CCM Arusha kwatifuka: Mary Chatanda akataliwa; yeye asema "sing'oki"

Leo majira ya saa kumi na nusu kumetokea vurugu hapa CCM mkoani Arusha, baada ya vijana kumtoa Mary Shitanda kwenye mkutano wekiimba hatukutaki ondoka zako.

Baada ya kuona watu wanazidi kumzonga alichukuliwa na kuingizwa ndani na askari kanzu waliofika hapo na kufunga milango. Kuna wandishi wa startv na Ch 10 walibahatika kuingia ndani.

Sijajua hasa chanzo ni nn?..nimeona twitter JMakamba anapuuza taarifa hizi, kudundwa si lazima fimbo au mawe, maneno makali ni kichapo tosha. vurugu zimetokea, labda kama atapuuza na tbc1

Siasa ni biashara na ndio maana wenye fedha sasa wanaonekana maadui kwa wale wanaotaka kwenda huko! Tutayasikia mengi hadi 2014 kila mtu atakapojidai kuwa mtii kwa chama ili maoni yasiwaangushe.
 
Mi amenichafuaga NDEVU kbs huu pepo wa kuzimu,na alipowa2si wachunga Kondoo wa Bwana hapo ndipo alinigusa NDEVU tena yani mi ni kwamba ckuwepo ON LINE muda ule maana angenijua leo Mi ni MWANAUME ama Mwanamke kama yeye. Hiyo ni Traller tu. Lijinga kabisa!
 
January Makamba ametumia nguvu nyingi na muda mwingi akiibeza JF kuwa ni wazushi tunaandika habari za uongo na matusi.. Nimesikiliza taarifa ya tbc taifa kukawa na taarifa juu ya vijana walioandamana mpaka CCM Mkoa (Arusha) wakishinikiza Mary Chitanda ang'atuke..

Sasa ningependa kumwambia January Makamba aache kukurupuka kwani bado tunakumbuka mauaji yaliyotokea Arusha yaliyosababishwa uropokaji wake na kiburi chake kwakuwa alikuwa ameshashauliwa na akina Lowassa kuwa wakae CDM na CCM wajadili
 
Vijana wa uvccm leo alhamis wameandamana wakimpinga katibu wao wa mkoa, (yule mama aliyehamishiwa kutoka Tanga), wakidai kuwa hana uchungu na chama chao, wamemtaka ajivue gamba. vinginevyo watamtoa kwa nguvu.
 
HA HA HA na baado huyo lichefa yake ambae amemweka huko wamemfua gamba sasa tuone sasa itakuaje. MAKAMBA BWANA WAKE HAUPO SASA TUONE ATAFANYA NINI. Tena nitafurahi angeKOLIMBA because she is so wicked and also a bad news all over.

yuko makamba b kwani huja msikia kwenye twitter alivyokuwa anajitutumuu kukanusha kuwa mama mdogo wake hajabobolewa na wa arusha..
 
Mi amenichafuaga NDEVU kbs huu pepo wa kuzimu,na alipowa2si wachunga Kondoo wa Bwana hapo ndipo alinigusa NDEVU tena yani mi ni kwamba ckuwepo ON LINE muda ule maana angenijua leo Mi ni MWANAUME ama Mwanamke kama yeye. Hiyo ni Traller tu. Lijinga kabisa!

alijisahau akajiona yeye ni kila kitu..
 
Ni wakati wa John Tendwa kutumia katiba ya vyama vya siasa na maadili. kuangalia uwezekano wa Chadema kufutwa.
Ni chama kinacjhochea Vurugu kwani ndio maana matikeo mingi ya uvunjaji wa amani unaendelea.

Umetoka wapi wewe? Tunazungumzia vurugu za CCM Arusha na Mary Chitanda unaleta ya Tendwa ebu usitupotezee mjadala. Hata mwambie Tendwa hayo maneno kama hatakuona chizi maana humtakii mema.
 
Huyu bi mkubwa analo limemganda. Na shosti wake Makamba baba kwishney. Tutaona mengi to 2015. Wangemvunja mguu.
 
alichokosea Maria Chatanda ni kutukana/kukashfu viongozi wa dini, ndicho kilichomfanya avune maadui wengi sana kimyakimya. Arusha watu wanaheshimu sana dini na viongozi wao. kutukana viongozi wa dini for the sake of politics/ccm alifanya kosa kubwa mbele ya watanzania wote na Mungu.
 
