Bizari kiungo cha mboga chenye faida nyingi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,322
33,126
Inawezekana katika maisha yako hujawahi kula mboga iliyowekwa kiungo kinachoitwa bizari, kama umewahi, inawezekana pia hujawahi kujua faida zake mwilini.

Bizari (Turmeric) ni kiungo cha mboga jamii ya mimea unaochimbwa kama mizizi, mfano wa tangawizi, lakini tangawizi yenyewe ina rangi ya njano na hujulikana pia kama ‘manjano’ kutokana na rangi yake.

Kiungo hiki kinatumiwa sana katika Bara la Asia na hasa India na China. Kutokana na umuhimu wake kiafya, vyakula vingi hupikwa kwa kuchanganya na kiungo hiki ambacho sasa kimeenea dunia nzima, ikiwemo Tanzania.

FAIDA ZA BIZARI KIAFYA
Bizari hutumika na watu wengi kama kiungo cha mboga cha kuongeza ladha katika mchuzi na pengine kuweka rangi, lakini kuna faida nyingi unazozipata unapotumia kiungo hiki kila mara katika mapishi yako.

Inaelezwa kuwa bizari ina virutubisho vyenye uwezo wa kuimarisha kinga ya mwili, mara 8 zaidi ya Vitamin C na Vitamin E, ina uwezo wa kushusha kiwango cha lehemu (cholesterol) na kuzuia mtu kuzeeka kabla ya wakati.
Aidha, bizari huimarisha sehemu za magoti hivyo kukuepusha na matatizo ya miguu kuuma. Bizari pia hun’garisha ngozi na kuifanya kuwa yenye afya na huimarisha pia mfumo wa usagaji chakula (Digestion).

SUALA LA UBORA NI MUHIMU
Katika ulimwengu wa maendeleo ya sayansi na teknolijia tulionao sasa, bizari hutengenezwa viwandani na kuhifadhiwa kwa usafirishaji sehemu mbalimbali duniani na kwa ajili ya matumizi ya muda mrefu. Katika hali kama hiyo, si ajabu kukuta bizari iliyoongezewa kemikali zingine za kuhifahdia chakula.

Bizari ya aina hiyo, tayari inakosa faida zilizoelezwa hapo juu, hivyo ni suala muhimu kuangalia ubora wa bizari unayoitumia na mahali inapotoka. Katika nchi yetu, Mungu ametujaalia ardhi yenye rutuba ambapo kiungo kama hiki kinalimwa na kupatikana kwa wingi na kwa uhalisia wake.

Katika suala la kujali ubora, pendelea zaidi kununua bizari kutoka sokoni ambayo imetengenezwa katika mazingira safi na salama na bila kuchanganywa na kitu kingine. Iwapo pia utanunua bizari iliyokwisha hifadhiwa, ni vyema ukasoma maelezo yake kuona kama haina vikorombwezo (additives) vingine.

Ni ukweli ulio wazi kuwa ukitumia bizari iliyobora utapa faida nyingi kiafya, hivyo hakikisha katika upikaji wako wa kitoweo cha nyama, kama vile kuku, samaki, ngo’mbe unaweka bizari. Upikaji mzuri ni ule wa kuweka kiungo hicho mwisho baada ya mboga yako kuchemka na kuiva, kwani haitakiwi bizari kuchemka sana.

turmericdryleaf.jpg


Kwa ujumla hizi ndizo faida utakazozipata ukiifanya bizari kuwa sehemu ya viungo katika mlo wako wa kila siku:
UTAIMARISHA KINGA YA MWILI WAKO

UTAIMARISHA AFYA YA MACHO

UTAIMARISHA SEHEMU ZA VIUNGIO VYA MWILI WAKO

UTAIMARISHA UTENDAJI KAZI WA INI

UTAIMARISHA CHEMBE HAI ZA MWILI

UTAIMARISHA MFUMO WA USAGAJI CHAKULA

UTAIMARISHA MFUMO WA DAMU MWILINI

UTASHUSHA KIWANGO CHA KOLESTRO MWILINI

UTAIMARISHA MFUMO WA UZALISHAJI MBEGU ZA UZAZI

UTAIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI MWILINI.
 
hizi bizari sikuiz sindo zinauzwa kwenye makopo mfano onga mchuzi mix, chicken masala na royco?nakumbuka enzi hzo,zilikuwa zinauzwa magengeni kwa kupimwa,unamwambia muuzaji nipimie ya kiasi kadhaa.
 
asante sana mzizi kwa kunikumbusha, i previously used this, will resume.

mee too na hasa kwa ajili ya

UTASHUSHA KIWANGO CHA KOLESTRO MWILINI

UTAIMARISHA MFUMO WA UZALISHAJI MBEGU ZA UZAZI

UTAIMARISHA KIWANGO CHA SUKARI MWILINI.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom