Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,488
- 908
Sehenleed.. *!!
Watu wapitao jamvini, watu makini walao chakula cha maneno hapa kwenye jamvi hili makini, sehenleed!!
Chama chetu CCM, kinaweza kuingia kwenye orodha ya vyama Katili vilivyowahi kutokea hapa kwenye DUNIA hii ya Mola.
Ukatili Wa Chama hiki unatokana Na propaganda zake za kinazi, kizayuni zenye umauti, ambazo wamebahatika kuzishusha na kuzikandamizia kwenye Mawazo yetu watanzania Na kutulevya, propaganda zilizosheheni *uongo mzito sana Na Kwa asilimia kubwa watanzania wengi sasa tunachukiana, kutengana Na kudharauliana Kwa misingi ya Ukabila Na udini
Propaganda hizi zina ufashisti, zinazolenga kuhakikisha kwamba watawala wanabaki madarakani Kwa gharama iwayo yoyote ile hata Kama ni Kwa kumwaga damu ya watanzania..
Ziko propaganda nyingi Lakini Leo niongelee mbili.
1. UDINI.. CCM wametengeneza propaganda kwamba CHADEMA ni Chama cha UDINI.. Ukristu. Na Mgombea wake wa urais ni padre.. Propaganda hii ikanenepa sana kiasi Radio Iman maskini ya mungu wakawa wanamtaja mgombea huyu kama padre Slaa. CCM iwaombe sana radhi Waislam Tanzania Kwa kuwapotosha sana Na wakakosea si Kwa hiari Yao Bali Kwa matakwa ya uroho uliopitiliza Wa kutamani kuendelea kutawala. Sasa hadanganywi *mtu tena. Chama kina Katiba, sera, na taratibu iweje kiwe na Udini mbona wametufanya sisi kuku that way jamani.. ?Propaganda ni kama kansa kwenye ubongo Wa Mwanadamu, propaganda hii walifanikiwa nayo kwenye Chama cha CUF, Chama chetu kile kikadidimia, kikadidimia Na kuzama sasa kinajitutumua ila njaa Kali sana Sijui Kama kitatoka matopeni. Professor Lipumba akaitwa pumba tu, he watu wote tukamdharau kwamba ni professor wa Pumba, kumbe kichwa cha nguvu kiasi DUNIA ya uchumi inamtamani Na sasa inamtumia.. Nakushauri Lipumba kubali walikufanyia TIMING that time, embu JIUNGE CDM, wang'olewe kwanza hawa wasio Na roho za ibinaadam. Mengine baadae
2. UKABILA. baada ya Dola ya propaganda ya UDINI kupata matatizo mawili, moja la uchaguzi wa Igunga, ambapo mbali Na kudumbukiza propaganda hiyo Kwa nguvu sana, Na kushinikiza viongozi wetu wa Dini kutoa matamko makali sana, Lakini CCM ilishtuka sana ilipoambulia ushindi mwembamba sana kwenye kinyang'anyiro hicho, Na pigo la pili ni Uchaguzi jimbo la Uzini ambapo CDM ilikuwa ya pili badala ya kuwa ya tatu au nne. Upepo huo uliwapa ujumbe kwamba Kete ya UDINI sasa imeishiwa Charge.. Sasa wamekuja Na Gia nyingine mbaya zaidi ya Ukabila, kwamba CDM ni Chama cha wachaga, na wameiongezea nguvu kwamba ni Chama cha Ukanda.. Yaani propaganda za CCM ni za kimautimauti, watugawe watanzania kwenye ukanda, wa kaskazini, kusini, magharibi Na mashariki..manake nini Kama CCM wakipata kura nyingi kusini Na CDM kaskazini Basi wataoshika Dola upande wa pili watavutana wajitenge Na hapo ndipo tutarejea Sudan Na umwagaji Damu wa Kutisha..