CCM Arusha kwachafuka

CHATANDA ATAKIWA KUNG'OKA, GARI LAKE NUSURA LICHOMWE MOTO NA UVCCM

Moses Mashalla, Arusha

HALI si shwari chama tawala mkoani Arusha mara baada ya gari la Katibu wa CCM hapa, Mary Chatanda kunusurika kuchomwa moto na baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM).Wanachama wa umoja huo kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Arusha waliandamana katika Jengo la Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Arusha, wakishinikiza Chatanda pamoja na Mjumbe wa Baraza la Vijana mkoani Arusha, Mrisho Gambo "wajivue gamba".

Hali hiyo ilijitokeza jana katika jengo la makao makuu ya chama hicho wakati Kikao cha Kamati ya Siasa Mkoa kikiendelea ambapo, hali iliyosababisha dereva wa gari la katibu huyo wa CCM kulitoa nje ya jengo hilo na kisha kulikimbiza mahali kusikojulikana.

Vijana hao walikuwa wameshika mabango yenye ujumbe mbalimbali huku wakipaza sauti zilizokuwa zikimtaka Chatanda kuondoka katika nafasi yake ya uongozi kwa madai kwamba amekuwa akikivuruga CCM mkoani Arusha.

Wakizungumza na waandishi wa habari, wanachama hao kutoka wilaya za Monduli, Longido, Arusha, Arumeru, Karatu na Ngorongoro walisema pamoja na wao kutoa malalamiko mbalimbali juu ya Chatanda na Gambo, lakini uongozi wa CCM taifa umekuwa ukiwakumbatia viongozi hao na kudai sasa wamechoka.

Walisema malaliko yao kuwa Chatanda amekuwa akikivuruga chama chao ikiwa ni pamoja na kusababisha kukosa ushindi wa Jimbo la Arusha Mjini lililoenda kwa Chadema huku wakisema kwamba ikiwa atakataa kung'oka watajua cha kufanya.

“Hatumtaki Chatanda na hatumtaki Mrisho Gambo hawa watu kwanza ni wasaliti, lakini pia wamechangia sisi kushindwa kuchukua jimbo hili kwani walikuwa wanaiunga mkono Chadema tunataka waondoke mara moja hadi kieleweke,” ilisikika sauti ya mmoja wa vijana hao.

Miongoni mwa jumbe ambazo zilikuwa zimeandikwa kwenye mambango hayo ni "Chatanda umehujumu uchaguzi kwa siasa zako za makundi zilizojaa chuki, ubinafsi na ubabe usio na manufaa kwa Chama Cha Mapinduzi", "Chatanda kwa siasa zako za ubabe umetuchonganisha na viongozi wa dini”, na nyingine kadha wa kadha.

Hali hiyo ilisababisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha, James Ole Millya aliyekuwa kwenye kikao cha kamati ya siasa kutoka nje na kwenda ukumbini kuwatuliza wanachama hao, lakini juhudi zake ziligonga mwamba. Akizungumza na wanachama hao, Milya aliwataka wapunguze jazba na kusema kuwa yeye ni mjumbe ametumwa kusikiliza madai yao hivyo wampatie na kisha taufikisha ujumbe huo. “Jamani ninawaomba mtulie sidhani kama mtafanya fujo ninaomba mnipatie ujumbe mnitume niufikishe jamani nami nitaufikisha tulieni jamani,” alisema Milya

Hata hivyo, ushawishi wa Milya haukuzaa matunda na kuamua kurudi kikaoni kwani wanachama hao waliendelea kupaza sauti zao kwa wakidai kuwa wanamtaka katibu huyo aondolewe mkoani Arusha kwa kuwa amekuwa akiingilia uamuzi wa umoja wao na kuendelea kumkubatia Gambo. “Mheshimiwa tunakipenda sana chama chetu na tunakuheshimu sana, tunaomba Chatanda aondoke la sivyo tutachoma gari lake, tukikutana nalo tutamondoa kwa nguvu,” alisema kwa jazba mmoja wa vijana hao.

