CCM itawatishia wabunge wake hadi lini?

nice 2

JF-Expert Member
Aug 10, 2011
747
520
Lugola akaangwa kwenye 'caucus' ya CCM kwa kauli dhidi ya Mkulo Bungeni


Habari ifuatayo imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la MTANZANIA:

Aliyekuwa Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo ambaye ni Mbunge wa Kilosa (CCM) amemtolea lugha chafu za matusi ya nguoni mbele za watu, mbunge wa Mwibara Kangi Lugola (CCM).

Tuhuma za Mkulo ziliibuka juzi mjini Dodoma wakati wa kikao cha wabunge wa CCM, kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa, chini ya Uenyekiti wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na mambo mengine, iliibuka hoja ya kujadili kitendo cha Lugola kumwandama Mkulo ndani ya Bunge.

Lugola alitakiwa kutoa utetezi wake kwa kile kilichodaiwa ni kukiangusha Chama Cha Mapinduzi (CCM) mbele ya wananchi.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, wa kwanza kuibuka na ndani ya kikao hicho ambacho kiliitwa cha kujadili tuhuma za ufisadi kwa wabunge, alikuwa Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka aliyelaani hatua ya Lugola kumlipua Mkulo Bungeni.

"Ndugu yangu, kikao hiki kilikuwa na mambo kadhaa lakini kubwa ni kumjibu Lugola, wa kwanza alikuwa Ole Sendeka, ambaye alisimama na kulaani hatua kuhusu mwongozo wa Spika dhidi ya Mkulo...

"Kutokana na hali hiyo, ilimfanya Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba (CCM), kuinuka na kuzidi kupigilia msumari kwa Lugola, tena alikilani hatua ya kuwasilisha hoja hiyo kwa kutaja jina la Zitto Kabwe, ndani ya kikao...

"Hatua ya kumtaja Zitto, Nkumba, aliitafsiri kama ni kumpa ujiko, huku akilaumu kwa nini Mkulo aandamwe wakati si mbunge.

Hoja hiyo, iliwafanya wabunge kuzidi kuchagia kwa wingi, huku Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Kessy Mohammed (CCM), akipinga hatua hiyo na kusema katu hawako tayari kufungwa midomo na Serikali ya chama chao.

"Ndugu yangu, hili jambo lilizidi kuchukua sura mpya kila wakati huku nae Mbunge wa Mpendae, Salim Hassan Turky (CCM), ambaye alisema kuisema Serikali ndani ya Bunge ni sawa na si kudhalilisha mbele ya wananchi...

"Hata hivyo, ilionekana kama wamejipanga kuhusu hili maana hata mbunge wa Lushoto, Mlalo Henry Shekifu (CCM), aliunga mkono kauli iliyotolewa na Lugola, huku akiwataka viongozi wa Serikali pamoja na chama kutoa muongozo dhidi ya wabunge...

"Baba weeee hukuwepo ndani ya kikao, lakini malaika wako walikuwepo, kwani mara baada ya kusimama Lugola, aliweka wazi namna alivyodhalilishwa na Mkulo, mbele za watu kwa kutukanwa matusi ya nguoni, ambayo katu hayawezi kusema wala kuandikika gazeti...

"Kutokana na uteezi wa mbunge uyo wa Mwibara, kila mtu alibaki ameacha kinywa wazi na Waziri Mkuu Pinda kulazimika kutumia kila aina ya busara ili hali isizidi kuwa mbaya katika kikao hicho," kilisema chanzo hicho cha kuaminika kwa MTANZANIA.

Hata hivyo, hali hiyo ilionekana iliwalenga baadhi ya wabunge ambao huonekana wakorofi, ilimlazimu Waziri Mkuu Pinda, kumpa nafasi maalumu ya upendeleo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, George Mkuchika, kusema neno la mwisho katika kikao hicho.

"Ni dhahiri Mkuchika, alikuwa na ajenda iliyoandaliwa kwa ajli ya kuitetea Serikali, eeeee alisema huyo hakuna mfano...

"Mkuchika, alisema ni marufuku kuanzia jana (juzi), mbunge yoyote kwa CCM kuishambulia Serikali ndani ya Bunge na mbunge atakayefanya hivyo lazima atajadiliwa na chama...

