Bureau De Change na kushuka kwa thamani ya shilingi

Mchili

JF-Expert Member
Aug 19, 2009
725
46
Thamani ya shilingi ya Tanzania imekua ikishuka mfululizo mwaka hadi mwaka kutoka shilingi 20 kwa dolar miaka ya 1980 hadi tulipo shiling 1,330+ kwa dolar mwaka huu. Wataalam wa uchumi wanasema, thamani ya hela ya nchi inakua imara pale ambapo nchi husika inazalisha bidhaa nyingi za kuuza nje kiasi kwamba mahitaji ya fedha yanakua makubwa kwa watu wa nje. Yaani demand ya hela ikiwa kubwa thamani yake kwa dolar inakua kubwa.

Hivyo hivyo kama uzalishaji ni mdogo na nchi inapata mahitaji yake mengi kutoka nje, demand ya dolar inakua kubwa na dhamani ya dolar inapanda ukilinganisha na hela ya ndani. Kwa Tanzania tunauza nje mazao ya kilimo, madini, utalii n.k kupata fedha za kigeni ambazo tunahitaji kununulia mahitaji mbalimbali kama nguo, magari, malighafi, na wataalam.

Udhibiti wa fedha za kigeni uko chini ya Benki kuu ya Tanzania (BOT) na inatakiwa kuhakikisha hela ya kigeni inayopatikana inatumika kuagizia bidhaa au huduma zinazohitajika hapa nchini. Inatakiwa kuhakikisha kuwa hela ya kigeni haihamishwi kuhifadhiwa nchi nyingine. Wasiwasi wangu ni kwamba kwa jinsi Bureau de change zilivyo tapakaa hapa nchini na ufisadi uliopo BOT je kuna udhibiti wa kutosha kuhakikisha watu hawanunui dolar zilizopo na kuhamishia nje?

Je kushuka kwa dhamani ya shilingi yetu hakusababishwi na hizi bureau de change kuliko tunavyofikiri kwamba tunazalisha kidogo?

Nawasilisha.
 
Mkuu siku hizi thamani ya exports zetu ni ndogo kuliko imports. Tumefikia mahali tunaagiza kutoka nje meza, viti, etc. Hatutaki kutumia mbao za humu nchini. Kilimo cha mazao kama pamba, kahawa, korosho, mkonge etc kilisha dorora miaka mingi iliyopita kwa sababu ya jembe la mkono. Achana na porojo za "Kilimo Kwanza" maana hii ni gear ya kura za 2010. Mikataba ya madini imefanya tusiambulie chochote kwenye dhahabu. Hata hiyo Uranium mambo yatakuwa vivyo hivyo. Bado tunaagiza magari, mitambo na safari za majuu za vibosile wa nchi zinatafuna akiba kidogo ya fedha za kigeni tuliyonayo. Sasa ukitaka kununua dollar kwa hela zako za madafu ni lazima utauziwa kwa rate ya juu mwanangu. Thamani ya Shilingi yetu kwishnei bana.
 
Mkuu siku hizi thamani ya exports zetu ni ndogo kuliko imports. Tumefikia mahali tunaagiza kutoka nje meza, viti, etc. Hatutaki kutumia mbao za humu nchini. Kilimo cha mazao kama pamba, kahawa, korosho, mkonge etc kilisha dorora miaka mingi iliyopita kwa sababu ya jembe la mkono. Achana na porojo za "Kilimo Kwanza" maana hii ni gear ya kura za 2010. Mikataba ya madini imefanya tusiambulie chochote kwenye dhahabu. Hata hiyo Uranium mambo yatakuwa vivyo hivyo. Bado tunaagiza magari, mitambo na safari za majuu za vibosile wa nchi zinatafuna akiba kidogo ya fedha za kigeni tuliyonayo. Sasa ukitaka kununua dollar kwa hela zako za madafu ni lazima utauziwa kwa rate ya juu mwanangu. Thamani ya Shilingi yetu kwishnei bana.

Umegongelea misumari karibia yote... labda nyongeza tu kidogo:

Safari za viongozi wetu sizizo na tija yoyote kwa Taifa zimezidi. Safari hizi kwa mwaka zinatupunguzia kwa hali kubwa hata huto tu-dollar tuchache tunatobahatika kukusanya kwa kuuza ngozi na kuwalangua watalii!!

Kwa aliye na bahati ya kufika huko ng'ambo anaweza kujionea jinsi vile mazao ya kilimo kutoka Kenya yalivyo mengi kwenye ma-supermarket pahala pengi. Na tunajionea jinsi vile hela yao isivyoteteleka sana dhidi ya dollar. Lakini sisi mpaka msafara wa Mh. Rais uende ng'ambo ndo tusikie tetesi za 'potential investors!'
 
Kama mafisadi wana mabilioni ya shilingi na bureau de change hazina udhibiti si ndo wanakomba kata hicho kidogo wanaenda kufungua account kwenye off-shore banks mkuu!
 
Bureau de change haziwezi kufanya hivyo.

Labda tupate uelewa kidogo wa jinsi currency zinavyofanya kazi.

Ili kitu chochote kitumike kwa ajili ya kubadilishana thamani (yaani kama currency), nilazima kitu hicho kiwe na guarantee of value. Yaani ili mimi nikupe ndizi wewe unipe yale makaratasi, ni lazima kuwe na guarantee some where kwamba nikipeleka hayo makaratasi nitapata thamani inayokaribiana na thamani ya ndizi zangu. Without this guarantee no one would use the currency. Ndio maana gold inaweza kutumika kama currency. Haina explicit guarantee ya value, lakini mtu atakuwa tayari kubadilisha bidhaa yake na gold kama anaamini kwamba baadaye atarudisha thamani yake kwa kuibadilisha hiyo gold na kitu kingine chenye thamani sawa na hiyo. Na kuna maeneo kuna wakati hata chumvi imetumiaka kama currency, kwa sababu kwa wakati husika watu walikuwa wanaamini kwamba akibadilisha kitu na chumvi atarudhisha thamani yake baadaye.