Vijana wavamia kikao cha kamati ya siasa

Wakati hayo yakiendelea wanachama hao walikosa uvumilivu na kisha kuvamia ofisi ambapo Kikao cha Kamati ya Siasa mkoa kilipokuwa kikifanyika huku wakitishia kubomoa mlango kitendo kilichosababisha viongozi mbalimbali wa CCM mkoani hapa kuhaha kutuliza tafrani hiyo. Maafisa usalama wakiwemo askari kanzu walikuwa wametanda katika maeneo ya jengo hilo huku wengine wakionekana wakizungumza na viongozi wa UVCCM kujua chanzo cha vurugu hizo.

Chatanda ajifungia ukumbini

Hadi tunakwenda mitamboni, Chatanda alikuwa bado amejifungia ndani ya ukumbi wa mkutano na hakuna taarifa yoyote ya CCM Mkoa aliyotolewa kuhusiana na tukio hilo.Tuhuma dhidi ya Chatanda kutoka ndani ya chama chake zimekuja siku chache tangu ashutumiwe kuwa mmoja wa waliosababisha mgogoro mkubwa wa kisiasa mkoani Arusha baina ya vyama vya CCM na Chadema.

Mgogoro huo unafuatia Chadema kupinga katibu huyo wa CCM wa Mkoa wa Arusha kushiriki katika vikao vya Baraza la Madiwani na kupiga kura ya kumchagua meya wa Jiji la Arusha, hali Iliyosababisha maandamano makubwa ambayo yalisababisha vifo vya watu watatu. Wakati CCM wakidai kuwa Chatanda ni mjumbe halali wa vikao vya baraza hilo, Chadema wamekuwa wakipinga kwa maeleo kwamba mwanamama huyo ni mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tanga hivyo hana sifa ya kushiriki vikao vya Arusha.

CCM Arusha kwachafuka
 
Haya sasa 2liwambien huyo ndo alikuwa chanzo cha mauaji Arusha mkaona cdm wanazusha. Haya kanyaga twende. Magamba yatasema vjana hao ni wa cdm ngoja kukuche 2one
 
HALI si shwari chama tawala mkoani Arusha mara baada ya gari la Katibu wa CCM hapa, Mary Chatanda kunusurika kuchomwa moto na baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM).Wanachama wa umoja huo kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Arusha waliandamana katika Jengo la Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Arusha, wakishinikiza Chatanda pamoja na Mjumbe wa Baraza la Vijana mkoani Arusha, Mrisho Gambo "wajivue gamba".

Hali hiyo ilijitokeza jana katika jengo la makao makuu ya chama hicho wakati Kikao cha Kamati ya Siasa Mkoa kikiendelea ambapo, hali iliyosababisha dereva wa gari la katibu huyo wa CCM kulitoa nje ya jengo hilo na kisha kulikimbiza mahali kusikojulikana.

Vijana hao walikuwa wameshika mabango yenye ujumbe mbalimbali huku wakipaza sauti zilizokuwa zikimtaka Chatanda kuondoka katika nafasi yake ya uongozi kwa madai kwamba amekuwa akikivuruga CCM mkoani Arusha.

Wakizungumza na waandishi wa habari, wanachama hao kutoka wilaya za Monduli, Longido, Arusha, Arumeru, Karatu na Ngorongoro walisema pamoja na wao kutoa malalamiko mbalimbali juu ya Chatanda na Gambo, lakini uongozi wa CCM taifa umekuwa ukiwakumbatia viongozi hao na kudai sasa wamechoka.

Walisema malaliko yao kuwa Chatanda amekuwa akikivuruga chama chao ikiwa ni pamoja na kusababisha kukosa ushindi wa Jimbo la Arusha Mjini lililoenda kwa Chadema huku wakisema kwamba ikiwa atakataa kung'oka watajua cha kufanya.

"Hatumtaki Chatanda na hatumtaki Mrisho Gambo hawa watu kwanza ni wasaliti, lakini pia wamechangia sisi kushindwa kuchukua jimbo hili kwani walikuwa wanaiunga mkono Chadema tunataka waondoke mara moja hadi kieleweke," ilisikika sauti ya mmoja wa vijana hao.

Miongoni mwa jumbe ambazo zilikuwa zimeandikwa kwenye mambango hayo ni "Chatanda umehujumu uchaguzi kwa siasa zako za makundi zilizojaa chuki, ubinafsi na ubabe usio na manufaa kwa Chama Cha Mapinduzi", "Chatanda kwa siasa zako za ubabe umetuchonganisha na viongozi wa dini", na nyingine kadha wa kadha.

