Binadamu anaweza kutibu ugonjwa wa kuzeeka?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,226
12,733
Leo hii duniani hakuna ugonjwa unaoua watu wengi kama kuzeeka. Zaidi ya asilimi 60 ya watu wanaokufa leo hii wanakufa sababu ya uzee.

Ugonjwa wa kuzeeka unatokea pale seli za mwili zinapoacha kugawanyika na kutengeneza seli mpya. Inadaiwa kuwa kwa wastani seli ya binadamu inaweza kugawanyika mara 50 tu katika maisha yake yote. Baada ya hapo mwili unaanza kuzeeka sababu hauundi seli mpya.

Kuna viumbe havikabiliwi kabisa na ugonjwa huu. Viumbe kama bakteria na miti havisumbuliwi na ugonjwa wa kuzeeka.

Binadamu anaweza kutibu ugonjwa huu wa kuzeeka. Mfano anaweza kubadili genetic yake na kufanya seli zake zisiache kuunda seli mpya? Anaweza kujipandikiza genes za wanyama kama kobe ili kuchelewesha ugonjwa huu wa kuzeeka? Kuna namna binadamu anaweza kufanya kukabiliana na ugonjwa wa kuzeeka?
FB_IMG_1703870378799.jpg
 
Kula vizuri, fanya mazoezi hasa kutembea na mazoezi ya viungo, fanya ngono na mabinti wadogo, usinywe pombe sana wala usivute sigara hovyo.

Zaidi ya yote jichanganye zaidi na watu umewazidi miaka 10 - 15. Aisee watu waliokuzunguka wana uwezo wa kukuzeesha.

Itakusaidia kuchelewa kuporomoka mwili sababu ya umri mkubwa.
 
Kuzeeka sio Ugonjwa... Kuzeeka kunapelekea mwili kushindwa kuimili magonjwa... Juwa kutofautisha kuzeeka na kupata magonjwa.
Kuna viumbe havikabiliwi kabisa na ugonjwa huu. Viumbe kama bakteria na miti havisumbuliwi na ugonjwa wa kuzeeka.
Hapa duniani hakuna kiumbe hai, narudia tena kiumbe hai kinachoweza kuishi milele.

Viumbe vyote hai vimekuwa programmed kufa. Seli zetu zote mwilini zimekuwa programmed kuishi kwa muda fulani baada ya hapo kwa sababu zinakuwa zimepunguza uwezo wa kutenda kazi kwa ufanisi. Na njia moja wapo ta kugundua seli za mwili wako zimeanza kufa, ni kuanza kuona mvi. Mvi ni taarifa ya kwamba seli ambazo zinatakiwa kuipa nywele rangi zimeanza kushindwa kufanya kazi au zimeanza kufa.

Sasa seli za mwili uwa zinaanza kufa kwa sababu ziko programmed kuishi kwa kipindi fulani tu, sasa umri unavyozidi kwenda ndipo seli zako nyingi uanza kufikia ukomo wa kujitengeneza kwa sababu zimekuwa programmed kuwa hivyo. Sasa zile ambazo zimetengenezwa zikaanza kufa zinakosa seli mbadala kwa sababu kiwanda cha kutengenezea seli nacho wafanyakazi wake nao wameanza kuzeeka na kufa. Hapo ndipo magonjwa yanaanza kukunyemelea uzeeni kwa sababu mwili umeanza kukosa wanajeshi wa kutosha kupambana na magonjwa... Ndio maana wazee wengi inakuwa rahisi kuumwa. Au muda mwingine viungo kama moyo, figo na viungo vingine ukosa nguvu kwa sababu seli hazina uwezo tena wa kuchapa kazi kutokana na zimeanza kubaki chache.

Kwa sasa bado hakuna teknolojia ya kufanya seli zisizeeke, sijasemq kufa, nimesema kuzeeka, kwa sababu kufa kuko palepale... Sana sana sayansi itazifanya seli ziweze kuishi muda mrefu tu na kumpeleka binadamu kuchelewa kuzeeka, lakini bado zitazeeka tu na kufa. Lakini Teknolojia ya robots inaweza kufanya mageuzi na akili za binaadam na ufahamu ukaamishiwa kwenye robots. Yani tukawa Cyborg.
 
Kuzeeka sio Ugonjwa... Kuzeeka kunapelekea mwili kushindwa kuimili magonjwa... Juwa kutofautisha kuzeeka na kupata magonjwa.

Hapa duniani hakuna kiumbe hai, narudia tena kiumbe hai kinachoweza kuishi milele.

