CCM kujitoa ghamba kuna maudhui gani haswa?

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
kulingana na kauli mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi mbali mbali wa CCM akiwemo mwenyekiti wa chama hicho rais Jakaya Kikwete, azma ya CCM ya kutaka kujivua ghamba lake la sasa, imelenga katika kukirejeshea chama hicho umaarufu wake wa miaka ya nyuma ambao hivi sasa unaelekea kupotea. Pengine ni vema tukajiuliza kujivua ghamba kuna maana gani hasa-kubadirisha safu ya uongozi au kubadirisha sera za chama? Nijuavyo mimi, kama kuna jambo lolote lililosababisha CCM kupoteza umaarufu wake, ni kitendo cha chama hicho kuitelekeza sera yake ya zamani ya kuwa mtetezi wa wanyonge katika jamii na badala yake kuwakumbatia wale wanaoendeleza vitendo vya ugandamizaji wa wanyonge hao. Kama hivyo ndivyo nilidhani maana ya kujitoa ghama siyo kubadirisha tu safu ya uongozi, bali pia kurejerea kwenye sera zake za zamani za kuwa mtetezi wa wonyonge.
 
ccm bado hawajajua walipo jikwaa wanadhani Gamba ni makamba and his friends ndo maana wakamtosa.Tatizo la ccm ni mfumo mzima wa chama si la mtu mmoja, kwani ccm imekuwa ikiamini siku zote kuwa pesa ndio njia pekee ya kuwapumbaza wananchi ndo maana imekuwa ikitumia pesa nyingi wakati wa uchaguzi kuonga wapiga kura au kuvuruga mwenendo mzima wa uchaguzi.
wameshindwa kutatua shida za watanzania kwa kukumbatia mafisadi wakitegemea wawasaidie kwenye kampeni za uchaguzi sasa yamewageuka wanaanza kuvuana magamaba.Tatizo sio magamba hata wakivuana magwanda wameisha chelewa hawaaminiki tena mbele ya wapiga kura.
kilichomponza Makamba ni kuchonga sana na kujifanya mtetezi mzuri wa mafisadi ndo maana jk amehamua kumfanya gamba la zamani hili watu waone ccm imejirudi ssb wanadhani makamba ndo kikwazo.
 
Usi - mind sana, haya ni mabadiliko ya kawaiida. Hatuna cha kujadiri hapa. Kama ni makamba na CCm yake na familia yake wamejadiliwa mno humu ndani. Ni wakati wa kujadiri mambo mangine ya maana.
 
Back
Top Bottom