Hali hiyo ilisababisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha, James Ole Millya aliyekuwa kwenye kikao cha kamati ya siasa kutoka nje na kwenda ukumbini kuwatuliza wanachama hao, lakini juhudi zake ziligonga mwamba.

Akizungumza na wanachama hao, Milya aliwataka wapunguze jazba na kusema kuwa yeye ni mjumbe ametumwa kusikiliza madai yao hivyo wampatie na kisha taufikisha ujumbe huo.

"Jamani ninawaomba mtulie sidhani kama mtafanya fujo ninaomba mnipatie ujumbe mnitume niufikishe jamani nami nitaufikisha tulieni jamani," alisema Milya

Hata hivyo, ushawishi wa Milya haukuzaa matunda na kuamua kurudi kikaoni kwani wanachama hao waliendelea kupaza sauti zao kwa wakidai kuwa wanamtaka katibu huyo aondolewe mkoani Arusha kwa kuwa amekuwa akiingilia uamuzi wa umoja wao na kuendelea kumkubatia Gambo.

"Mheshimiwa tunakipenda sana chama chetu na tunakuheshimu sana, tunaomba Chatanda aondoke la sivyo tutachoma gari lake, tukikutana nalo tutamondoa kwa nguvu," alisema kwa jazba mmoja wa vijana hao.

Vijana wavamia kikao cha kamati ya siasa
Wakati hayo yakiendelea wanachama hao walikosa uvumilivu na kisha kuvamia ofisi ambapo Kikao cha Kamati ya Siasa mkoa kilipokuwa kikifanyika huku wakitishia kubomoa mlango kitendo kilichosababisha viongozi mbalimbali wa CCM mkoani hapa kuhaha kutuliza tafrani hiyo.

Maafisa usalama wakiwemo askari kanzu walikuwa wametanda katika maeneo ya jengo hilo huku wengine wakionekana wakizungumza na viongozi wa UVCCM kujua chanzo cha vurugu hizo.

Chatanda ajifungia ukumbini
Hadi tunakwenda mitamboni, Chatanda alikuwa bado amejifungia ndani ya ukumbi wa mkutano na hakuna taarifa yoyote ya CCM Mkoa aliyotolewa kuhusiana na tukio hilo.

Tuhuma dhidi ya Chatanda kutoka ndani ya chama chake zimekuja siku chache tangu ashutumiwe kuwa mmoja wa waliosababisha mgogoro mkubwa wa kisiasa mkoani Arusha baina ya vyama vya CCM na Chadema.

Mgogoro huo unafuatia Chadema kupinga katibu huyo wa CCM wa Mkoa wa Arusha kushiriki katika vikao vya Baraza la Madiwani na kupiga kura ya kumchagua meya wa Jiji la Arusha, hali Iliyosababisha maandamano makubwa ambayo yalisababisha vifo vya watu watatu.

Wakati CCM wakidai kuwa Chatanda ni mjumbe halali wa vikao vya baraza hilo, Chadema wamekuwa wakipinga kwa maeleo kwamba mwanamama huyo ni mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tanga hivyo hana sifa ya kushiriki vikao vya Arusha.

source: Gazeti la mwananchi
Chatanda hajui Kimya cha viongozi wa dini Arusha baada ya kuwakashfu kina mshindo gani, dalili zimeanza kuonekana.
 
Usimtukane nabii wa Mungu, anayokuambia ni sauti ya Mungu, kupingana au kumtukana unamdhalilisha Mungu, nenda katubu na ondoka amani irudi Arusha. WanaCCM wenyewe wanajua matatizo ya Arusha ni Chatanda, na Wanaarusha wanataka amani ipatikane, viongozi washirikiane katika kuijenga Arusha. Uchaguzi halali ambao umefuata taratibu na sheria sijaona Chadema walipogomea, nini kinaendelea Arusha?
 
alikuwa na moyo mgumu wa kutotaka maridhiano akiamini wanaCCM wote wanamuunga mkono.Inanishangaza sana,kulikuwa na tatizo gani kukaa meza moja na CDM na kumaliza tofauti zilizopo?mimi ninaamini hakuna tatizo,ugumu wa mioyo na roho zilijaa uchu wa madaraka wa viongozi wetu ndio iliyopelekea kuvuruga amani na wao wenyewe kuishi kwa wasiwasi .ni bora viongozi wetu wakajifunza kuwa watenda haki kwani haki hiyo lazima itapatikana hata kama itachelewa.
 
Back
Top Bottom