CCM akili zake sasa hazina akili tena. Kama inapumulia mpira si ikubali kufa peke yake kwani lazima ife Na damu za watu!!.. *Aah!!*
Watu wapitao jamvini, watu makini walao chakula cha maneno hapa kwenye jamvi hili makini, sehenleed!!
Chama chetu CCM, kinaweza kuingia kwenye orodha ya vyama Katili vilivyowahi kutokea hapa kwenye DUNIA hii ya Mola.
Ukatili Wa Chama hiki unatokana Na propaganda zake za kinazi, kizayuni zenye umauti, ambazo wamebahatika kuzishusha na kuzikandamizia kwenye Mawazo yetu watanzania Na kutulevya, propaganda zilizosheheni *uongo mzito sana Na Kwa asilimia kubwa watanzania wengi sasa tunachukiana, kutengana Na kudharauliana Kwa misingi ya Ukabila Na udini
Propaganda hizi zina ufashisti, zinazolenga kuhakikisha kwamba watawala wanabaki madarakani Kwa gharama iwayo yoyote ile hata Kama ni Kwa kumwaga damu ya watanzania..
Ziko propaganda nyingi Lakini Leo niongelee mbili.
1. UDINI.. CCM wametengeneza propaganda kwamba CHADEMA ni Chama cha UDINI.. Ukristu. Na Mgombea wake wa urais ni padre.. Propaganda hii ikanenepa sana kiasi Radio Iman maskini ya mungu wakawa wanamtaja mgombea huyu kama padre Slaa. CCM iwaombe sana radhi Waislam Tanzania Kwa kuwapotosha sana Na wakakosea si Kwa hiari Yao Bali Kwa matakwa ya uroho uliopitiliza Wa kutamani kuendelea kutawala. Sasa hadanganywi *mtu tena. Chama kina Katiba, sera, na taratibu iweje kiwe na Udini mbona wametufanya sisi kuku that way jamani.. ?Propaganda ni kama kansa kwenye ubongo Wa Mwanadamu, propaganda hii walifanikiwa nayo kwenye Chama cha CUF, Chama chetu kile kikadidimia, kikadidimia Na kuzama sasa kinajitutumua ila njaa Kali sana Sijui Kama kitatoka matopeni. Professor Lipumba akaitwa pumba tu, he watu wote tukamdharau kwamba ni professor wa Pumba, kumbe kichwa cha nguvu kiasi DUNIA ya uchumi inamtamani Na sasa inamtumia.. Nakushauri Lipumba kubali walikufanyia TIMING that time, embu JIUNGE CDM, wang'olewe kwanza hawa wasio Na roho za ibinaadam. Mengine baadae
2. UKABILA. baada ya Dola ya propaganda ya UDINI kupata matatizo mawili, moja la uchaguzi wa Igunga, ambapo mbali Na kudumbukiza propaganda hiyo Kwa nguvu sana, Na kushinikiza viongozi wetu wa Dini kutoa matamko makali sana, Lakini CCM ilishtuka sana ilipoambulia ushindi mwembamba sana kwenye kinyang'anyiro hicho, Na pigo la pili ni Uchaguzi jimbo la Uzini ambapo CDM ilikuwa ya pili badala ya kuwa ya tatu au nne. Upepo huo uliwapa ujumbe kwamba Kete ya UDINI sasa imeishiwa Charge.. Sasa wamekuja Na Gia nyingine mbaya zaidi ya Ukabila, kwamba CDM ni Chama cha wachaga, na wameiongezea nguvu kwamba ni Chama cha Ukanda.. Yaani propaganda za CCM ni za kimautimauti, watugawe watanzania kwenye ukanda, wa kaskazini, kusini, magharibi Na mashariki..manake nini Kama CCM wakipata kura nyingi kusini Na CDM kaskazini Basi wataoshika Dola upande wa pili watavutana wajitenge Na hapo ndipo tutarejea Sudan Na umwagaji Damu wa Kutisha..
CCM akili zake sasa hazina akili tena. Kama inapumulia mpira si ikubali kufa peke yake kwani lazima ife Na damu za watu!!.. *Aah!!*