Bodi ya Utalii yaanza rasmi kumtangaza Babu!

Ehud

JF-Expert Member
Feb 12, 2008
2,685
337
Hayawi hayawiiii....sasa yamekua...ktk hali ambayo haikutegemewa na wengi...bodi ya Utalii Tanzania(TTB), imeanza kuitangaza tiba inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Kijiji cha Sumange, wilayani Loliondo.

Kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano wa bodi hiyo, Geofrey Tengeneza, alisema wameanza kutengeneza picha na taarifa kuhusu tiba inayotolewa na babu huyo na kuzitangaza.

Alisema taarifa hizo zimeanza kusambazwa katika mitandao mbalimbali, ili kuueleza ulimwengu, aina mpya ya utalii inayopatikana nchini.Alisema tiba inayotolewa na Mchungaji Mwasapile ni aina mpya ya utalii, inayopatikana hapa nchini na kwamba mataifa mengine hayana aina hiyo ya utalii.

"Sisi kama bodi tumeliona hilo na tumeanza kulifanyia kazi kwa sababu medical tourism ni aina ya utalii ambayo ni mpya hapa kwetu,"alisema.

Ofisa huyo alisema kazi yao ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini na kwamba kazi hiyo imeanza kuzaa matunda baada ya kujitokeza kwa watu kutoka mataifa mbalimbali.

Tangu Mchungaji Mwasapile aanze kutoa tiba hiyo, mamia ya watu kutoka ndani na nje ya nchi, wamekuwa wakifurika katika Kijiji cha Samunge, kupata tiba hiyo.


Bodi ya Utalii yaanza rasmi kumtangaza Babu!
 
Asee yaani kwa hiyo watu wa mataifa mengine wanatakiwa kuja kutalii au kutibiwa?
 
Asee yaani kwa hiyo watu wa mataifa mengine wanatakiwa kuja kutalii au kutibiwa?

wanakuja kutalii!wanakuja kuona jinsi mwanadamu aliyedumaa(mentally retarded humanbeing)anavyotumia njia za kizamani za kutibu magonjwa katika karne ya 21.ni utalii haswa....!kumbuka mwanadamu wa kale zaidi aliaminika kuishi tanzania,yawezeka kabisa tanzania bado ina watu wa kale(kama zinjanthropus)
hongera sana bodi ya utalii.keep it up!
 
kweli Mungu anaipenda Tanzania, nchi ya kipekee duniani pamoja na sayari zingine zote zenye viumbe. Mungu endelea kuibariki Tz, Mungu mbariki na JK maana haya yanatokea katika regime yake!!!!!!!!!!!!!!!
 
Wanashindwa kutangaza Mt. Kilimanjaro na mbuga wanamtangaza babu Pumbavu Nchi ya Vilaza:embarassed2:
 
Mmmmmmh,
Sio lazima kusema sana, acha ninyamaze.
Anyway si watatuletea fedha za kigeni,
Walete tu.
 
Hayawi hayawiiii....sasa yamekua...ktk hali ambayo haikutegemewa na wengi...bodi ya Utalii Tanzania(TTB), imeanza kuitangaza tiba inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Kijiji cha Sumange, wilayani Loliondo.

Kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano wa bodi hiyo, Geofrey Tengeneza, alisema wameanza kutengeneza picha na taarifa kuhusu tiba inayotolewa na babu huyo na kuzitangaza.

Alisema taarifa hizo zimeanza kusambazwa katika mitandao mbalimbali, ili kuueleza ulimwengu, aina mpya ya utalii inayopatikana nchini.Alisema tiba inayotolewa na Mchungaji Mwasapile ni aina mpya ya utalii, inayopatikana hapa nchini na kwamba mataifa mengine hayana aina hiyo ya utalii.

"Sisi kama bodi tumeliona hilo na tumeanza kulifanyia kazi kwa sababu medical tourism ni aina ya utalii ambayo ni mpya hapa kwetu,"alisema.

Ofisa huyo alisema kazi yao ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini na kwamba kazi hiyo imeanza kuzaa matunda baada ya kujitokeza kwa watu kutoka mataifa mbalimbali.

Tangu Mchungaji Mwasapile aanze kutoa tiba hiyo, mamia ya watu kutoka ndani na nje ya nchi, wamekuwa wakifurika katika Kijiji cha Samunge, kupata tiba hiyo.


Bodi ya Utalii yaanza rasmi kumtangaza Babu!

Sasa nani atatoa patent ya hiyo dawa? Ingekuwa kwa nchi za wenzetu wangeifanyia kazi na kuhakikisha inaliingizia taifa mpunga.
 
Mkuu hata kama watakuja kutibiwa
Hawa watu watakaa katika mahotel yetu
Watatumia migahawa yetu ya aina mbalimbali
Tanzania itajulikana sana
Na pesa za kigeni zitaingia bac hapo sekta ya utalii inajipatia kipato na inakua,
Twende kazi!
 
kweli Mungu anaipenda Tanzania, nchi ya kipekee duniani pamoja na sayari zingine zote zenye viumbe. Mungu endelea kuibariki Tz, Mungu mbariki na JK maana haya yanatokea katika regime yake!!!!!!!!!!!!!!!

nafikiri unamaanisha ulichoandika
 
Sasa nani atatoa patent ya hiyo dawa? Ingekuwa kwa nchi za wenzetu wangeifanyia kazi na kuhakikisha inaliingizia taifa mpunga.

si ndio kama hivyo watalii walika wataspend and other accomodation watajilipia .....ndio mpunga wenyewe huo kaka
 
Back
Top Bottom