Sasa currency za nchi hazina tofauti. Bila kuwa na guarantee of value, hakuna mtu angekubali kuzitumia. Sasa the question is: how is this value guaranteed? Ukielewa hilo itasaidia kuepuka asking the wrong questions.

Mimi ninaweza kuissue currency yangu nikaiita Manitoba Shilling (MNS). Ili wewe ukubali kuitumia kwenye biashara zako ni lazima nikuhakikishie kwamba ukipokea MNS na kuiweka nyumbani unaweza ukarudi kwangu siku yoyote na ntakurudishia thamani yako. Thamani ya 1 MNS ni kiasi gani? Mimi naweza kusema kila 1 MNS ntakupa kilo moja ya mahindi. Kwanini isiwe gram 1 ya gold? Well, ningeweza kuchagua hicho, ila lazima nichague kitu ambacho kila mtu atakuwa anaamini thamani yake haibadiliki over time (au haibadiliki-badiliki sana over time). Sasa watu watakubali kutumia MNS zangu ikiwa tu wanaamini thamani yake ni relatively stable, na kwamba ni convenient kuitumia kwa ajili ya kuhifadhia thamani.

Kwa kuwa nimeguarantee kwamba kwa kila MNS 1 nitatoa kilo moja ya mahindi, itanibidi kwa kila MSN 1 ninayo issue nihakikishe kuna kilo moja ya mahindi store kwangu ili jamaa akirudi nayo niwe na mahindi ya kumpa. Bila kufanya hivyo watu hawataamini kwamba nitaweza kuwarudishia 1kg ya mahindi kwa kila MSN 1 watakayorudisha, therefore thamani yake itaporomoka to 0 na hakuna atakayekuwa tayari kuitumia.

Kwa hiyo kama 1,000MSN zipo kwenye circulation, lazima niwe na 1,000Kg za mahindi store kwangu. Hizo 1,000Kg za mahindi ndiyo "guarantee of value" kwa hizo noti za MSN zilizoko kwenye mzunguko. Ghala langu la mahindi likiungua na watu wakajua, basi thamani ya MSN itashuka, na hakuna takayetaka kuitumia. Walionazo watakuwa wamefulia, kwa sababu siwezi tena ku-guarantee value ya MSN 1. (Ndicho kilichotokea Zimbabwe)

Hivyo ndivyo jinsi currency za nchi zilivyokuwa zinaendeshwa wakati flani, na gold imetumika sana ku-guarantee value ya currency. Kwa mfano nchi flani inaweza ikawa inatumia currency inayoitwa Manitoba. Ikisema Manitoba 1 ni sawa na gram 10 za gold, then watahakikisha kwa kila Manitoba moja wanayoingiza kwenye mzunguko, kuna gram 1 ya gold inayoingia kwenye reserve ya central bank yako. Na central bank itakuwa ina warehouses kwa ajili ya kuhifadhi gold hizo.

Kwa mfano huo, ili kuingiza noti zaidi kwenye mzunguko, inabidi wawe na uwezo wa kupata na khifadhi kiasi cha gold sawa sawa na thamani ya hiyo hizo pesa wanazoingiza kwenye mzunguko. Kwa jinsi hiyo thamani ya Manitoba haiwezi kushuka kwa sababu yoyote isipokuwa thamani ya gold kushuka.

Sasa imagine wewe ndio mkuu wa nchi hiyo ya kizamani. Na uongozi wako unataka kutengeneza pyramid flani lakini pesa iko tight. Unajua unahitaji Manitoba 10,000 kwa ajili ya hilo. Maana yake unahitaji gram 1,000 za gold ili iweze kuwapelekea central bank wakupe pesa hizi ukamilishe project. Lakini kama huna uwezo wa kupata hizo gold, unafanyaje? Unaweza ukaamua kuwalazimisha central bank watengeneze na wakupe hizo pesa. Kitakacotokea ni kwamba zitaingia Manitoba 10,000 kwenye mzunguko ambazo hazina backup, na hivyo in reality thamani ya Manitoba moja itakuwa imepungu na sio 10 gram za gold tena. Watu wasipojua poa, lakini wakija kujua, thamani ya Manitoba moja itapungua accordingly. Sikuhizi wanaita hii inflation.

Hicho ndicho moja ya vitu vilivyoangusha Roman Empire.

Sasa kabla ya miaka ya 1970s, nchi nyingi zilikuwa zime-guarantee currency zao kwa kutumia gold. Na maana yake ni kwamba kulikuwa na gold reserves mainteined kwa kila noti na sarafu iliyokuwa inatolewa.

Baadaye na mpaka sasa hiyo ikawa tofauti. Sasa swali ni je, nini kina-guarantee value ya USD au Tanzanian Shilling (TZS) siku hizi? Wengine wanasema exports na imports, wengine demand na supply, etc na wote wako sawa. Ila kwa maneno ya jumla zaidi ni kwamba uchumi wa nchi ndio una-act kama guarantee ya value ya currency ya nchi husika.

Chochote kingine utakachojaribu kufanya (kudhibiti nani anaweza kununuafedha za kigeni, etc) kunaweza kukaonekana kama kusaidia ku-stabilizie currency ya nchi. Lakini in the long run, haitasaidia kama uchumi wa nchi si mzuri.

