Bureau De Change na kushuka kwa thamani ya shilingi

Kwahiyo unataka kusema serikali ikitaka pesa inaenda kujichotea tu BOT? Mimi naamini uhusiano kati ya BOT naserikali hauna tofauti na uhusiano wa CRDB na wewe kama account holder wa CRDB na wewe mfano ni mmoja wa directors wa CRDB. Kama wewe ni mmoja wa directors wa CRDB, unaweza tu kwenda kujikopea unavyotaka? Je, unaweza kwenda kujichote tu pesa pale?

Nadhani hata commercial banks zina accounts BOT, kama vile ambavyo serikali ina accounts BOT.

Tena shukuru hapa serikali ndio inasimamia BOT. Unajua kwamba Federal Reserve ya marekani ni partly privately owned organization?
Duh ingekuwa kujichotea basi ingekuwa kazi saana. Kila kitu kina usimamizi. Wale ni banker wa serikali ndio maana miaka kama 2 iliyopita serikali ilitangaza kuondoa fedha zake zote (S ikumbuki vizuri zinakadiriwa kuwa trilioni 2) kutoka kwenye benki binafsi. Na madhara yake yakaelezeka kwa kirefu saana. Wale jamaa pale BOT hawana ubavu mbele ya serikali kabisaa. Si kama mie na CRDB. Inasemekana Dr Idrisa wakati akiwa Governor alijifanya kogoma kutoa pesa kwa ajili ya kampeni, wakamuweka kando. Kwahiyo elewa si seperate entity. Ni nadharia tu hususani kwa nchi yetu.
 
Naomba nitofautiane kidogo.

Kinachoanza si dolarization. Dolarization inafuata baada ya thamani ya shilingi kuanza kutokuaminika. Its all about Trust.

Kuelezea kwa kutumia supply and semand ni ku-simplify kinachotokea. Inasaidia kuelewa, lakini sio the whole truth.
Rejea post number 14.
 
Duh ingekuwa kujichotea basi ingekuwa kazi saana. Kila kitu kina usimamizi. Wale ni banker wa serikali ndio maana miaka kama 2 iliyopita serikali ilitangaza kuondoa fedha zake zote (S ikumbuki vizuri zinakadiriwa kuwa trilioni 2) kutoka kwenye benki binafsi. Na madhara yake yakaelezeka kwa kirefu saana. Wale jamaa pale BOT hawana ubavu mbele ya serikali kabisaa. Si kama mie na CRDB. Inasemekana Dr Idrisa wakati akiwa Governor alijifanya kogoma kutoa pesa kwa ajili ya kampeni, wakamuweka kando. Kwahiyo elewa si seperate entity. Ni nadharia tu hususani kwa nchi yetu.

Unachozungumzia hapo ni matokeo ya siasa yetu kuruhusu influence ya wanasiasa pale BOT. Na wala haimaanishi ndivyo inavyotakiwa iwe.

Na alichofanya Dr. Idrisa inabidi umpongeze na sio kumkejeli, kwa sababu hivyo ndivyo alivyotakiwa kufanya kisheria. Kutolewa kwake ni matokeo ya kuruhusu siasa iingie pale, na matokeo yake tumeyaona.
 
Unachozungumzia hapo ni matokeo ya siasa yetu kuruhusu influence ya wanasiasa pale BOT. Na wala haimaanishi ndivyo inavyotakiwa iwe.

Na alichofanya Dr. Idrisa inabidi umpongeze na sio kumkejeli, kwa sababu hivyo ndivyo alivyotakiwa kufanya kisheria. Kutolewa kwake ni matokeo ya kuruhusu siasa iingie pale, na matokeo yake tumeyaona.
Sorry kwa maandishi ya kuonyesha kumkejeli Idrisa. Naomba niwe wazi, Idrissa ni miongoni mwa wasomi ninaowaamini saana, kamwe sitamkejeli.
 
Halafu kuna kitu kingine ambacho nadhani kinachangia kwenye inflation nchi hiii.

Sijui kama wengine msha-notice kwamba hii nchi kila mtu sasa anakuwa dalali, na anataka cha juu. Yaani hata ndugu yako ukimwambia tu unatafuta kitu, unaweza ukadhani anakusaidia kutafuta, kumbe na yeye anatafuta cha juu.

Na unakuta dalali mmoja anamwambia mwengine "ukileta mteja unakula pasenti yako". Na huyo anayeambiwa hivyo naye anamwambia mwingine hivyo hivyo. Sasa kitu cha sh 200 kikipita kwa madalali kadhaa unaweza ukajikuta unalipa zaidi ya mara mbili ya thamani yake.

