Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Nikijibu hoja ya kuhusu Rafiki yangu January Makamba kwenda Bumbuli kutoa magari, kuna mtu alitoa kauli na kuainisha kuwa January, Baba yake Mzee Makamba ni mtu mwenye ushawishi Serikalini. Nikauliza Ushawishi na kujuana kunasaidiaje mtu kuwa kiongozi mzuri, mwenye tija, juhudi, maarifa na ufanisi?
Sasa nikiwa naendelea kutafakari hilo, Wabunge wawili wameibuka na kutoa kauli kudai kuwa wao wanafaa kuendelea kuwa viongozi kutokana na jinsi walivyojenga mitandao ya ndani na nje ya marafiki ambao huwasaidia hawa Wabunge katika shughuli za MISAADA kwa majimbo yao kama sehemu ya kujipatia ujiko wa kuwa ni Urafiki wao na Kujuana na Watu ndiko kunakochangia maendeleo ya Majimbo yao.
Waheshimiwa Marmo na Kaboyonga wakijibu hoja ya Wabunge kuwekewa muda maalumu wa kuwa Wabunge walikaririwa wakisema hivi
Najiuliza, kwa vijisababu walivyotoa hawa Wabunge ambavyo narudia tena naamini ndio taswira halisi ya asilimia 95% ya Viongozi wa CCM (Wabunge, Mawaziri, Wajumbe wa NEC, CC, Viongozi wa Mikoa nk.), je tunafaida gani kama Taifa kuendelea kuamini kuwa CCM ni chama Mbadala ambacho kinaweza ifikisha Tanzania katika maendeleo ya kweli na kuvuka daraja la kuwa nchi tegemezi kwa misaada na kuushinda umasikini?
Labda niulize, jimbo la Marmo na la Kaboyonga, yamekuwa chini ya himaya ya CCM tangu tupate Uhuru. Je kila baada ya miaka mitano ambao CCM imekuwa ikinadi Wabunge na Rais katika majimbo hayo, imekuwaje kila mbunge aje na ajenda yake na mipango ya maendeleo ambayo ni huru na si kufuata mchakato wa Ilani ya Chama chao?
Ikiwa Kaboyonga anadai kuwa Tabora mjini imeshindwa kupata maendeleo kutokana na kubadilishwa Wabunge na Marmo anadai kuwa maendeleo wilayani mwake yametokana na "connections" zake binafsi, je kweli watu hawa wanafaa kuwa Viongozi na CCM inafaa kuendelea kuaminiwa?
Hivi katika majimbo ya hawa ndugu wawili, ni lini wamekwenda kuhamasisha Uzalishaji mali na shughuli za maendeleo bila kuwa ombaomba au kudai wanahitaji muda?
Je Kaboyonga anapodai kuwa miaka mitano ya kwanza ya Mbunge ni kujifunza taratibu za Bunge na Sheria, ina maana kama jimbo na Taifa tunapoteza muda na fedha zetu kama walipa kodi na kuchapa miguu (makitaimu) tukisubiri mtu, watu au kikundi ambacho kilijinadi kuwa kina uwezo wa kuongoza na kuleta maendeleo kumbe wanahitaji kupigwa twisheni?
Sasa kwa kauli ya kusema miaka mitano ya kwanza ni kujifunza kazi, kunaonyesha wazi kuwa Watu wengine hukimbiliakuwa Wabunge hata kugombea Urais bila kujua awali ni majukumu gai wanayopaswa kufanya na zaidi ni kuwa wanaupungufu mkubwa wa kiakili na sifa za uongozi kwa madai yao kuwa miaka ya mwanzo ni kujifunza kazi.
Je kuhamasisha Wananchi wachimbe mifreji, wajenge barabara, wasafishe Mazingira, wapeleke watoto shule, waongeze ufanisi na kufanya kazi kwa bidii iwe ni mashambani, viwandani au maofisini kunahitaji mafunzo ya namna gani na ya muda gani ili Wanajimbo wasikae mguu pande wakimsubiri Mbunge wao afuzu darasa la Uongozi?
Nikirudi kwenye kauli zao Marmo na Kaboyonga kuwa wao wameleta maendeleo majimboni mwao kutokana na "Connection" za ndani na nje, je ni nini tafsiri ya Maendeleo na ni maendeleo ya namna gani waliyoyaleta kwa kutumia "Connections"?
Je wanaweza kutuambia masharti ya "Connections" zao ambazo hayatafikia kuhujumu nchi au kuingiza dhululma? Je wanaweza kutuambiakuwa "Connections" hizi ni huru hazina mkono wa Takrima na ufisadi na je wao Marmo na Kaboyonga watalipa vipi Ufadhili na Fadhila za hawa "Connections" wa ndani na nje ya nchi?
Je kujenga vyoo, kutumia samadi na mbolea, kulima kwa usatadi na kisasa, kuzoa takataka, kusafisha mazingira, kulisha mifugo, kujikinga na maradhi, kuishi kwa maadili, kujituma, kutumia juhudi, kuwa na maarifa, kuongeza tija na kuhamasisha ama kwa motisha au kauli ni lazima tuwe na "Connections na Network" kufanikisha hilo?
Zi wapi zile kauli na msukumo wa Viongozi kujumuika na Wananchi kuzalisha mali na kuwa mfano wa kuigwa na kujenga jamii inayojitegemea? Je Viongozi wa namna hiyo tumewapoteza kabisa na Mzee Simba wa Vita alikuwa ndiyte pekee aliyebakia?
NI aibu na inasikitisha jinsi ambavyo kila Mbunge anavyokimbilia kujenga "Connections na Network" za marafiki wa nadni na nje eti kuleta maendeleo jimboni!
Je ina maana hamuiamini Ilani yenu wenyewe na mipango ya kimaendeleo na Bajeti mnayowaundia Watanzania kila mwaka?
Hizi "Connections na Network" zenu ndizo zilizotuletea EPA, Meremeta, Richmond, IPTL na matakataka mengi tuu hata hili la leo la Kilimo Kwanza na Matrekta kutoka India!
Mnauza uhuru na fikra za Mtanzania kwa kudhania kuwa mkitembeza bakuli nje na ndani ya nchi, basi ile misaada na sadaka za wenye fedha ndio zitakazoleta tija na maendeleo kwa nchi yetu.
Mbaya zaidi ni kuwa mfumo huu wa "Connections na Network" umekomaa hata kuzidi kwenye nyanja ya siasa. Angalia kila NGO, Makanisa, Misikiti na Taasisi nyingine, kila mmoja inategemea "Connections, Network na Ufadhili" wa Nchi, Taasisi, NGO, Dayosisi au Madrass fulani iliyoko nje ya Nchi ili eti tupate maendeleo!
Je ni lini tutaanza kujivunia maendeleo na matunda ya uhuru wetu kwa kutumia Jasho letu wenyewe bila kumtegemea mtu au kutoa rehani Uhuru wetu kisa tumepewa vitanda vya Zahanati, Vitabu, Mashuka, Baisikeli, Pembejeo, Visima na mengineyo mengi ambayo tunavishangilia kwa jina la msaada wa Wafadhili?
Ni wazi kuwa CCM ni chama kilichojaa watu wanaotoa kauli lakini si Wachapa kazi!
Ni dhahiri kuwa ndani ya CCM kuna ukosefu mkubwa wa Watu wenye uwezo wa kuwa Wabunifu wa maendeleo na kuyafanyia kazi kwa nguvu na jasho lao wenyewe na mtji wao bila kungoja msaada au kukimbilia kutegemea ufadhili!
Ni ukweli usiopingika kuwa kushindwa kwetu kama Taifa kuendelea mbele katika vita dhidi ya Ujinga, Umasikini na Maradhi, kunatokana na Udhaifu wa hali ya juu wa Chama Tawala CCM, kwa kuwa kimekosa dira, mwamko na msisimko wenye nishati ya uchapakazi!
Je ni miaka mingapi mingine tuvumilie na tuwape CCM nafasi ya wao kuendelea kupoteza muda wetu na kuvujisha hazina yetu ili kujifunza kazi, kufanya majaribio na kuendelea kutafuta "Connections na Network" za kuleta maendeleo kwa Taifa letu?
Mwaka huu wa 2010, ni mwaka ambao ama tutasuka au tutanyoa, tutakua na kukomaa au kudumaa MILELE!
Sasa nikiwa naendelea kutafakari hilo, Wabunge wawili wameibuka na kutoa kauli kudai kuwa wao wanafaa kuendelea kuwa viongozi kutokana na jinsi walivyojenga mitandao ya ndani na nje ya marafiki ambao huwasaidia hawa Wabunge katika shughuli za MISAADA kwa majimbo yao kama sehemu ya kujipatia ujiko wa kuwa ni Urafiki wao na Kujuana na Watu ndiko kunakochangia maendeleo ya Majimbo yao.
Waheshimiwa Marmo na Kaboyonga wakijibu hoja ya Wabunge kuwekewa muda maalumu wa kuwa Wabunge walikaririwa wakisema hivi
The Minister of State in the Prime Minister's Office, Co-ordination , Policy and Parliamentary Affairs, Mr Phillip Marmo, who spoke as Mbulu MP (CCM), also said: "Let the people decide.''
He took the opportunity to confirm that he would re-contest his seat for the sixth term this year and that secret opinion polls from both opposition and CCM "show that he would win by 80 per cent against any contestant."
He added that as a long-serving MP, he has brought immense development to his constituency, through connections within and outside the country, that would take a long time for a newcomer to accomplish.
"I have connections within and outside the country; friends who have been helping me to accomplish development projects in my constituency, something that will take time for a newcomer," noted Mr Marmo, a lawyer by profession.
The same sentiments were echoed by Tabora Urban MP (CCM), Mr Siraju Kaboyonga, who said experience and knowledge were the best tools for development.
"The first five years is usually when one is trying to understand the laws and regulations, understand how the Parliament operates while the following years, are for getting friends and trying to bring development to a constituency," he noted.
Mr Kaboyonga said limiting MPs' term would leave many constituencies underdeveloped, as Members of Parliament will not have enough time to prepare and bring development to their constituencies.
Citing Tabora Urban as an example, Mr Kaboyonga said it was underdeveloped, because there had been frequent changes of MPs serving the constituency.
"Some constituencies in Tabora are well developed because their MPs have served for long time," he noted.
Najiuliza, kwa vijisababu walivyotoa hawa Wabunge ambavyo narudia tena naamini ndio taswira halisi ya asilimia 95% ya Viongozi wa CCM (Wabunge, Mawaziri, Wajumbe wa NEC, CC, Viongozi wa Mikoa nk.), je tunafaida gani kama Taifa kuendelea kuamini kuwa CCM ni chama Mbadala ambacho kinaweza ifikisha Tanzania katika maendeleo ya kweli na kuvuka daraja la kuwa nchi tegemezi kwa misaada na kuushinda umasikini?
Labda niulize, jimbo la Marmo na la Kaboyonga, yamekuwa chini ya himaya ya CCM tangu tupate Uhuru. Je kila baada ya miaka mitano ambao CCM imekuwa ikinadi Wabunge na Rais katika majimbo hayo, imekuwaje kila mbunge aje na ajenda yake na mipango ya maendeleo ambayo ni huru na si kufuata mchakato wa Ilani ya Chama chao?
Ikiwa Kaboyonga anadai kuwa Tabora mjini imeshindwa kupata maendeleo kutokana na kubadilishwa Wabunge na Marmo anadai kuwa maendeleo wilayani mwake yametokana na "connections" zake binafsi, je kweli watu hawa wanafaa kuwa Viongozi na CCM inafaa kuendelea kuaminiwa?
Hivi katika majimbo ya hawa ndugu wawili, ni lini wamekwenda kuhamasisha Uzalishaji mali na shughuli za maendeleo bila kuwa ombaomba au kudai wanahitaji muda?
Je Kaboyonga anapodai kuwa miaka mitano ya kwanza ya Mbunge ni kujifunza taratibu za Bunge na Sheria, ina maana kama jimbo na Taifa tunapoteza muda na fedha zetu kama walipa kodi na kuchapa miguu (makitaimu) tukisubiri mtu, watu au kikundi ambacho kilijinadi kuwa kina uwezo wa kuongoza na kuleta maendeleo kumbe wanahitaji kupigwa twisheni?
Sasa kwa kauli ya kusema miaka mitano ya kwanza ni kujifunza kazi, kunaonyesha wazi kuwa Watu wengine hukimbiliakuwa Wabunge hata kugombea Urais bila kujua awali ni majukumu gai wanayopaswa kufanya na zaidi ni kuwa wanaupungufu mkubwa wa kiakili na sifa za uongozi kwa madai yao kuwa miaka ya mwanzo ni kujifunza kazi.
Je kuhamasisha Wananchi wachimbe mifreji, wajenge barabara, wasafishe Mazingira, wapeleke watoto shule, waongeze ufanisi na kufanya kazi kwa bidii iwe ni mashambani, viwandani au maofisini kunahitaji mafunzo ya namna gani na ya muda gani ili Wanajimbo wasikae mguu pande wakimsubiri Mbunge wao afuzu darasa la Uongozi?
Nikirudi kwenye kauli zao Marmo na Kaboyonga kuwa wao wameleta maendeleo majimboni mwao kutokana na "Connection" za ndani na nje, je ni nini tafsiri ya Maendeleo na ni maendeleo ya namna gani waliyoyaleta kwa kutumia "Connections"?
Je wanaweza kutuambia masharti ya "Connections" zao ambazo hayatafikia kuhujumu nchi au kuingiza dhululma? Je wanaweza kutuambiakuwa "Connections" hizi ni huru hazina mkono wa Takrima na ufisadi na je wao Marmo na Kaboyonga watalipa vipi Ufadhili na Fadhila za hawa "Connections" wa ndani na nje ya nchi?
Je kujenga vyoo, kutumia samadi na mbolea, kulima kwa usatadi na kisasa, kuzoa takataka, kusafisha mazingira, kulisha mifugo, kujikinga na maradhi, kuishi kwa maadili, kujituma, kutumia juhudi, kuwa na maarifa, kuongeza tija na kuhamasisha ama kwa motisha au kauli ni lazima tuwe na "Connections na Network" kufanikisha hilo?
Zi wapi zile kauli na msukumo wa Viongozi kujumuika na Wananchi kuzalisha mali na kuwa mfano wa kuigwa na kujenga jamii inayojitegemea? Je Viongozi wa namna hiyo tumewapoteza kabisa na Mzee Simba wa Vita alikuwa ndiyte pekee aliyebakia?
NI aibu na inasikitisha jinsi ambavyo kila Mbunge anavyokimbilia kujenga "Connections na Network" za marafiki wa nadni na nje eti kuleta maendeleo jimboni!
Je ina maana hamuiamini Ilani yenu wenyewe na mipango ya kimaendeleo na Bajeti mnayowaundia Watanzania kila mwaka?
Hizi "Connections na Network" zenu ndizo zilizotuletea EPA, Meremeta, Richmond, IPTL na matakataka mengi tuu hata hili la leo la Kilimo Kwanza na Matrekta kutoka India!
Mnauza uhuru na fikra za Mtanzania kwa kudhania kuwa mkitembeza bakuli nje na ndani ya nchi, basi ile misaada na sadaka za wenye fedha ndio zitakazoleta tija na maendeleo kwa nchi yetu.
Mbaya zaidi ni kuwa mfumo huu wa "Connections na Network" umekomaa hata kuzidi kwenye nyanja ya siasa. Angalia kila NGO, Makanisa, Misikiti na Taasisi nyingine, kila mmoja inategemea "Connections, Network na Ufadhili" wa Nchi, Taasisi, NGO, Dayosisi au Madrass fulani iliyoko nje ya Nchi ili eti tupate maendeleo!
Je ni lini tutaanza kujivunia maendeleo na matunda ya uhuru wetu kwa kutumia Jasho letu wenyewe bila kumtegemea mtu au kutoa rehani Uhuru wetu kisa tumepewa vitanda vya Zahanati, Vitabu, Mashuka, Baisikeli, Pembejeo, Visima na mengineyo mengi ambayo tunavishangilia kwa jina la msaada wa Wafadhili?
Ni wazi kuwa CCM ni chama kilichojaa watu wanaotoa kauli lakini si Wachapa kazi!
Ni dhahiri kuwa ndani ya CCM kuna ukosefu mkubwa wa Watu wenye uwezo wa kuwa Wabunifu wa maendeleo na kuyafanyia kazi kwa nguvu na jasho lao wenyewe na mtji wao bila kungoja msaada au kukimbilia kutegemea ufadhili!
Ni ukweli usiopingika kuwa kushindwa kwetu kama Taifa kuendelea mbele katika vita dhidi ya Ujinga, Umasikini na Maradhi, kunatokana na Udhaifu wa hali ya juu wa Chama Tawala CCM, kwa kuwa kimekosa dira, mwamko na msisimko wenye nishati ya uchapakazi!
Je ni miaka mingapi mingine tuvumilie na tuwape CCM nafasi ya wao kuendelea kupoteza muda wetu na kuvujisha hazina yetu ili kujifunza kazi, kufanya majaribio na kuendelea kutafuta "Connections na Network" za kuleta maendeleo kwa Taifa letu?
Mwaka huu wa 2010, ni mwaka ambao ama tutasuka au tutanyoa, tutakua na kukomaa au kudumaa MILELE!