Adam Malima tumbo joto.
Sijawahi kuzingatia jambo lolote lisemwalo na Lukuvi, sijui kwanini!
apo ndo shida inapokuja
Wabunge wamezomea maana wamechoka na tabia ya Serikali kutaka kupelekewa majina ilhali Mkuu wa Nchi alisema anayo,kwanini wasianze na hayo?
Hivi kazi ya serikali ni KUTAJA MAJINA AU KUCHUKUA HATUA. Unataja majina unamtajia nani badala ya kuwachukulia hatua. We umekamata kina dada na ma bag ya madawa si waulize tu mabegi ni ya nani kisha uwachukulie hatua. Ni aibu sana kauli kama hizo kubungeni. Only in Tanzania!
Mimi nna ushahidi 100% wa mtu wa karibu yangu but sijui ni upeleke wapi..maana amesababisha maafa makubwa kwenye ukoo....maana police ndo kwanza wanamfata anawapa rushwa
Bunge limeanza leo mjini Dodoma na sasa ni kipindi cha maswali na majibu ambapo hoja inayoendelea kwa sasa ni wabunge kutaka wahusika wa biashara ya madwa ya kulevya watajwe.Waziri Lukuvi ameahidi kuwataja na ametaka mwenye ushahidi apeleke.Hata hivyo, wabunge wamemzomea na spika ameonya hiyo tabia ya kuzomea.
Baadhi ya wabunge waliotaka majina yatajwe ni mh.Mama Kilango wa CCM na mbunge wa karatu kupitia CHADEMA ambae amehoji inakuwaje hata Raisi amekiri kuwa na orodha ya wauza unga bila wahusika kutajwa na kuchukuliwa hatua.
Hata hivyo,waziri Lukuvi amesisitiza umuhimu wa kuwa na ushahidi kwani amesema kama ni kutajwa tu na wengine wamo humu bungeni na ameongeza hata gazeti la Jambo leo limewataja kwahiyo kitu muhimu ni ushahidi na sio kutaja tu.
Vile vile mh.Lukuvi ameeleza nia ya serikali kubadilisha sheria ili madawa ya kulevya yakishakamatwa na ushahidi kupatikana(kuwa kwenye kumbukumbu) basi madawa hayo yaharibiwe mara moja kuliko utaratibu wa sasa ambao madawa hayo huhifadhiwa mpaka kesi husika kuisha na ametoa mfano wa madawa kuwekwa kwa miaka hata kumi kusubiri kesi ikamilike.
MY TAKE:KAMA RAISI AMESHINDWA KUTAJA HAO VIGOGO HADHARANI, LUKUVI ATAWEZA VIPI?
anatoka na gari la umma kuelekea kazini huku raia wengine wakitakiwa kulipisha, alafu anafika ofisini kwenye kiti cha kuzunguka huku kiyoyozi kikiendelea kupuliza. ....anangojea wananchi walete ushahidi!Eti polisi kakaa sebuleni kwake anasema apelekewe ushahidi! Kuna wakati huwa najiuliza kuwa wajibu wao ni nini hasa?