Na kingine ni kwamba wakuu wanaweza kushawishika ku-print fedha ili kugharimia miradi ambayo fedha zake inakuwa ngumu kuzipata kutokana na mikopo au mapato. Sasa effect ya ku print fedha huku ni sawa na effec ya ku-issue Manitoba bila kuongeza size ya gold reserve. Zote zitasababisha thamai ya fedha husika kushuka. Mwingine atasema bei za vitu zimepanda, ambayo ni sawa. Lakini ukweli ni kwamba thamani ya fedha husika ndio imeshuka. Mtu akisema mahindi yamepanda bei, mimi ntamwambia shilingi imeshuka bei. Na wote tutakuwa sawa.

Kwa hayo pengine unaweza kuona kwamba, hata tuki-export vitu vichache, bado kuna uwezekano wa kuwa na currency ambayo inathamani. La sivyo ingebidi tuhitimishe kwamba nchi ambayo hai-export chochote basi fedha yake itakuwa haina thamani kabisa, kitu ambacho si kweli pengine.

Uchumi weto ukikomaa, uzalishaji ukaongezeka hata kama ni kwa ajili ya mahitaji ya ndani tu, ajira zikaongezeka, etc, hata kama exports hazitapanda kihivyo kuna uwezekano wa thamani ya shilingi kupanda.

Kwa maoni yangu, sababu kwa nini export na import zina-corelate na thamani ya shilingi ni kwa sababu mara nyingi uchumi ukikomaa hivyo, maana yake bidhaa zenu ni nyingi pengine zina ubora sana na kuna uwezekano zaidi wa watu wa nje kuzihitaji, na hivyo demand yake ya nje itaongezeka. Lakini hii demand ya nje sio lazima kiwe ndio kitu kilichosababisha thamani ya fedha hiyo kukua moja kwa moja. Of couse hiyo itakuwa tofauti kama nchi husika imekuza uchumiwake kwa kutumia exports (exports led growth).

Tukirudi kwa swala la Bureau De Change, wale jama ni wafanyabiashara, na wanafanya biashara ya fedha jinsi mtu mwingine anavyofanya biashara ya mahindi na maharage. Kwake yeye demand na supply ndio vinavyopanga bei. Akiuza ghali sana na asipopata mteja, atashusha bei. Akitaka kunua rahisi sana asipopata anayemuuzia, atapanda dau. Na kumbuka bei zao huwa zinakuwa guided na mi-market rate (bei ya kati ya mauzo na manunuzi ya fedha baina ya mabenk nadhani) ya bei za fedha ambazo wao Beureau De Change hawana influence nazo kabisa.

Mimi sio mchumi, kwa hiyo inawezekana nimefikiria upande kuhusu hili. Jisikie huru kukosoa.
 
Maelezo murua kabisa hayo mkulu Manitoba. Ahsante.

...Ila kwa maneno ya jumla zaidi ni kwamba uchumi wa nchi ndio una-act kama guarantee ya value ya currency ya nchi husika.

Chochote kingine utakachojaribu kufanya (kudhibiti nani anaweza kununuafedha za kigeni, etc) kunaweza kukaonekana kama kusaidia ku-stabilizie currency ya nchi. Lakini in the long run, haitasaidia kama uchumi wa nchi si mzuri.
...
Kwa hayo pengine unaweza kuona kwamba, hata tuki-export vitu vichache, bado kuna uwezekano wa kuwa na currency ambayo inathamani. La sivyo ingebidi tuhitimishe kwamba nchi ambayo hai-export chochote basi fedha yake itakuwa haina thamani kabisa, kitu ambacho si kweli pengine
Nikisoma maelezo yako kitu kinachobakia kama sababu na guarantee ya thamani ya pesa ni SIASA za hii nchi yetu na matendo ya Wanasiasa kwa ujumla. Au, kuna kingine tena...?
 
Maelezo murua kabisa hayo mkulu Manitoba. Ahsante.


Nikisoma maelezo yako kitu kinachobakia kama sababu na guarantee ya thamani ya pesa ni SIASA za hii nchi yetu na matendo ya Wanasiasa kwa ujumla. Au, kuna kingine tena...?

Kabisa mkuu.

Sera ya fedha ndiyo inatumiwa ku-control thamani ya pesa pamoja na ukuaji wa uchumi ([ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Monetary_policy[/ame] ). Na siasa mkono wake unafikaga huko ... so u see the link. Sera ya fedha yaweza kutmika vibaya kwa manufaa ya kisiasa, au ya watu wachache wenye influence na kusababisha mengi tu ikiwa ni pamoja na kushuka kwa thamani ya fedha au hata kuporomoka kwa uchumi.
 
Kabisa mkuu.

Sera ya fedha ndiyo inatumiwa ku-control thamani ya pesa pamoja na ukuaji wa uchumi (http://en.wikipedia.org/wiki/Monetary_policy ). Na siasa mkono wake unafikaga huko ... so u see the link. Sera ya fedha yaweza kutmika vibaya kwa manufaa ya kisiasa, au ya watu wachache wenye influence na kusababisha mengi tu ikiwa ni pamoja na kushuka kwa thamani ya fedha au hata kuporomoka kwa uchumi.

Ahsante Manitoba kwa maelezo yako mazuri. Kwa Tanzania sera ya fedha na utekelezaji wake haufanywi inavyotakiwa. Mathalani moja ya mashtaka ya wakubwa wa BoTwaliofikishwa mahakamani juzi ni kuchapisha hela in eccess. Kwahiyo ile calculated reserve haiwezi kulingana na hela iliyoko kwenye mzunguko kwa sababu kuna mianya mingi ya kuingiza fedha chafu kwenye huo mzunguko.

Suala la bureau de change linakuja kutokana kwamba anayepata hizi hela nyingi nje ya utaratibu atataka kuzihamishia nje ya nchi zikiwa in form of dolar or euro etc. Historia inaonyesha waafrica wanapenda kuficha mahela yao nje.
 
Off topic kidogo, lakini kuna-kitu kimoja interesting ambacho wengi hatukijui: fedha zako inwezekana si zako. Hata serikali yako haina pesa. Pesa zote unazoziona ni mikopo.