Na pia madalali hawa wanasaidia sana kupandisha thamani ya kitu. Kumbuka wao wanalipwa kamisheni, kwa hiyo anavyouza kwa bei kubwa ndivyo kamisheni yake inakuwa kubwa, kwa hiyo ana kila insentive ya kuhakikisha bei iko juu.

Nadhani hii imechangia kwa kiasi flani ku-inflate bei za nyumba, viwanja, etc.

Hii hali kwa kweli mimi binafsi inanitisha. Labda wataalamu wa uchumi watatusaidia. Lakini ninaloliona wazi ni kwamba kunakuwa na kundi hili la watu ambao hawazalishi kitu lakini wanaishi, wakigharimiwa na wachache wanaozalisha. Sasa nguvu kazi ambayo ndiyo ingebidi iende kwenye "Kilimo Kwanza" ndiyo ambayo tayari ina shughuli nyingine inayolipa.

lol
 
Duu Kumbe Tanzania bila umaskini inawezekana kabisa kama tutaweza kutengeza ajira na zikawa national guarantee economy basi Tz itakuwa juu kama tukiamua kuwapiga chini wabunge wababaishaji 2010.
 
Halafu kuna kitu kingine ambacho nadhani kinachangia kwenye inflation nchi hiii.

Sijui kama wengine msha-notice kwamba hii nchi kila mtu sasa anakuwa dalali, na anataka cha juu. Yaani hata ndugu yako ukimwambia tu unatafuta kitu, unaweza ukadhani anakusaidia kutafuta, kumbe na yeye anatafuta cha juu.

Na unakuta dalali mmoja anamwambia mwengine "ukileta mteja unakula pasenti yako". Na huyo anayeambiwa hivyo naye anamwambia mwingine hivyo hivyo. Sasa kitu cha sh 200 kikipita kwa madalali kadhaa unaweza ukajikuta unalipa zaidi ya mara mbili ya thamani yake.

Na pia madalali hawa wanasaidia sana kupandisha thamani ya kitu. Kumbuka wao wanalipwa kamisheni, kwa hiyo anavyouza kwa bei kubwa ndivyo kamisheni yake inakuwa kubwa, kwa hiyo ana kila insentive ya kuhakikisha bei iko juu.

Nadhani hii imechangia kwa kiasi flani ku-inflate bei za nyumba, viwanja, etc.

Hii hali kwa kweli mimi binafsi inanitisha. Labda wataalamu wa uchumi watatusaidia. Lakini ninaloliona wazi ni kwamba kunakuwa na kundi hili la watu ambao hawazalishi kitu lakini wanaishi, wakigharimiwa na wachache wanaozalisha. Sasa nguvu kazi ambayo ndiyo ingebidi iende kwenye "Kilimo Kwanza" ndiyo ambayo tayari ina shughuli nyingine inayolipa.

lol
Kwa 100% nakubaliana. Hili ni tatizo kubwa sana.
 
Halafu kuna kitu kingine ambacho nadhani kinachangia kwenye inflation nchi hiii.

Sijui kama wengine msha-notice kwamba hii nchi kila mtu sasa anakuwa dalali, na anataka cha juu. Yaani hata ndugu yako ukimwambia tu unatafuta kitu, unaweza ukadhani anakusaidia kutafuta, kumbe na yeye anatafuta cha juu.

Na unakuta dalali mmoja anamwambia mwengine "ukileta mteja unakula pasenti yako". Na huyo anayeambiwa hivyo naye anamwambia mwingine hivyo hivyo. Sasa kitu cha sh 200 kikipita kwa madalali kadhaa unaweza ukajikuta unalipa zaidi ya mara mbili ya thamani yake.

Na pia madalali hawa wanasaidia sana kupandisha thamani ya kitu. Kumbuka wao wanalipwa kamisheni, kwa hiyo anavyouza kwa bei kubwa ndivyo kamisheni yake inakuwa kubwa, kwa hiyo ana kila insentive ya kuhakikisha bei iko juu.

Nadhani hii imechangia kwa kiasi flani ku-inflate bei za nyumba, viwanja, etc.

Hii hali kwa kweli mimi binafsi inanitisha. Labda wataalamu wa uchumi watatusaidia. Lakini ninaloliona wazi ni kwamba kunakuwa na kundi hili la watu ambao hawazalishi kitu lakini wanaishi, wakigharimiwa na wachache wanaozalisha. Sasa nguvu kazi ambayo ndiyo ingebidi iende kwenye "Kilimo Kwanza" ndiyo ambayo tayari ina shughuli nyingine inayolipa.

lol

Yeah man.True.True.
Kwa thread hii,kweli upele umepata mkunaji:Manitoba.
 
Halafu kuna kitu kingine ambacho nadhani kinachangia kwenye inflation nchi hiii.

Sijui kama wengine msha-notice kwamba hii nchi kila mtu sasa anakuwa dalali, na anataka cha juu. Yaani hata ndugu yako ukimwambia tu unatafuta kitu, unaweza ukadhani anakusaidia kutafuta, kumbe na yeye anatafuta cha juu.

Na unakuta dalali mmoja anamwambia mwengine "ukileta mteja unakula pasenti yako". Na huyo anayeambiwa hivyo naye anamwambia mwingine hivyo hivyo. Sasa kitu cha sh 200 kikipita kwa madalali kadhaa unaweza ukajikuta unalipa zaidi ya mara mbili ya thamani yake.

Na pia madalali hawa wanasaidia sana kupandisha thamani ya kitu. Kumbuka wao wanalipwa kamisheni, kwa hiyo anavyouza kwa bei kubwa ndivyo kamisheni yake inakuwa kubwa, kwa hiyo ana kila insentive ya kuhakikisha bei iko juu.

Nadhani hii imechangia kwa kiasi flani ku-inflate bei za nyumba, viwanja, etc.

Hii hali kwa kweli mimi binafsi inanitisha. Labda wataalamu wa uchumi watatusaidia. Lakini ninaloliona wazi ni kwamba kunakuwa na kundi hili la watu ambao hawazalishi kitu lakini wanaishi, wakigharimiwa na wachache wanaozalisha. Sasa nguvu kazi ambayo ndiyo ingebidi iende kwenye "Kilimo Kwanza" ndiyo ambayo tayari ina shughuli nyingine inayolipa.

lol
Haya ni matokeo ya kuporomoka kwa shilingi pia. Maana mtu anahakika kabisa kwamba price yoyote atakayotaja basi mtu atalipa. Inamaana pesa zipo nyingi kwenye mzunguko. Ila pia sababu nyingine ni market yenyewe si efficiency. Hii hasa inazungumzika vizuri kwenye content ya asymetric information. Information hakuna kuna wengine wanapata quality/superior inf than others kwahiyo wanacapitalise hapo. Hapa pia yapo mengi kuanzia kwenye IT na government system itself. Ukisafiri kwenda nje utakuta inf karibu za kila kitu kwenye website za serikali husika, kwahiyo bei zaidi ya unayotegemea lazima utaishtukia.
Lingine pia ni ugumu wa kupata huduma nao unafanya utumie mtu wa kati bila sababu, in the end unajikuta umeliwa. But all in all, kama watu wanaweza kulipa gharama zaidi ya bei halisi hicho ni kiashiria cha inefficiency markets na weak currencies, licha ya kuwa na hayo mengine yanahusika. Mf real estates kwa Tz ni hovyohovyo
 
Lingine pia ni ugumu wa kupata huduma nao unafanya utumie mtu wa kati bila sababu, in the end unajikuta umeliwa. But all in all, kama watu wanaweza kulipa gharama zaidi ya bei halisi hicho ni kiashiria cha inefficiency markets na weak currencies, licha ya kuwa na hayo mengine yanahusika. Mf real estates kwa Tz ni hovyohovyo

Nakupa tano mkuu,
Na uhaba huu unatokana na uzalishaji kidogo unaosababishawa na mazingira magumu yanayotengenezwa kwa makusudi na serikali....viwanja vinapimwa lakini ukiomba hupewi mpaka kupitia kwa fulani, kinachofuata ni kumtafuta dalali anayemjua fulani, naye anamtafuta fulani anayemjua fulani. Kwa hiyo inakua ni mwanzo wa huo mduara.
 
Halafu kuna kitu kingine ambacho nadhani kinachangia kwenye inflation nchi hiii.

Sijui kama wengine msha-notice kwamba hii nchi kila mtu sasa anakuwa dalali, na anataka cha juu. Yaani hata ndugu yako ukimwambia tu unatafuta kitu, unaweza ukadhani anakusaidia kutafuta, kumbe na yeye anatafuta cha juu.

lol

Mkuu mpaka creativity ya miradi ya uzalishaji imepotea. Kila mtu anafikiria kuwa mchuuzi, .. kuchukua nguo, viatu, toy etc toka china na kuuza. Ukimuuliza mtu anafikiria biashara gani atakuambia bar inalipa - sasa huo uchumi utakuaje kwa kuuza vya wenzetu tu?
 
Back
Top Bottom