Bungeni: Julai 26, 2012

Na kama anataka na yeye apite huko kwao! kwanza na mshangaa aolewe Mtera aje agombee Same Wapare nao wanampa kura
 
Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema mwanasiasa anayeongelea watu badala ya sera ana matatizo ya upeo wa uelewa. Mh. Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati akijbu swali la Mbunge wa Same Mashariki, ANNE KILANGO aliyetaka kujua hatua gani Serikali inachukua kwa wabunge wanaokwenda kwenye majimbo ya wabunge wenzao na kutoa maneno yenye dalili za kuhatarisha amani na ambayo yanaweza kuliingiza taifa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe.
 
Huyu sasa anaiita M4C kwa nguvu hata kama hawakuwa na ratiba ya kupita jimboni kwake!

Chama cha msimu kinamsumbua nini jamani?

Hivi nchi hii ina sheria inayomzuia mwanasiasa yeyote kupita katika Jamhuri hii na kueleza sera zake za kisiasa?

Tena hjimbo la Same wanatakiwa wakae wiki nzima!...Amewadanganya siku nyingi watu wa jimbo lake kuwa analeta mitambo ya kusindika hoho na pilipili mbuzi!
 
Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema mwanasiasa anayeongelea watu badala ya sera ana matatizo ya upeo wa uelewa. Mh. Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati akijbu swali la Mbunge wa Same Mashariki, ANNE KILANGO aliyetaka kujua hatua gani Serikali inachukua kwa wabunge wanaokwenda kwenye majimbo ya wabunge wenzao na kutoa maneno yenye dalili za kuhatarisha amani na ambayo yanaweza kuliingiza taifa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Kama wanavyofanya CCM chama tawala lakini kimekuwa kama cha Upinzani muda wote wanazungumzia ndoa ya Slaa wakati wanazo ahadi 70 za Mr Dhaifu za kutekeleza
 
Si mlisema ni vyama vya MSIMU iweje leo mnapiga mayowe!

BTW Mama Anna Kilango nani kamukataza kwenda kwenye majimbo ya upinzani na kuwakosea?

Kwa hiyo Mama kilango alitaka Wapinzani wapite kwenye majimbo "yao" na kuwasifia?
Still living in one party politics, Wake up, that era has gone dude.
 
Naona hajuhi kuwa Tanzania ni moja,na vyama vya siasa ni vya nchi nzima,si vya kijimbo.Chama kina haki ya kuendesha shughuli zake Eneo lote la Tanzania Bara..

Waziri Mkuu amejibu vizuri tu kuwa wana haki ya kufanya hivyo,ila wasilenge wantu binafsi katika hotuba zao bali wanadi sela zao na kulenga Issues za kitaifa.
 
Source: Bunge-maswali ya papo kwa hapo.
Sasa yeyote anaweza kufanya chochote kinachoenda kinyume na Katiba alimradi tu itasaidia kufanya mambo yaende vizuri! Swali langu kila mtu/taasisi ikitaka kufanya hivi kwa justification zao itakuwa sawa? Au ni kwa wachache wenye mkono mrefu zaidi ya wa sheria na katiba?

Mh. Pinda alikua akijibu hoja ya mh. Msigwa kwanini wakaazi wote wa Zanzibar walazimishwe kutii masharti ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, bila kujali imani za dini nyingine? Na kwamba huku si kusema upande mmoja wa Muungano ni wa kiislamu na mwingine sio?

Na hata lile la Anne Kilango, ati majimbo Yao yanaingiliwa na wanasiasa kutoka maeneo mengine, kwani haya majimbo yameandikwa owners wao hivyo wasiingiliwe? Hii ownership ya majimbo kwa individuals iko kikatiba au?
 
Katika kikao cha leo cha bunge Mbunge Anne Kilango Malecela amemuomba Waziri mkuu atoe kauli ya Serikali juu ya suala la Vyama vya siasa kupita kwenye majimbo ya wenzao na kuwakosoa:

My take.
CCM ni dhahiri wamejeruhiwa na CHADEMA

Huyu Bi Mkora Anne Kilango anaweseseka maana anajua mwaka 2015 hana tena Ubunge jimboni kwake!!!Mama ana wasiwasi sana na CHADEMA. Huu ni upumbavu na upuuzi kwa Wabunge wa CCM kufikiri kwamba wapinzani hawaruhusiwi kupita kwenye majimbo yanayoongozwa na CCM. Huu ni ujinga ambao unatakiwa ukemewe kwa nguvu zote.

Je,ina maana CCM nao wasiruhusiwe kupita kwenye majimbo yanayoongozwa na CHADEMA???Kweli wabunge wa CCM wamechoka na kinachotakiwa ni kuwapumzisha once and for all! Pumbaf zao.

 
Natamani Waziri Mkuu amkumbushe Mama Kilango yafuatayo:

a) Sheria ya vyama vya siasa inataka kabla ya kuandikishwa, chama mwombaji kithibitishe kuwa na wanachama wasiopungua 200 kutoka kila mkoa wa JMT (bila kujali wanatoka jimbo gani!!)
b) Katiba ya nchi, haimzuii mgeni wala mTanzania kwenda sehemu yoyote ya nchi!!

Lakini sina imani na Pinda, ni tatizo kuu la pili kwa nchi hii.
 
Huu muungano ufutwe tu...Pinda kaulizwa atoe kauli kama serikali ya upande mmoja ina dini(zanzibar) na huku bara hakuna dini....lalkin PM hajatoa jibu la msingi
 
Na yeye azunguke kwenye majimbo ya wenzake kumwaga sera hajakatazwa.:A S-baby:
 
Waziri Mkuu wetu ameshindwa kujibu kuhusu serikali ya SUK kuagiza migahawa, mamantilie kufunga shughuli zao za kuuza vyakula wakati wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Mchungaji Msigwa alitaka WM aseme Zanzibar ni nchi ya Kiislamu. WM amekwepa maswali yote hayo.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Peter Pinda amesema mwanasiasa anayeongelea watu badala ya sera ana matatizo ya upeo wa uelewa. Mh. Waziri Mkuu ameyasema hayo wakati akijbu swali la Mbunge wa Same Mashariki, ANNE KILANGO aliyetaka kujua hatua gani Serikali inachukua kwa wabunge wanaokwenda kwenye majimbo ya wabunge wenzao na kutoa maneno yenye dalili za kuhatarisha amani na ambayo yanaweza kuliingiza taifa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Wamiliki wa majimbo ni wananchi wenyewe na sio mbunge/wabunge. Kila mtanzania ana haki ya kwenda mahali popote na kuongea na yoyote, Anne Kilango asome katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa makini. Mwaka jana yeye mwenyewe Kilango alikuwa Kiwira akifanya campaign, kama wenyeji wa huko wangekuwa na mtazamo kama wake asingetakiwa awe huko Kiwira. Na huu uwoga unatoka wapi kama umefanya kazi vizuri?
 
Adai wakiristo wa Zanzibar wanaonewa.hii ni wazi waislam wanaposema Chadema kipo kwa ajili ya kutetea kanisa sasa imepata nguvu.
hata wale wanaopinga sasa hawana hoja.
mungu anusuru chadema kushika nchi. vita vya kidini vitazuka
 
Back
Top Bottom