Hebu jiulize, serikali ikitaka pesa inafanyaje? Inakopa kutoka kwa benki kuu au kutoka kwa watu binafsi kwa kupitia benki kuu, na riba kubwa tu. Cha kushangaza hapa ni kwamba serikali ambayo pengine ndiyo ingebidi iwe mmiliki wa hizo pesa inabidi ikope na tena ilipie mkopo huu riba.

Serikali inapata wapi pesa sa kulipa deni hilo? Ni kwa kutukata sisi kodi. Ndio maana sehemu ya kodi tunayolipa lazima iende kwenye kulipa deni hilo, na inayobaki ndio tunaigawa-gawa kwenye bajeti.

Kwa hiyo serikali yetu huwaga haina pesa. Sasa kama haina pesa je, supply ya fedha huwa inakuwa controled vipi?

Kumbuka supply ya fedha ikiwa kubwa kuliko ambavyo uchumi unaruhusu tuna inflation kwa sababu thamani yake inshuka. Supply ikiwa ndogo, tunakuwa na deflation ambayo inaweza kuwa mbaya zaidi.

Unaweza ukalia ukijua ukweli.

Ili ku-control inflation inabidi kuondoa fedha kwenye mzunguko. Kufanikisha hili inabidi kupunguza matumizi yake. Na tunajua jinsi hii inavyokuwa tofauti na malengo ya kisiasa.

Ili ku-control deflation inabidi kuongeza pesa kwenye mzunguko. Lakini kwa kuwa serikali haina pesa, inabidi kwenda kukopa tena. Na hiyo inamaanisha riba inaongezeka. Itatoa wapi hii riba? Tunakamuliwa kodi!

Sasa kuna watu wachache ambao wao wanakula kuku kwa mrija. Kazi yako ni kuikopesha serikali na kusubiri riba. Hawa watu hawawezi kulala njaa kwa sababu serikali tayari iko kwenye deni na haina pesa, na inahitaji kukopa.

Sasa jiulize hawa watu wanatoa wapi pesa za kuikopesha serikali ambazo haziishi?

Pengine tujiulize hawa watu ni wakina nani? Kwanza ni Benki Kuu lakini kwa hapa TZ Benki kuu tunaweza kusema ni ya serikali (pengine kwa kuangalia juu juu), kwa hiyo pengine tuko safe kuliko wamarekani kwa mfano. Pili ni mabenki.

Hivi unajua mabenki yanatengeneza fedha? Nnaposema kutengeneza fedha simmanishi kuzalisha kama tunavyomaanisha tukiwa mtaani. Namaanisha ni kama vile kuchapisha pesa, na kuziingiza kwenye mzunguko

Chukulia wewe n benki, na ukapokea deposit ya buku moja, 1,000TZS kutoka kwa mteja M1. Mteja M2 anakuja anataka mkopo wa 900TZS. Unampa 900TZS. Kwa hiyo M1 anasema na 1,000TZS na M2 akiulizwa anasema na 900TZS. Jumla una 1,900TZS. Kwa bahati M2 ana-deposit hiyo 900 yake kwenye account iliyo kwenye benki yako. Anakuja M3 naye anataka 800TZS. Kutoka kwa 900 ya M2 unatoa 800 unampa M3. Mpaka sasa tuna 2,700TZS. Kwa hiyo benki yako kwa kupokea 1,000TZ ya deposit imeweza kutengeneza pesa kiasi cha 1,700TZS na kukiingiza kwenye mzunguko. Na hapo sio mwisho.

Na utamu hapo ni pale mteja anayefuata (M4) anapokuwa serikali, utakosa pesa ya kuikopesha?

Na unaweza kuta hata ile 1,000TZS ni pesa ambayo engineer flani amelipwa na mkandarasi kwa pesa ambayo imetoka kwa serikali, ambayo serikali imekopa kutoka kwa benki yako.

Sasa hapo utaona jinsi gani banks na sio bureau de change zinaweza kusaidia inflation kwa sababu wana uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza fedha (yaani ni kama ku-print notes).

Tunajua kwamba ongezeko la money supply ndio linalosababisha inflation. Yaani kunakuwa na pesa nyingi zaidi ya zinazohitajika kwa ajili ya kuimarisha bei za vitu. Na kwa kuwa mabenki yana uwezo kwa kutengeneza pesa, na uwezo huu upo nje ya uwezo wa serikali, utaona kwa nini inaweza kuwa ngumu sana saa nyingine kwa serikali ku-control inflation.

Kwa hiyo ukiona watu wanakuwa-encouraged sana kukopa, anza kuangalia kwa mtazamo tofauti kidogo. Waofaidika kwa kiasi kikubwa ni mabeki wakati sisi wengine wote tunaingizwa kwenye madeni, hasa pale pesa hizi zinpokuwa zinazunguka bila kuzalisha.
 
Ahsante Manitoba kwa maelezo yako mazuri. Kwa Tanzania sera ya fedha na utekelezaji wake haufanywi inavyotakiwa. Mathalani moja ya mashtaka ya wakubwa wa BoTwaliofikishwa mahakamani juzi ni kuchapisha hela in eccess. Kwahiyo ile calculated reserve haiwezi kulingana na hela iliyoko kwenye mzunguko kwa sababu kuna mianya mingi ya kuingiza fedha chafu kwenye huo mzunguko.

Sadakta!

Suala la bureau de change linakuja kutokana kwamba anayepata hizi hela nyingi nje ya utaratibu atataka kuzihamishia nje ya nchi zikiwa in form of dolar or euro etc. Historia inaonyesha waafrica wanapenda kuficha mahela yao nje.

