Kama kweli Mkuchika amesema hayo basi tuna tatizo kubwa sana. Mkuchika atatumiaje vyombo vya ulinzi na usalama kama TAKUKURU kushughulikia wabunge anaoona wanapingana na CCM? Kubambikizia kesi maybe?
"Ni dhahiri Mkuchika, alikuwa na ajenda iliyoandaliwa kwa ajli ya kuitetea Serikali, eeeee alisema huyo hakuna mfano...
"Mkuchika, alisema ni marufuku kuanzia jana (juzi), mbunge yoyote kwa CCM kuishambulia Serikali ndani ya Bunge na mbunge atakayefanya hivyo lazima atajadiliwa na chama...
"… tena alisema hivi sasa ana nafasi nzuri ya kufanya kazi na endapo atatokea mbunge na kuanza kuisema vibaya Serikali atamshughulikia kwa kuwa hivi sasa yupo wizara mayo ina vyombo vya ulinzi na salama kama TAKUKURU, tena huku akiungwa mkono kila mara na Waziri Mkuu Pinda.
"Alisema kuanzia sasa takuwa nafutilia mijadala yote ya bunge pamoja na kusoma hansard za Bunge, ili kufitilia mchango wa kila mbunge, na atakayeisema CCM, atachukuliwa hatua za kinidhamu...
"Waziri Mkuu, alisema haiwezekani unakuta mtu anachangia lakini hakitaji chama cha Mapinduzi (CCM), hata mara moja..
.