wataalamu hebu nifafanulieni hapa
binamu ndio nani kwa kiingereza?
na cousin kwa kiswahili?
na niece kwa kiswahili?
nephew kwa kiswahili????????
asanteni.....
binamu ndio nani kwa kiingereza? = cousin
na cousin kwa kiswahili? = binamu
na niece kwa kiswahili? = mpwa
nephew kwa kiswahili???????? = mpwa
Kiswahili ni maneno machache sana yenye gender na hata kiingereza kina limits za gender, kiarabu hakina shaka ndani. Usihamanike.
faiza asante
hebu niambie tofauti ya binamu na mpwa......
halafu hapo kwenye niece na nephew.....which is which....??????/
faiza asante
hebu niambie tofauti ya binamu na mpwa......
halafu hapo kwenye niece na nephew.....which is which....??????/
ok na mpwa yupi ni niece
na yupi ni nephew....
usichoke faiza...itwasaidia wengi....
Binamu ni watoto kwa watoto (peers). Kama mimi na wewe tuwe watoto wa mtu (kaka) na dada yake ndiyo tutakuwa mabinamu (cousins).
Kama wewe ni mtoto wa dada yake na baba yangu basi utakuwa mpwa wa baba. Kwa hiyo mpwa ni kwa mjomba na shangazi.
Nephew ni mpwa wa kiume na niece mpwa wa kike.
sasa 'cousin' hapo ndo naona kama
umetofautiana na ff au ni maana hiyo hiyo?
Wala hatujatofautiana. Cousins ni binamuz. Lakini hao hao binamuz kwa jinsia zao wataitwa tofauti na wazazi. Wa kike ataitwa niece na wa kiume ataitwa nephew.
Nyani kidogo kuna marekebisho.
Cousins sawa ni "binamus" lakini niece na nephew ni wapwa. Yaani ni watoto wa ndugu zako.
Tuko pamoja. Mama au baba, mjomba au shangazi, ndiyo watawaita hao watoto nephew na niece kulingana na jinsia zao. Watoto kwa watoto hawawezi kuitana nephew na niece. Wao kwa wao wataitana cousins (binamuz). Si ndiyo?
kwa ufupi nieces na nephews ni watoto wa cousins....
na cousins ya kizungu ni mtoto wa baba yako mdogo,mkubwa,mjomba,shangazi na kadhalika....sawa???????
Ngoja nikupe huu mfano ambao nadhani ni rahisi kuuelewa. Chukulia mimi na wewe ni ndugu. Baba mmoja na mama mmoja. Pia tuna dada yetu. Kwa hiyo tumezaliwa watatu.
Mimi ni mkubwa kwako. Wewe unanifuatia na dada yetu ndiyo kitinda mimba. Kwa hiyo mimi na wewe ni mtu na kaka yake/ mtu na mdogo wake. Mimi ni kaka mkubwa, wewe unafuatia na dada yetu (mdogo wetu) ndiyo wa mwisho kuzaliwa.
Mimi nimeoa na nina watoto wawili. Mmoja ni wa kiume na mmoja ni wa kike. Na wewe umeoa na una watoto wawili pia. Watoto wako wote ni wa kike. Dada yetu (mdogo wetu) yeye bado hajaolewa ila ana mtoto mmoja wa kike.
Hao watoto wangu wewe utakuwa baba yao mdogo (kwa Kiingereza uncle). Mdogo wetu wa mwisho atakuwa shangazi yao (au auntie kwa Kiingereza). Mwanangu wa kiume kwako atakuwa mwanao lakini kwa Kiingereza atakuwa nephew. Mwanangu wa kike atakuwa niece.
Vivyo hivyo, mwanangu wa kiume atakuwa nephew (mpwa) kwa shangazi yake (ambaye ni mdogo wetu wa mwisho). Na yule wa kike atakuwa niece (mpwa wa kike).
Watoto wako mimi nitakuwa baba yao mkubwa. Lakini kwa Kiingereza hakuna baba mkubwa. Baba mkubwa au mdogo wote ni uncles. Kwa hiyo mimi nitakuwa uncle wao hao mabinti zako wawili. Nitawaita nieces.
Shangazi yao (kitinda mimba wetu) atawaita hao mabinti zako nieces pia. Sasa huyu kitinda mimba wetu si naye ana mtoto kike - basi huyo binti yake sisi atatuita wajomba na sisi tutamuita yeye niece.
Watoto wangu mimi, watoto wako wewe, na mtoto wa huyo dada yetu mdogo wao kwa wao ndiyo mabinamu (cousins).
I know it's kinda convoluted but I hope you'll understand. If not let me know.
asante nilikuwa naelewa hivyo
nahisi umejibu swali langu kuwa mjomba na shangazi ya kiswahili siyo sawa na uncle na aunt....
nafikiri nimeelewa....
Uko sawa. Kwa Kiingereza baba wakubwa, baba wadogo, mama wakubwa, mama wadogo, wajomba, na shangazi wote ni uncles na aunties. Ili kuleta umahsusi zaidi huwaga wana qualify kwa kusema 'on my mother's side' au 'on my father's side'. Kwa mfano, 'my uncle on my father's side' au 'paternal uncle/ aunt' au 'maternal uncle/aunt'.
ok thanx
labda nikuulize kwa kiingereza 'mkaza wa mjomba' lol
halafu kama unajua kwa kiingereza mjukuu,kitukuu.kilembwe...lol
kwa ufupi nieces na nephews ni watoto wa cousins....
na cousins ya kizungu ni mtoto wa baba yako mdogo,mkubwa,mjomba,shangazi na kadhalika....sawa???????
Tuko pamoja. Mama au baba, mjomba au shangazi, ndiyo watawaita hao watoto nephew na niece kulingana na jinsia zao. Watoto kwa watoto hawawezi kuitana nephew na niece. Wao kwa wao wataitana cousins (binamuz). Si ndiyo?