Nakubaliana na wewe kwamba Bureau de change zinaweza kutumika kama mianya ya kupitishia pesa kupeleka nje. Lakini hizo sio njia pekee. Na mtu mwenye Billion 100 anataka kuzipeleka nje, ataenda Bureau de change ipi? Au aytapita kwenye moja moja na kukusanya kidogo kidogo? Na akishabadilisha ataondoka nazo kwenye masanduku? Sisemi kwamba haziwezi kutumika, lakini sijawa convinced kwamba Bureau de change zinanipa wasiwasi kihivyo.
 
Off topic kidogo, lakini kuna-kitu kimoja interesting ambacho wengi hatukijui: fedha zako inwezekana si zako. Hata serikali yako haina pesa. Pesa zote unazoziona ni mikopo.

Hebu jiulize, serikali ikitaka pesa inafanyaje? Inakopa kutoka kwa benki kuu au kutoka kwa watu binafsi kwa kupitia benki kuu, na riba kubwa tu. Cha kushangaza hapa ni kwamba serikali ambayo pengine ndiyo ingebidi iwe mmiliki wa hizo pesa inabidi ikope na tena ilipie mkopo huu riba.

Serikali inapata wapi pesa sa kulipa deni hilo? Ni kwa kutukata sisi kodi. Ndio maana sehemu ya kodi tunayolipa lazima iende kwenye kulipa deni hilo, na inayobaki ndio tunaigawa-gawa kwenye bajeti.

Kwa hiyo serikali yetu huwaga haina pesa. Sasa kama haina pesa je, supply ya fedha huwa inakuwa controled vipi?

Kumbuka supply ya fedha ikiwa kubwa kuliko ambavyo uchumi unaruhusu tuna inflation kwa sababu thamani yake inshuka. Supply ikiwa ndogo, tunakuwa na deflation ambayo inaweza kuwa mbaya zaidi.

Unaweza ukalia ukijua ukweli.

Ili ku-control inflation inabidi kuondoa fedha kwenye mzunguko. Kufanikisha hili inabidi kupunguza matumizi yake. Na tunajua jinsi hii inavyokuwa tofauti na malengo ya kisiasa.

Ili ku-control deflation inabidi kuongeza pesa kwenye mzunguko. Lakini kwa kuwa serikali haina pesa, inabidi kwenda kukopa tena. Na hiyo inamaanisha riba inaongezeka. Itatoa wapi hii riba? Tunakamuliwa kodi!

Sasa kuna watu wachache ambao wao wanakula kuku kwa mrija. Kazi yako ni kuikopesha serikali na kusubiri riba. Hawa watu hawawezi kulala njaa kwa sababu serikali tayari iko kwenye deni na haina pesa, na inahitaji kukopa.

Sasa jiulize hawa watu wanatoa wapi pesa za kuikopesha serikali ambazo haziishi?

Pengine tujiulize hawa watu ni wakina nani? Kwanza ni Benki Kuu lakini kwa hapa TZ Benki kuu tunaweza kusema ni ya serikali (pengine kwa kuangalia juu juu), kwa hiyo pengine tuko safe kuliko wamarekani kwa mfano. Pili ni mabenki.

Hivi unajua mabenki yanatengeneza fedha? Nnaposema kutengeneza fedha simmanishi kuzalisha kama tunavyomaanisha tukiwa mtaani. Namaanisha ni kama vile kuchapisha pesa, na kuziingiza kwenye mzunguko

Chukulia wewe n benki, na ukapokea deposit ya buku moja, 1,000TZS kutoka kwa mteja M1. Mteja M2 anakuja anataka mkopo wa 900TZS. Unampa 900TZS. Kwa hiyo M1 anasema na 1,000TZS na M2 akiulizwa anasema na 900TZS. Jumla una 1,900TZS. Kwa bahati M2 ana-deposit hiyo 900 yake kwenye account iliyo kwenye benki yako. Anakuja M3 naye anataka 800TZS. Kutoka kwa 900 ya M2 unatoa 800 unampa M3. Mpaka sasa tuna 2,700TZS. Kwa hiyo benki yako kwa kupokea 1,000TZ ya deposit imeweza kutengeneza pesa kiasi cha 1,700TZS na kukiingiza kwenye mzunguko. Na hapo sio mwisho.

Na utamu hapo ni pale mteja anayefuata (M4) anapokuwa serikali, utakosa pesa ya kuikopesha?

Na unaweza kuta hata ile 1,000TZS ni pesa ambayo engineer flani amelipwa na mkandarasi kwa pesa ambayo imetoka kwa serikali, ambayo serikali imekopa kutoka kwa benki yako.

Sasa hapo utaona jinsi gani banks na sio bureau de change zinaweza kusaidia inflation kwa sababu wana uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza fedha (yaani ni kama ku-print notes).

Tunajua kwamba ongezeko la money supply ndio linalosababisha inflation. Yaani kunakuwa na pesa nyingi zaidi ya zinazohitajika kwa ajili ya kuimarisha bei za vitu. Na kwa kuwa mabenki yana uwezo kwa kutengeneza pesa, na uwezo huu upo nje ya uwezo wa serikali, utaona kwa nini inaweza kuwa ngumu sana saa nyingine kwa serikali ku-control inflation.

