Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
kulingana na kauli mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi mbali mbali wa CCM akiwemo mwenyekiti wa chama hicho rais Jakaya Kikwete, azma ya CCM ya kutaka kujivua ghamba lake la sasa, imelenga katika kukirejeshea chama hicho umaarufu wake wa miaka ya nyuma ambao hivi sasa unaelekea kupotea. Pengine ni vema tukajiuliza kujivua ghamba kuna maana gani hasa-kubadirisha safu ya uongozi au kubadirisha sera za chama? Nijuavyo mimi, kama kuna jambo lolote lililosababisha CCM kupoteza umaarufu wake, ni kitendo cha chama hicho kuitelekeza sera yake ya zamani ya kuwa mtetezi wa wanyonge katika jamii na badala yake kuwakumbatia wale wanaoendeleza vitendo vya ugandamizaji wa wanyonge hao. Kama hivyo ndivyo nilidhani maana ya kujitoa ghama siyo kubadirisha tu safu ya uongozi, bali pia kurejerea kwenye sera zake za zamani za kuwa mtetezi wa wonyonge.