Danisamweswa
JF-Expert Member
- Jun 26, 2013
- 453
- 154
Sijui atachukua mikoba ya Kinana?
Sijui atachukua mikoba ya Kinana?
hahahah mbona hakushinda pamoja na wizi wenu.... hehehe lyatonga anadaiwa milioni AROBAINI kwa ujinga wake... ccm imechokwa ndio na ndo maana zile sehemu zooote ambapo wananji wenye akili haijapita... kule wananji walipozubaa na kupenda ubwabwa maharagwe na vitenge +kofia za kijani waliibiwa kura na huo ndio ukweliUlimchoka wewe na nani acha kuingilia yasiokuhusu nyumbu wewe
Acheni visasi jengeni chama
Abdallah Bulembo, amesema, wote walio kisaliti CCM katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana, waanze kujiondoa mapema ndani ya chama hicho vinginevyo watang’olewa baada kufanyika tathimini ya uchaguzi.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo, amesema, wote walioisaliti CCM katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana, waanze kujiondoa mapema ndani ya chama hicho vinginevyo watang’olewa baada kufanyika tathimini ya uchaguzi.
Bulembo alisema kuwa chama hicho kipo mbioni kufanya tathimini ya kina kuanzia ngazi ya shina hadi taifani kuwabaini wasaliti waliochangia kukidhoofisha chama wajulikane na kwamba wote watakaobainika wataondolewa bila kuangaliwa vyeo na mahali walipo.
“Wapo watu ndani ya CCM walitusaliti katika uchaguzi uliopita hayo ni sehemu ya majipu mengi na lazima tuyatumbue, mtanuna sana lakini chama hakiwezi kuendelea kuwakumbatia wasaliti kama hao,” alionya Bulembo.
Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 61 ya Jumuiya ya Wazazi, yaliyofanyika kitaifa mkoani Morogoro sherehe zilizohudhuriwa na viongozi wa kitaifa wa mikoa na wilaya wa chama hicho, juzi, alikumbusha kuwa wakati umefika wa kujitathmini.
Bulembo, alieleza kuwa uchaguzi umekwisha na sasa viongozi walioshinda kila mmoja afanye kazi ya kuwatumikia wananchi kwani serikali iliyopo madaraka inayongozwa na CCM imeonyesha uwezo wa kuwatumikia Watanzania lakini wakati hayao yakiendelea ni lazima CCM ifanye tathimini.
Alitoa tahadhari kuwa tathimini hiyo haitofanywa kwa chuki binafsi au kwa kumuonea mtu badala yake uwepo wa ushahidi wa kutosha wa kisaliti ndicho kigezo cha kushughulikia waliohusika.
Kadhalika aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani pamoja na wanachama wao kuacha kutoa maneno ya kumkatisha tamaa na kumbeza Rais John Magufuli kwakuwa anaonyesha kasi nzuri ya utendaji kwa manufaa ya Watanzania.
Alisema kuwa jumuiya hiyo imeridhishwa na uchapaji kazi na kasi ya utendaji wa Rais Dk Magufuli,ikiwamo kudhibiti upotevu wa mapato ya serikali na kuvitaka vyama vya upinzani kumuunga mkono kwa kazi nzuri anayofanya.
Alisema Dk Magufuli pamoja na Baraza la Mawaziri kwa muda mfupi wamerudisha heshima ya nchi kutokana na kuwawajibisha watendaji wasio waadilifu na mafisadi bila kuwaonea haya hivyo anapaswa kuungwa mkono ili aweze kuwatumikia Watanzania.
Awali Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Morogoro Meck Mdaku, aliwataka wanachama wa CCM kuvunja makundi kwani yanakidhoofisha chama na wakati mwingine kukinyima ushindi.
Alisema kuwa jumuiya hiyo imekiimarisha chama kuanzia ngazi ya shina hadi taifa na kwamba imeweza kuhakikisha chama kinapata ushindi katika uchaguzi uliopita.
Source: Nipashe
Umeongea kweli Kamanda. Maana wakimwacha Mzee Wa msoga na mwanae hatutakubali na sisi kuondolewaMtamaliza chama maana hakuna msafi