Kwa hiyo ukiona watu wanakuwa-encouraged sana kukopa, anza kuangalia kwa mtazamo tofauti kidogo. Waofaidika kwa kiasi kikubwa ni mabeki wakati sisi wengine wote tunaingizwa kwenye madeni, hasa pale pesa hizi zinpokuwa zinazunguka bila kuzalisha.
Nadhani kuna point ya kuhighlight pia. Serikali ndio msimamizi na mmiliki wa benki kuu. Sasa benki kuu wakisema akiba yetu ya fedha ya kigeni natosha miezi nane, wanamaanisha mkopo??? Nadhani jibu ni hapana. Naomba ni tofautiane na wewe kwahili si kwamba serikali hawana pesa, wana pesa na wanamamlaka hata ya kuprint fedha ya ziada. Lakini sasa wakiprint hiyo fedha, effect yake ndio inflation uliyoitaja na in the end consumer wanaloose appetite ya local currency.
Labda kucement hii point, nadhani ipo haja ya kufaham kuwa katika finacial markets (masoko ya fedha), utaona securities (dhamana) za serikali zinakuwa a return( interest), riba kidogo. Sababu kubwa ni underlying assumption that the government cannot default. Maana yake ni kwamba serikali kama ilivyo inauwezo wa kuprint notes, pesa za ziada pale itakapohitajika kulipa na ndio maana risks iliyopo kwenye dhamana zake huwa ni ndugu kuliko dhamana binafsi na za makampuni na hata hiyo riba inabidi iwe kidogo. Kwahiyo serikali inuwezo wa kutengeneza fedha ya ziada, rejea ishu ya zimbambwe na kwa maana hiyo serikali inaweza kuwa na pesa but while accounting for fiscal and monetary policy.
Hoja ya bureau, mfano wako ni mzuri saaana. Lakini kwa wale wanaosema bureau zinatumika kuhamisha pesa, hapana hii si kweli kuna procedures zimeongezeka tokea March mwaka huu hata kutransfer pesa nje inayozidi 10mil BOT wanahitajika kuidhinisha. Kwahiyo ishu is rahisi hivyo. Labda ukizungumzia issue ya speculation kwa hawa wanaofanya bashara ya pesa inaweza kuwa sahihi na hii inafanywa popote duniani ila Tanzania u can always bet the market b'se the market itself has never been efficiency.
Suala la KILIMO KWANZA ni technique nzuri saana kuinua uchumi wa nchi yetu kama tu siasa itawekwa kando. Tukweza kuzalisha na hata tusiwaze kuuza Ulaya na Marekani, bado Afrika kuna msoko ya kutosha kwenye vyakula. Jirani zetu hapo Kenya, they have always been starving. Ukweli kwenye kilimo bado kuna opportunities.
 
Manitoba,

Swali - je ni nini kisababisha chenzake kati ya doralization* na kushuka kwa thamani ya TZS? Je ni doralization ndio inachangia thamani ya hela yetu kudorola au ni thamani ndogo ya hela yetu ndio inasababisha doralization?

*doralization - tabia ya baadhi ya watu nyumbani kupanda bei kwa kutumia dollar.
 
Nadhani kuna point ya kuhighlight pia. Serikali ndio msimamizi na mmiliki wa benki kuu. Sasa benki kuu wakisema akiba yetu ya fedha ya kigeni natosha miezi nane, wanamaanisha mkopo??? Nadhani jibu ni hapana. Naomba ni tofautiane na wewe kwahili si kwamba serikali hawana pesa, wana pesa na wanamamlaka hata ya kuprint fedha ya ziada. Lakini sasa wakiprint hiyo fedha, effect yake ndio inflation uliyoitaja na in the end consumer wanaloose appetite ya local currency.
Labda kucement hii point, nadhani ipo haja ya kufaham kuwa katika finacial markets (masoko ya fedha), utaona securities (dhamana) za serikali zinakuwa a return( interest), riba kidogo. Sababu kubwa ni underlying assumption that the government cannot default. Maana yake ni kwamba serikali kama ilivyo inauwezo wa kuprint notes, pesa za ziada pale itakapohitajika kulipa na ndio maana risks iliyopo kwenye dhamana zake huwa ni ndugu kuliko dhamana binafsi na za makampuni na hata hiyo riba inabidi iwe kidogo. Kwahiyo serikali inuwezo wa kutengeneza fedha ya ziada, rejea ishu ya zimbambwe na kwa maana hiyo serikali inaweza kuwa na pesa but while accounting for fiscal and monetary policy.
Hoja ya bureau, mfano wako ni mzuri saaana. Lakini kwa wale wanaosema bureau zinatumika kuhamisha pesa, hapana hii si kweli kuna procedures zimeongezeka tokea March mwaka huu hata kutransfer pesa nje inayozidi 10mil BOT wanahitajika kuidhinisha. Kwahiyo ishu is rahisi hivyo. Labda ukizungumzia issue ya speculation kwa hawa wanaofanya bashara ya pesa inaweza kuwa sahihi na hii inafanywa popote duniani ila Tanzania u can always bet the market b'se the market itself has never been efficiency.
Suala la KILIMO KWANZA ni technique nzuri saana kuinua uchumi wa nchi yetu kama tu siasa itawekwa kando. Tukweza kuzalisha na hata tusiwaze kuuza Ulaya na Marekani, bado Afrika kuna msoko ya kutosha kwenye vyakula. Jirani zetu hapo Kenya, they have always been starving. Ukweli kwenye kilimo bado kuna opportunities.

Kwa fedha za kigeni, mfano uliotoa unaonyesha kwamba BOT ni banker tu wa serikali. Je wewe CRDB akiwa ni banker wako, haiwezekani account yako ya dolar ikawa positive wakati account yako ya TZS ikawa negative? Je, hata kama una account moja mbili zilizo positive, haiwezekani jumla ya pesa ulizo nazo kwa benki hiyo zikawa negative (kama kwa mfano kuna account ome overdraw kupita kiasi?

BOT waki-print fedha kuna mawili.

Kwanza kuna ku-replace fedha zilizochakaa. Fedha zilizochakaa zinarudishwa BOT na BOT wanatoa fedha mpya.

Pili, serikali ikipewa pesa na BOT nje ya pesa zilizo kwenye account za serikali ndani ya BOT, haipewi bure baba. Inakopeshwa kwa riba. Uhusiano wa serikali na BOT hauna tofauti na wewe na CRDB au NMB kama banker wake. Ila kwa sababu siasa zetu zinaruhusu muingilione, then tunaweza tukadhani kila kilichopo BOT ni cha serikali. Na tushaona madhara ya muingiliano huu.
 
Manitoba,

Swali - je ni nini kisababisha chenzake kati ya doralization* na kushuka kwa thamani ya TZS? Je ni doralization ndio inachangia thamani ya hela yetu kudorola au ni thamani ndogo ya hela yetu ndio inasababisha doralization?

*doralization - tabia ya baadhi ya watu nyumbani kupanda bei kwa kutumia dollar.
Natambua limemlenga Manitoba lakini naomba kuchangia. Dollarization ni matokeo tu, ila behind dollarisation ndio kuporomoka kwa shilingi. Shilingi ingekuwa stable dollarisation isingekuwepo. Refer Zimbabwe. Lakini shilingi imekuwa weak na watu wanafanya biashara zao kwa kuimport raw materials na other products. Sasa unaimport leo just after days vitu kabla bidhaa haijafika exchange rates zinabadilika, unategemea nini. Hapo ndio maana watu wakaopt kwa dollarisation. Lakini option hii ndio ikafanya hali ya shilingi iwe mbaya zaidi maana hakuna anayetaka kuitumia, kwa maneno mengine dollarisation has created weak demand for Tsh. Hapo kazi ikaongezeka people are shunning away from Tshs. Inamaana Tsh is becoming cheaper na ndio matokeo yanayoonekana.
 
Manitoba,

Swali - je ni nini kisababisha chenzake kati ya doralization* na kushuka kwa thamani ya TZS? Je ni doralization ndio inachangia thamani ya hela yetu kudorola au ni thamani ndogo ya hela yetu ndio inasababisha doralization?

*doralization - tabia ya baadhi ya watu nyumbani kupanda bei kwa kutumia dollar.

Swali zuri kupita yote.

Ili currency yoyote ifaye kazi lazima kuwe na trust. Lazima watumiaji waamini kwamba currency hiyo thamnani yake ni stable. Wasipoamini hivyo watapunguza matumizi yake au kuacha kabisa. Na thamani yake itazidi kuporomoka. Trust ni muhimu kwa currency yoyote. Hata kama umei-peg kwa gold, lazima mtu aamini kwamba thamani ya gold haitashuka over time.

Dolarization ni dalili tu kwamba watu hawaiamini thamnani ya Tanzanian Shilling (TZS). Na kwa maoni yango hii ni dalili ya ugonjwa na sio ugonjwa.

Tatizo sasa sisi badala ya kutatua matatizo yanayofanya watu wasiwe na imani na currency hiyo (yaani kutibu ugonjwa), tunataka kuwalazimisha waitumie kwa nguvu (tunatibu dalili). Hiyo itafanya kazi in the short run, lakini in the long run haitasaidia.

If the worse comes to the worse, utakuwa watu wanaanza kubadilishana vitu kuepuka kutumia TZS. Je, utapendekeza tuweke sheria kwamba watu hawaruhusiwi kubadilishana vitu? tehetete

Solve the core problems, au mvumilie tu madhara ya inflation. Huwezi kuwalazimisha watu watumie currency wasiotaka. Wataizunguka tu. Angalia kinachotokea Zimbabwe.
 
Kwa fedha za kigeni, mfano uliotoa unaonyesha kwamba BOT ni banker tu wa serikali. Je wewe CRDB akiwa ni banker wako, haiwezekani account yako ya dolar ikawa positive wakati account yako ya TZS ikawa negative? Je, hata kama una account moja mbili zilizo positive, haiwezekani jumla ya pesa ulizo nazo kwa benki hiyo zikawa negative (kama kwa mfano kuna account ome overdraw kupita kiasi?

BOT waki-print fedha kuna mawili.

Kwanza kuna ku-replace fedha zilizochakaa. Fedha zilizochakaa zinarudishwa BOT na BOT wanatoa fedha mpya.

Pili, serikali ikipewa pesa na BOT nje ya pesa zilizo kwenye account za serikali ndani ya BOT, haipewi bure baba. Inakopeshwa kwa riba. Uhusiano wa serikali na BOT hauna tofauti na wewe na CRDB au NMB kama banker wake. Ila kwa sababu siasa zetu zinaruhusu muingilione, then tunaweza tukadhani kila kilichopo BOT ni cha serikali. Na tushaona madhara ya muingiliano huu.
Hiyo kaka ni nadharia tu. Nadhani we need to ge back kuangalia roles za central banks. Uhusiano wangu na CRDB au NMB haulingani kamwe na BOT. Nani anasimamia BOT? Utagundua ni serikali. Policies zote za fedha zinaandaliwa na BOT, unadhani kwanini? BOT ni entity ya Serikali, ukijitahidi kuwatofautisha ni kinadharia tu. Ndio maana hata dhamana za serikali na kucontrol money circulation hiyo kazi inafanywa na BOT kwa niaba ya serikali is nt about Banker. Inamaana taarifa ya benki kuu sio ya serikali. Mf Akiba ya fedha ya kigeni tunachokiasi kadhaa......... ni kina nani kama si serikali?
Hv unadhani tumefikaje kwenye notes za TSh 10,000. Hii ni madhara ya inflation ambayo yanauhusiano na extra notes printing. Ingekuwa wanareplace tu?????
 
Natambua limemlenga Manitoba lakini naomba kuchangia. Dollarization ni matokeo tu, ila behind dollarisation ndio kuporomoka kwa shilingi. Shilingi ingekuwa stable dollarisation isingekuwepo. Refer Zimbabwe. Lakini shilingi imekuwa weak na watu wanafanya biashara zao kwa kuimport raw materials na other products. Sasa unaimport leo just after days vitu kabla bidhaa haijafika exchange rates zinabadilika, unategemea nini. Hapo ndio maana watu wakaopt kwa dollarisation. Lakini option hii ndio ikafanya hali ya shilingi iwe mbaya zaidi maana hakuna anayetaka kuitumia, kwa maneno mengine dollarisation has created weak demand for Tsh. Hapo kazi ikaongezeka people are shunning away from Tshs. Inamaana Tsh is becoming cheaper na ndio matokeo yanayoonekana.

