MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Huwa najiuliza kila siku. Je ni kweli CCM huwa wanaiba kura au ni wapinzani na baadhi ya wananchi kudhani uchaguzi wa huru na haki ni chama tawala kushinda tu? Ukiangalia matokeo ya uraisi mwaka 2005 JK alipata kura karibia 80%. Sasa ingechukuwa wizi wa kiasi gani kufikia asilimia hiyo? Ingekua ni wizi wa kura watu wasingesha stukia hapo? Na hata useme CCM wanaiba kura kwenye ubunge tu bado haiji akilini. Kwa sababu.
1.Wananchi wengi huchagua chama badala ya mtu. Kama mgombea chama chake ni maarufu eneo fulani ana nafasi kubwa ya kushinda.
2.Kama mgombea uraisi anaweza kushinda kwa asilimia 80 basi ina maana chama chake kina umaarufu wa kutosha kuji nyakulia wabunge wa kutosha.
Mimi naona ni wakati upinzani waache kukinyooshea CCM kidole kila wakati na badala yake wajiangalie wao wenyewe ni wapi wanakosea. Hakuna uchaguzi ambao upinzani unashindwa bila wao kutoa sababu na visingizo. Uipende CCM au uichukie lakini ukweli unabaki kuwa CCM ni chama makini kinacho jua nini cha kufanya kushinda. Upinzani una kazi kubwa ya kuifikia CCM. Kama tatizo ni katiba basi katiba ibadilishwe lakini sidhani kama CCM wana fanya kitu chochote ambacho chama kingine kisingefanya. Mfano ni Chadema ilipo sema itawa gawia wanawake nguo za ndani kama waki wachagua.
Mtazamo wangu tu. Upinzani kazeni buti muifikie CCM.
1.Wananchi wengi huchagua chama badala ya mtu. Kama mgombea chama chake ni maarufu eneo fulani ana nafasi kubwa ya kushinda.
2.Kama mgombea uraisi anaweza kushinda kwa asilimia 80 basi ina maana chama chake kina umaarufu wa kutosha kuji nyakulia wabunge wa kutosha.
Mimi naona ni wakati upinzani waache kukinyooshea CCM kidole kila wakati na badala yake wajiangalie wao wenyewe ni wapi wanakosea. Hakuna uchaguzi ambao upinzani unashindwa bila wao kutoa sababu na visingizo. Uipende CCM au uichukie lakini ukweli unabaki kuwa CCM ni chama makini kinacho jua nini cha kufanya kushinda. Upinzani una kazi kubwa ya kuifikia CCM. Kama tatizo ni katiba basi katiba ibadilishwe lakini sidhani kama CCM wana fanya kitu chochote ambacho chama kingine kisingefanya. Mfano ni Chadema ilipo sema itawa gawia wanawake nguo za ndani kama waki wachagua.
Mtazamo wangu tu. Upinzani kazeni buti muifikie CCM.