"… tena alisema hivi sasa ana nafasi nzuri ya kufanya kazi na endapo atatokea mbunge na kuanza kuisema vibaya Serikali atamshughulikia kwa kuwa hivi sasa yupo wizara mayo ina vyombo vya ulinzi na salama kama TAKUKURU, tena huku akiungwa mkono kila mara na Waziri Mkuu Pinda.

"Alisema kuanzia sasa takuwa nafutilia mijadala yote ya bunge pamoja na kusoma hansard za Bunge, ili kufitilia mchango wa kila mbunge, na atakayeisema CCM, atachukuliwa hatua za kinidhamu...

"Waziri Mkuu, alisema haiwezekani unakuta mtu anachangia lakini hakitaji chama cha Mapinduzi (CCM), hata mara moja..

"Hata hivyo pamoja na yote kubwa ushahidi alioutoa Lugola, namna alivyotukanwa matusi ya nguoni na Mkulo, hakika kijana wangu huwezi kuyasikia wala kuyatamka mbele ya watu," kilisema chanzo hicho kilipokuwa kikizungumza na gazeti la MTANZANIA.
 
Ubeti wa pili wa wimbo wa taifa wa UK unasomeka hivi:

O lord God arise,
Scatter our enemies,

And make them fall!
Confound their knavish tricks,
Confuse their politics,
On you our hopes we fix,
God save the Queen!
 
Wabunge wa ccm kuzuiwa wasiiseme ccm na serikali yao ndo msumari wa mwisho kwenye jeneza la ccm, M4C itatawala bunge kwa kutoa hoja ambazo watanzania wanataka kusikia R.I.P ccm
 
John 15:19 "If you belonged to the world, it would love you as its own. As it is, you do not belong to the world, but I have chosen you out of the world. That is why the world hates you" Mark 13:13 "All men will hate you because of me, but he who stands firm to the end will be saved"

Lugola: Your character does not reflect (by all measures) the character of CCM members, but GOD has chosen you out of CCM to save the majority poor Tanzanians, that's why CCM hates you!!. Stand firm Lugola, surely you will be saved.
 
Sidhani kama watafika mbali siamini kama ndipo walipo fikia. Nape anapoteza muda aliko bora angeacha kuliko kuongeza aibu.
 
Mkuchika ana bebwa sana ni wa kwanza kufanya madudu muda umefika hata ukiwanyamazisha kuongea lakini sauti zitatoka na kupaza kwa umma kwa njia tofauti kama hii na wananchi wataelewa hatimae watachukua hatua.
 
Kwahiyo wao ccm hawataki mtu akiboronga ambiwe ukweli? Hili tatizo la kutoambizana ukweli ndilo jinamizi linaloimaliza ccm kwa sasa na mwishowe litawamaliza kabisa
 
Guys, when you see all these happening just know that the end of CCM is coming.
 
Wabunge wa ccm kuzuiwa wasiiseme ccm na serikali yao ndo msumari wa mwisho kwenye jeneza la ccm, M4C itatawala bunge kwa kutoa hoja ambazo watanzania wanataka kusikia R.I.P ccm
Rejea kauli ya NAPE akiwa mjini Mafinga (IRINGA)- Watumishi pia tumetishiwa, tukiwa kazini tuwe Mabubu, tusijadili mukstakabali wa nchi yetu, tukifanya hivyo ni makada wa vyama. WITO: tusikubali ukandamizaji huu, huu ni sawa na ukoloni.
 
These are old fashioned politicians,pm behave, in the coming constitution mp should be legislature not executive
 
Wabunge wa CCM wajue kwamba wapo bungeni kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi hivyo maslahi ya kwanza yawe kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wao na maslahi ya kulindana kichama yapewe nafasi ya pili. Hongereni sana wabunge Mpina, Lugora, Filikunjombe kwa kuelewa kile kilichowapeleka bungeni.
 
Hawa viongozi wa magamba bungeni ni wajinga sana , wanafikiri wanaweza kuwatisha wabunge kama watoto wa shule za chekechea; hawajui kuwa uchaguzi ujao hawa wabunge wa ccm wengi wao hawatakuwa na chama hicho na ishara zinajionesha, kwahiyo kuwatisha kuwa watawachukulia hatua za kuwafukuza chama ni kujipunguzia wabunge kwani in any coming by-election anywhere in the country ccm is bound to lose!!
 
Rejea kauli ya NAPE akiwa mjini Mafinga (IRINGA)- Watumishi pia tumetishiwa, tukiwa kazini tuwe Mabubu, tusijadili mukstakabali wa nchi yetu, tukifanya hivyo ni makada wa vyama. WITO: tusikubali ukandamizaji huu, huu ni sawa na ukoloni.