Kama nimekuelewa vizuri - kwa hiyo mwanzo ilikuwa thamani ndogo ya shiling ilisababisha dollarization. Lakini mara dollarization ilipoota mizizi ika-take over na kudidimiza shilling. Au sio?

Kama uelewo wangu hapo juu ni sahihi, basi inamaana kwamba kama benki kuu wakiweza kudhibiti ishu ya dollarization, basi wanaweza kuikoa shilling kwa kiasi fulani. Si ndio?

Kwa sababu, demand ya dollar imeongozeka maradufu mara baada ya baadhi ya wafanya biashara kujiingiza kwenye dollarization system. Hivyo basi, ili kuweza kuinua thamana ya Tshs angalau kiduchu, itabidi dollarization idhibitiwe. Matokeo safari za kwenda kubadilisha hela zitapungua, na mwishowe Bureau De Change watapunguza bei za Dollar.
 
Hiyo kaka ni nadharia tu. Nadhani we need to ge back kuangalia roles za central banks. Uhusiano wangu na CRDB au NMB haulingani kamwe na BOT. Nani anasimamia BOT? Utagundua ni serikali. Policies zote za fedha zinaandaliwa na BOT, unadhani kwanini? BOT ni entity ya Serikali, ukijitahidi kuwatofautisha ni kinadharia tu. Ndio maana hata dhamana za serikali na kucontrol money circulation hiyo kazi inafanywa na BOT kwa niaba ya serikali is nt about Banker. Inamaana taarifa ya benki kuu sio ya serikali. Mf Akiba ya fedha ya kigeni tunachokiasi kadhaa......... ni kina nani kama si serikali?
Hv unadhani tumefikaje kwenye notes za TSh 10,000. Hii ni madhara ya inflation ambayo yanauhusiano na extra notes printing. Ingekuwa wanareplace tu?????

Kwahiyo unataka kusema serikali ikitaka pesa inaenda kujichotea tu BOT? Mimi naamini uhusiano kati ya BOT naserikali hauna tofauti na uhusiano wa CRDB na wewe kama account holder wa CRDB na wewe mfano ni mmoja wa directors wa CRDB. Kama wewe ni mmoja wa directors wa CRDB, unaweza tu kwenda kujikopea unavyotaka? Je, unaweza kwenda kujichote tu pesa pale?

Nadhani hata commercial banks zina accounts BOT, kama vile ambavyo serikali ina accounts BOT.

Tena shukuru hapa serikali ndio inasimamia BOT. Unajua kwamba Federal Reserve ya marekani ni partly privately owned organization?
 
Kama nimekuelewa vizuri - kwa hiyo mwanzo ilikuwa thamani ndogo ya shiling ilisababisha dollarization. Lakini mara dollarization ilipoota mizizi ika-take over na kudidimiza shilling. Au sio?

Kama uelewo wangu hapo juu ni sahihi, basi inamaana kwamba kama benki kuu wakiweza kudhibiti ishu ya dollarization, basi wanaweza kuikoa shilling kwa kiasi fulani. Si ndio?

Kwa sababu, demand ya dollar imeongozeka maradufu mara baada ya baadhi ya wafanya biashara kujiingiza kwenye dollarization system. Hivyo basi, ili kuweza kuinua thamana ya Tshs angalau kiduchu, itabidi dollarization idhibitiwe. Matokeo safari za kwenda kubadilisha hela zitapungua, na mwishowe Bureau De Change watapunguza bei za Dollar.
Very true inawezekana tatizo likapungua. Lakini impact yake sasa inawezekana kuwa kubwa zaidi ya kuzuia matumizi ya dollar. Maana hakuna mfanyabiashara ambaye yupo tayari kuuza kwa hasara. Hata kama ukiamua kutumia Tshs, curency yenyewe sio stable inamaana utabadilisha bei mara ngapi. Je customers implication inakuwa wapi hapo? Cha kufanya ni kutokimbizana na wafanyabiashara. Wao wahakikishe wanasound Macro economic policy. Ikibidi hata intervention ingawa sio proper approach. Angalia Japan na China, wao wanaintervene saana fadha zao ndio maana Marekani wanalalamika kila asubuhi.
Kubwa zaidi ni kuhakikisha kuna balance kati ya export na import, hizi zinachangia saana uimara wa shilingi
 
Kama nimekuelewa vizuri - kwa hiyo mwanzo ilikuwa thamani ndogo ya shiling ilisababisha dollarization. Lakini mara dollarization ilipoota mizizi ika-take over na kudidimiza shilling. Au sio?

Kama uelewo wangu hapo juu ni sahihi, basi inamaana kwamba kama benki kuu wakiweza kudhibiti ishu ya dollarization, basi wanaweza kuikoa shilling kwa kiasi fulani. Si ndio?

Kwa sababu, demand ya dollar imeongozeka maradufu mara baada ya baadhi ya wafanya biashara kujiingiza kwenye dollarization system. Hivyo basi, ili kuweza kuinua thamana ya Tshs angalau kiduchu, itabidi dollarization idhibitiwe. Matokeo safari za kwenda kubadilisha hela zitapungua, na mwishowe Bureau De Change watapunguza bei za Dollar.

Naomba nitofautiane kidogo.

Kinachoanza si dolarization. Dolarization inafuata baada ya thamani ya shilingi kuanza kutokuaminika. Its all about Trust.

Kuelezea kwa kutumia supply and semand ni ku-simplify kinachotokea. Inasaidia kuelewa, lakini sio the whole truth.
 
Back
Top Bottom