kifulambutez
New Member
- Dec 23, 2011
- 1
- 0
Nimeulizwa na Mwanangu siku ya Boxing Day ina maana gani nikamweleza ni siku ya kufungua zawadi. Akaniuliza tena mbona hapa naona kuna kadi nyingi za Christmas lakini mabox ya zawadi siyaoni... nikaanza kujiuma unajua sio utamaduni wetu tumerithi kutoka kwa wenzetu..na mambo kama hayo...leo wakati napitia magazeti nikakuta Kipanya kakata Boxing Day na kuandika Hang-over day...ebu nisaidieni majibu niliyompa mwanangu yanatosheleza au nilimdanganya..!!!?