The one who appeals to authority uses memory and not reason. Hizi ni ishara tosha kwamba magamba wameacha kutumia "reasoning" bali wanatumia tu "memory". Relying on fallacies can't rescue them long enough.
 
Ubeti wa pili wa wimbo wa taifa wa UK unasomeka hivi:

O lord God arise,
Scatter our enemies,

And make them fall!
Confound their knavish tricks,
Confuse their politics,
On you our hopes we fix,
God save the Queen!

Mkuu hapo kwenye red nashauri iwe adopted na CDM ili iwe sala/dua yao daima kabla hajaanza ratiba ya siku ya shughuli za M4C! Hahahahaaaa! Scatter our enemies (Magamba), And make them fall! Confound their knavish tricks, Confuse their politics! Good prayer for the M4C!
 
HUWEZI KUWA MNAFIKI SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO IPO SIKU UTAUMBUKA. USHAURI KWA WABUNGE WA CCM KUMBUKA HUO UBUNGE UNAOPATA NI KUTOKA KWA WANANCHI KWA HIYO JIPIME MWENYEWE BOSS WAKO NI NANI HASA? TENA UKIJADILIWA NDANI YA KAMATI YA CCM ETI UMEISEMA VIBAYA SERIKALI YA BABA MWANAASHA UJUE UNAPATA SIFA KIBAO KWA WANANCHI WAKO NA ITAKUONGEZEA IMANI KUTOKA KWAO KWA HIYO MJUE KABISA NDANI YA CCM SASA HIVI HAKUNA NAHODHA KILA MTU NI NAHODHA TAFADHALI JICHUKULIE BOYA LAKO MAPEMA ILI USIZAME NA HIYO MELI MAANA DALILI ZA KUZAMA ZINAONEKANA NA WALA HAKUNA VIFAA VYA KUTOSHA VYA UOKOAJI. akili ku mkichwa wabunge wa ccm hakika na waambieni acheni na hivyo vikao vya kawaha mko kwa ajili ya wananchi wenu. sisi ndio majaji mtaona tutakavyopiga kura kwa hasira uwiii jamani mungu nisaidie nifike 2015 nitakavyoona watu wazima wanatembelea kichwa badala ya miguu maana na uhakika ni siku ya mapinduzi makubwa sana hapa nchi na kwa africa. tutaandikwa sana kwnye internationa media kuwa we made it.
 
Staili hii ya CCM ndo haswa inaua chama. Kama serikali inakosea af mtu aisifu ati kwa vile ni chama chake inazidisha hasira za wananchi na mjue ya KANU yanawasuburia
 
Ili wananchi wawakilishwe vizuri inatakiwa pawepo na Mgombea Binafsi huyo atakua anawawakilisha wananchi na si chama,ukiwa mbunge kupitia chama lazima kwenye hoja zako utetee chama pia.
 
Haya ni matokeo ya kuacha Tiba ya tatizo na kukimbilia kulificha tatizo......ishu ni kwamba bajeti ni ya kulipa mishahara na posho na hakuna jitihada za kuwa na njia mbadala za kuongeza mapato na kubana matumizi so badala ya CCM ku deal ni hili wana deal na wanaliongelea hili.............watawaziba midomo wabunge wao wengine wataongea na mbaya wananchi wataongea kwenye masanduku ya kupigia kura kwenye majimbo ya hao wanaozibwa midomo...
 

“Mkuchika, alisema ni marufuku kuanzia jana (juzi), mbunge yoyote kwa CCM kuishambulia Serikali ndani ya Bunge na mbunge atakayefanya hivyo lazima atajadiliwa na chama...

“… tena
alisema hivi sasa ana nafasi nzuri ya kufanya kazi na endapo atatokea mbunge na kuanza kuisema vibaya Serikali atamshughulikia kwa kuwa hivi sasa yupo wizara mayo ina vyombo vya ulinzi na salama kama TAKUKURU, tena huku akiungwa mkono kila mara na Waziri Mkuu Pinda.

.

Kama kweli Mkuchika amesema hayo basi tuna tatizo kubwa sana. Mkuchika atatumiaje vyombo vya ulinzi na usalama kama TAKUKURU kushughulikia wabunge anaoona wanapingana na CCM? Kubambikizia kesi maybe?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom