CCM inahitaji Ukawa bungeni ili ionekane ya maana

Nena

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
2,297
892
Nimejaribu ku study mwenendo mzima wa Bunge letu na nilichogundua ni hiki:
Wabunge wa CCM hawana jipya, hawana maono na wengi wao hawana elimu ya kutosha. Wabunge wa Chadema wana elimu, wana mwamko lakini hawana maturity ya kutosha. Wabunge wa CUF ni mature, kinachowashinda ni kutenganisha masuala ya Zanzibar na ya Muungano.

Wabunge wa CCM wanapata ujiko pale wanapowachokonoa wenzao ambao wana react negatively Chadema (immaturity) na CUF (bias). Sasa hapa ndio wanapanda chati na kutuambia mnaona! Lakini Ukawa wanapotoka , wanaobaki huwa hawana hoja, sana sana uswahili unatawala. Ki ujumla CCM si lolote si chochote. Hata Magufuli ilibidi a outsource mawaziri wake. Ilitakiwa asichukue zaidi ya watano bungeni.

Ombi langu kwa wabunge umefika wakati kila mmoja aangalie mapungufu yake na ajirekebishe. Tunachotaka ni uwakilishi.

Naomba kuwasilisha!
 
Back
Top Bottom