ni utakaso wa zile lugha chafu mwisho za uswahilini kwa sehemu kubwa ya wabunge wa upande wa CCM kweli ndio haki inavyokwenda kweli mtani???

Ninavyomkosa Mzee Samwel Sitta a.k.a mzee wa viwango na kasi salama bungeni, ama kweli sipati picha mimi. Naona kuna haja tena ya dharura kwake Mheshimiwa Sitta akaandae darasa la uspika kwa hawa wanagenzi au akajitwalie kabisa mkoba wake uuuupya!!!!!!

Mpaka hivi sasa ni dhahiri kwa namba SITA katika uwanja wa mpira pale bungeni inapwaya hakuna mfano wake na hivyo kulazimisha timu yetu ya maendeleo kwa taifa kucheza muda wote golini kwao bila kiungo muhimu huyu wa kuweza kuwalisha washambuliaji mahiri akina Zitto, Lema, Lissu, Sugu, ... Msigwa ... kwenda kuwafungia bao umma wa Tanzania.

Kama kuna yeyo anabisha juu ya madai haya mazito ajitokeze apate kuhesabisa si kwa povu bali hoja tu.


Kumzuia askari kufanya kazi yake ni kosa la jinai. Hao wabunge watano walifanya kosa kumkinga Lissu asitolewe nje (Sugu akawa anarap hatoki mtu, hatoki mtu hapa!), je hilo sio kosa?
 
Hali sio nzuri chama kipo ICU na nasikia wameshaanza kuchanganya dawa ya kumdunga akiwa mochuari lakini cha ajabu dawa yenyewe imegoma kuchanganyika. RIP chama changu CCM.:A S cry::A S cry::A S cry:
 
Kweli inatia uchungu! Nashundwa kuelewa kwenye vikao vya Chama kama kweli huwa wanajadiliana mambo haya. Lakini wanapaswa kuelewa kuwa watanzania wa leo si wajinga na wanaona kwani unaweza kumdanganya mtu kwa miaka 100 lakini hutafanikiwa kumdanganya siku zote. Tunaamini mungu ni mwema ipo siku nguvu ya umma ikiamua kuchagua mabadiliko ndio mwisho wa CCM na sio mbali. Ni vibaya sana kujifariji kuwa Watanzania hawajui kitu wakati ukweli wenyewe wanaujua.
 
Unapenda zaidi CCM au Tanzania? Kama unaipenda Tanzania zaidi, basi achana na hicho chama mfu. Jiunge na wa akina Mnyika ushiriki kuitoa Tanzani mikononi mwa hao CCM.
 
mkuu umenena ila subiri ritz,chama,majebele,sumu watakavyokuwakia.
 
nakupongeza Mzalendo msema kweli acha wanaojifanya mungu wao ni ccm watakiona duniani siku moja na mbinguni siku zao za mwisho maana kwa wizi wao na uzambeki hawajui kama kuna mwisho
 
WanaCCM wenzangu hiki chama chetu kila kichoambiwa wanabaki kusema umetumwa! na wadai CCM ina wenyewe..hili pia ni ANGUKO kubwa sana wana CCM wenzangu.
 
Hizi ni pumba, baada ya kuzidiwa hoja kwa vurugu zenu bungeni mmemua kujifanya wana ccm..na bado
 
Leo wote humu jukwaani mtavaa kijani bila kupenda..kinana anazidi kuwacharaza mboko za mgongo huko morogoro..
 
Embu weka hapa ushaidi kama kweli wewe ni mwana ccm . Hizi ni propaganda za kitoto . Hata mimi naweza kujisemea ni mwana TADEA kwa manufaa fulani wakati sio kweli mwana TADEA.
 
Mkiacha ugaidi na utekaji, mkaacha kuibagua zanziba na kuacha siasa za kibaguzi na kibabe mnaweza kupiga hatua lakini hadi sasa mmeloa. Mwigulu, nape na kinana wanakusalimieni
 
Kamuulize mwigulu nchemba madelu ndio atakwambia umakini wa ccm sio ukurupuke na njaa zako za kulipwa kwa thred na post uje uwahadae watu humu.mleta mada shame on you!
 
Cha cha wafu literarly,only the living could see this,and the dead well they know themselves
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom