Msafiri Kasian
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 2,133
- 659
Aliyekuwa mwewnyekiti wa Chadema bw Nuru Maeda akirudisha kadi ya chadema na kuchukua ya CCM MBele ya katibu wa CCM wilaya ya Meru bw Langaeli Akyoo Picha, Habari na Gladness Mushi wa Fullshangwe- Arusha Wakati chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikiwa kinaendelea na Oparesheni ya Vua Gamba vaa Gwanda ikiwa inaendelea chama cha mapinduzi (CCM)kimefanikiwa kuvuna wanachama wapya 150 kutoka Chadema ndani ya Eneo la Magadirisho Wilyani Meru Mkoani hapa akiwemo Mwenyekiti wa Tawi la Magadirisho, Bw Nuru Maeda.
Hayo yamebainishwa na Katibu wa CCM wilaya ya Meru bw Langaeli Akyoo wakati wa kuwapokea wanachama wapya akiwemo mwenyekiti huyo sanjari na kufungua ofisi mpya ya tawi hilo mapema jana. Aidha bw Akyoo alisema kuwa wamefanikiwa kupata wanachama hao wapya 150 kwa kipindi cha wiki mbili ambapo wanachama hao hapo awali walikuwa ndani ya chama cha Chadema na hivyo kurudi katika chama Tawala Alifafanua kuwa mbali na kuweza kuvuna wanachama wapya 150 kutoka Chadema pia wamedhamiria kufanya mabadiliko mbalimbali ambapo mabadiliko hayo yataweza kuchochea kwa kiwango kikubwa Mabadiliko hata ndani ya Mashina,Kata,na hatimaye kwa Wilaya nzima.
"hawa wanachama 150 ni wapya kabisa na wanatoka hapa hapa Magadirisho na tunachofurai ni kuona kuwa watu wanatiumia vema
demokrasia yao wenyewe na pia zoezi hili halitakuwa lakuisha kwa mfululizo tumejipanga kuhakikisha kuwa tunaendelea kuvuna wanachama wengi zaidi nah ii ni dalili kuwa Jimbo bado lipo ndani yetu kwani kwa sasa ni sawa na limekopeshwa tu ila bado ni mali ya CCM"aliongeza Bw Akyoo Pia alisema kuwa ingawaje wamefanikiwa kuvuna wanachama 150 pamoja na mwenyekiti wa Chadema bado wana mipango na mikakati mbalimbali ya kuweza kusaidia jamii ya watu wa eneo la Magadirisho hasa kwa Upande wa kukuza na
kuimarisha zaidi uchumi wa maisha yao Alisema kuwa Chama hicho kwa Wilaya ya Meru kimejidhatiti kuimarisha chama cha kuweka na kukopa (SACCOS) ya Magadirisho ambapo kupitia chama hicho wananchi wataweza kuimarisha shuguli zote za kiuchumi ambapo wengine wanakosa dhamana kama hiyo hali ambayo inachangia sana umaskini.
Awali aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema, Bw Nuru Maeda akikabidhi kadi hiyo ya Chadema na kupokea ya CCM alisema kuwa kilichomfanya akimbie chama hicho ni pamoja na kukosekana kwa uzalendo ambao unatangazwa kila siku hali ambayo inasababisha
madhara kwa wanachama wake Alifafanua kuwa demokmrasia ndiyo iliyomfanya akimbie chama hicho na kutokana na hali hiyo bado ana mpango wa kuendelea kuwachukua wafuasi wake mbalimbali ambao alikuwa nao ndani ya Chadema kwa kuwa hata Katiba ya Nchi nayo ina waruhusu kufanya hivyo.
"Nilikuwa ni Miongoni mwa Viongozi wa Chadema lakini leo narudi Ccm ili niweze kuboresha zaidi chama changu hapa kijijini na pia
nawasihi sana wananchi wenzangu hakikisheni kuwa kamwe hamuwui kwenye utawala wa vita ambao uanchangia kupata matatizo makubwa sana"aliongeza Bw Maeda.
Chanzo: GUMZO LA JIJI BLOG.
Hayo yamebainishwa na Katibu wa CCM wilaya ya Meru bw Langaeli Akyoo wakati wa kuwapokea wanachama wapya akiwemo mwenyekiti huyo sanjari na kufungua ofisi mpya ya tawi hilo mapema jana. Aidha bw Akyoo alisema kuwa wamefanikiwa kupata wanachama hao wapya 150 kwa kipindi cha wiki mbili ambapo wanachama hao hapo awali walikuwa ndani ya chama cha Chadema na hivyo kurudi katika chama Tawala Alifafanua kuwa mbali na kuweza kuvuna wanachama wapya 150 kutoka Chadema pia wamedhamiria kufanya mabadiliko mbalimbali ambapo mabadiliko hayo yataweza kuchochea kwa kiwango kikubwa Mabadiliko hata ndani ya Mashina,Kata,na hatimaye kwa Wilaya nzima.
"hawa wanachama 150 ni wapya kabisa na wanatoka hapa hapa Magadirisho na tunachofurai ni kuona kuwa watu wanatiumia vema
demokrasia yao wenyewe na pia zoezi hili halitakuwa lakuisha kwa mfululizo tumejipanga kuhakikisha kuwa tunaendelea kuvuna wanachama wengi zaidi nah ii ni dalili kuwa Jimbo bado lipo ndani yetu kwani kwa sasa ni sawa na limekopeshwa tu ila bado ni mali ya CCM"aliongeza Bw Akyoo Pia alisema kuwa ingawaje wamefanikiwa kuvuna wanachama 150 pamoja na mwenyekiti wa Chadema bado wana mipango na mikakati mbalimbali ya kuweza kusaidia jamii ya watu wa eneo la Magadirisho hasa kwa Upande wa kukuza na
kuimarisha zaidi uchumi wa maisha yao Alisema kuwa Chama hicho kwa Wilaya ya Meru kimejidhatiti kuimarisha chama cha kuweka na kukopa (SACCOS) ya Magadirisho ambapo kupitia chama hicho wananchi wataweza kuimarisha shuguli zote za kiuchumi ambapo wengine wanakosa dhamana kama hiyo hali ambayo inachangia sana umaskini.
Awali aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema, Bw Nuru Maeda akikabidhi kadi hiyo ya Chadema na kupokea ya CCM alisema kuwa kilichomfanya akimbie chama hicho ni pamoja na kukosekana kwa uzalendo ambao unatangazwa kila siku hali ambayo inasababisha
madhara kwa wanachama wake Alifafanua kuwa demokmrasia ndiyo iliyomfanya akimbie chama hicho na kutokana na hali hiyo bado ana mpango wa kuendelea kuwachukua wafuasi wake mbalimbali ambao alikuwa nao ndani ya Chadema kwa kuwa hata Katiba ya Nchi nayo ina waruhusu kufanya hivyo.
"Nilikuwa ni Miongoni mwa Viongozi wa Chadema lakini leo narudi Ccm ili niweze kuboresha zaidi chama changu hapa kijijini na pia
nawasihi sana wananchi wenzangu hakikisheni kuwa kamwe hamuwui kwenye utawala wa vita ambao uanchangia kupata matatizo makubwa sana"aliongeza Bw Maeda.
Chanzo: GUMZO LA JIJI BLOG.