nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
BRIGEDIA Jenerali mstaafu Hashim Mbita ameionya serikali kama hakutakuwa na majadiliano baina yake na wananchi uwezekano wa kuvunjika kwa amani ni mkubwa.
Mbita alitoa onyo hilo jana jijini Dar es Salaam katika kongomano la uundwaji wa jukwaa la taifa la Asasi za Kiraia (AZAKI) la kitaifa na la kikanda.
Alisema tatizo kubwa lililopo katika serikali na utawala wa nchi nyingi za ukanda wa Afrika ikiwemo Tanzania ni kutokuwa na majadiliano ya pamoja kati yao na wananchi.
Shida kubwa iliyopo ni kukosa majadiliano ya pamoja kati ya watawala na raia, amani na utulivu inaweza kutoweka kwenye ukanda wa nchi za Afrika endapo majadiliano hayo hayatakuwepo, alisema Jenerali Mbita.
Akitolea mfano kwenye nchi zilizokumbwa na machafuko zikiwemo za Libya na Tunisia, alisema nchi hizo zimefika katika hatua hiyo kutokana na kutokuwa na majadiliano kati ya watawala na raia wake.
Alisema kwa miaka ya hivi karibuni nchi nyingi za Afrika zikiwemo zile za Uarabuni zimekumbwa na matukio ya uvunjifu wa amani, hivyo hali hiyo inaweza pia kutokea katika nchi nyingine za Afrika kama hakutafikiwa kwa hatua hiyo.
Kukosekana kwa majadiliano kati ya raia na watawala hawa kunaweza kuzaa malumbano na kutoweka kwa amani, aliongeza. Jenerali Mbita ambaye pia ni Balozi mstaafu na Mdhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, alisema lengo la AZAKI ni kufaya kazi kwa pamoja na serikali katika kutekeleza mipango mbalimbali na kuleta maendeleo ya nchi.
Mbita alitoa onyo hilo jana jijini Dar es Salaam katika kongomano la uundwaji wa jukwaa la taifa la Asasi za Kiraia (AZAKI) la kitaifa na la kikanda.
Alisema tatizo kubwa lililopo katika serikali na utawala wa nchi nyingi za ukanda wa Afrika ikiwemo Tanzania ni kutokuwa na majadiliano ya pamoja kati yao na wananchi.
Shida kubwa iliyopo ni kukosa majadiliano ya pamoja kati ya watawala na raia, amani na utulivu inaweza kutoweka kwenye ukanda wa nchi za Afrika endapo majadiliano hayo hayatakuwepo, alisema Jenerali Mbita.
Akitolea mfano kwenye nchi zilizokumbwa na machafuko zikiwemo za Libya na Tunisia, alisema nchi hizo zimefika katika hatua hiyo kutokana na kutokuwa na majadiliano kati ya watawala na raia wake.
Alisema kwa miaka ya hivi karibuni nchi nyingi za Afrika zikiwemo zile za Uarabuni zimekumbwa na matukio ya uvunjifu wa amani, hivyo hali hiyo inaweza pia kutokea katika nchi nyingine za Afrika kama hakutafikiwa kwa hatua hiyo.
Kukosekana kwa majadiliano kati ya raia na watawala hawa kunaweza kuzaa malumbano na kutoweka kwa amani, aliongeza. Jenerali Mbita ambaye pia ni Balozi mstaafu na Mdhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, alisema lengo la AZAKI ni kufaya kazi kwa pamoja na serikali katika kutekeleza mipango mbalimbali na kuleta maendeleo ya nchi.