CCM sio Nchi, Chama Kinachoongozwa na Mafisadi

Mzalendo80

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
2,508
1,338
Watanzania wanachokihitaji ni maendeleo sio porojo zenu na magamba yenu. Kujivua magamba, kujipaka rangi, kufukuza mafisadi na mambo mengine kwenye yanayohusu chama chenu sisi watanzanai hayatuhusu.
TUNACHOKIHITAJI SISI NI KAZI, BEI YA VYAKULA ISHUKE, UMEME, MAJI SAFI, BARABARA, HUDUMA ZA JAMII KAMA VILE HOSPITAL, WAZEE NA WATOTO WANAPATA TIBA BUER BILA MIZENGWE NA HUDUMA NYINGINE AMBAZO NI MUHIMU KWA BINAADAMU.
Nafikiri CCM hamjatuelewa kuwa Watanzania tunachohiji, nyinyi mnakimbilia kujivua magamba au kung’o meno wakati bado mnanuka na sumu ni ilele inayoweza kuwang’ata watanzania.
CCM SOMENI ALAMA ZA NYAKATI SIO MNAKIMBILIA KUKISAFISHA CHAMA AMBACHO KINAWAKUMBATIA WALA RUSHWA NA WAKANDAMIZAJI WA WATANZANIA.
TUNAHITAJI MENDELEO SIO MNAKIMBILIA KUJIVUA MAGAMBA YENU, TUNAHITAJI MAENDELEO YA NCHI YETU MAENDELEO MAENDELEO, MAENDELEO SIO PROJO NA VITUKO VYENU.
 
Itatugharimu FEDHA ZA KIGENI kuwaelewesha hawa!...Wana upofu fulani unaotisha!
Nape Nnauye anasema kuwa sasa wapinzani watamkoma, na ana dawa yao...my hairs:Cry::Cry:...can you imagine this?
Hivi shida yetu ni wapinzani?
Kweli kabisa siasa haitakiwi kuachwa kwa wanasiasa pekee, wanaweza kuipeleka nchi Jehanam!
 
Nilikuwa nasubiria thread ya namna hii.....
Afadhali ndugu umeliona hilo, hawa jamaa ni mabingwa wa kuwatoa watu kwenye hoja za msingi na kuingiza vitu vya kijinga jinga na vya mda mfupi, mjadala mkubwa ni kujenga taifa kitu ambacho ni wazi kimewashinda sababu kwa miaka 50 bado wanambwelambwela tu na bado eti Rais na waziri wake mkuu hawajui kwanini nchi ni masikini, sasa hapo hilo gamba litatusaidia nini hata kama likitika ingali madereva wetu hawajui tumekwama wapi sasa watatufikisha vipi huko tunakotaka kwenda (Tanzani bora).
Afu mijitu na akili yao imekazana eti ".... tunampongeza mwenyekiti kwa maamuzi magumu"
 
Back
Top Bottom