Viumbe vyote hai vimekuwa programmed kufa. Seli zetu zote mwilini zimekuwa programmed kuishi kwa muda fulani baada ya hapo kwa sababu zinakuwa zimepunguza uwezo wa kutenda kazi kwa ufanisi. Na njia moja wapo ta kugundua seli za mwili wako zimeanza kufa, ni kuanza kuona mvi. Mvi ni taarifa ya kwamba seli ambazo zinatakiwa kuipa nywele rangi zimeanza kushindwa kufanya kazi au zimeanza kufa.

Sasa seli za mwili uwa zinaanza kufa kwa sababu ziko programmed kuishi kwa kipindi fulani tu, sasa umri unavyozidi kwenda ndipo seli zako nyingi uanza kufikia ukomo wa kujitengeneza kwa sababu zimekuwa programmed kuwa hivyo. Sasa zile ambazo zimetengenezwa zikaanza kufa zinakosa seli mbadala kwa sababu kiwanda cha kutengenezea seli nacho wafanyakazi wake nao wameanza kuzeeka na kufa. Hapo ndipo magonjwa yanaanza kukunyemelea uzeeni kwa sababu mwili umeanza kukosa wanajeshi wa kutosha kupambana na magonjwa... Ndio maana wazee wengi inakuwa rahisi kuumwa. Au muda mwingine viungo kama moyo, figo na viungo vingine ukosa nguvu kwa sababu seli hazina uwezo tena wa kuchapa kazi kutokana na zimeanza kubaki chache.

Kwa sasa bado hakuna teknolojia ya kufanya seli zisizeeke, sijasemq kufa, nimesema kuzeeka, kwa sababu kufa kuko palepale... Sana sana sayansi itazifanya seli ziweze kuishi muda mrefu tu na kumpeleka binadamu kuchelewa kuzeeka, lakini bado zitazeeka tu na kufa. Lakini Teknolojia ya robots inaweza kufanya mageuzi na akili za binaadam na ufahamu ukaamishiwa kwenye robots. Yani tukawa Cyborg.
Si viumbe wote seli zao ziko programmed kufa baada ya muda fulani. Mfani mmoja ni Mamba. Mamba huwa hazeeki. Atakufa kwa sababu zingine lakini si uzee. Seli zake hazikomi kuzaliana. Hakunagq mamba mzee. Hapo utaona kuwa kuna viumbe hawaathiriwi na huu ugonjwa wa uzee.

Binadamu awekewe vinasaba vya mamba. Iwe kama chanjo dhidi ya huu ugonjwa mbaya wa kuzeeka.
 
Ukisema kuzeeka ni ugonjwa basi hata kipindi cha utoto ni ugonjwa, Kuzeeka sio ugonjwa ni kipindi km vipindi vingine ktk maisha .
Ni ugonjwa hatari kuliko yote. Maana ndiyo unaongoza kwa kuua watu. Kuzeeka kama magonjwa mengine, kunaharibu utendaji kazi wa mwili. Utoto hauuni wala kuharibu utendaji wa mwili.
 
Kula vizuri, fanya mazoezi hasa kutembea na mazoezi ya viungo, fanya ngono na mabinti wadogo, usinywe pombe sana wala usivute sigara hovyo.

Zaidi ya yote jichanganye zaidi na watu umewazidi miaka 10 - 15. Aisee watu waliokuzunguka wana uwezo wa kukuzeesha.

Itakusaidia kuchelewa kuporomoka mwili sababu ya umri mkubwa.
Aiseeh

Tusioporomoka miili,wote tunazingatia haya?
 
Uwez kuzuia kuzeeka ila yapo mafuta yatakayo kufanya uwe na baby face n ya asili
Kitu kingine kinachochangia ugonjwa wa kuzeeka, hasa kuzeeka ngozi ni kupigwa na jua kali. Na hili watu wenye ngozi nyeupe huathiriwa zaidi kuliko watu wenye ngozi nyeusi. Ndiyo maana wanasema "Black Don't crack." Yaani weusi hawazeeki. Pia kuna mafuta ya kuzuia ukali wa jua, yanasaidia kupunguza makali ya ugonjwa wa kuzeeka. Pengine unazungumzia mafuta ya aina hiyo.
 
Kuna tofauti ya uzee na kuchakaa ukikosa nidham ukaendekeza ulevi na starehe kama huyo Wayne Rooney utachakaa mapema miaka 38 ila utaonekana kama 65 mtoto mdogo ila muonekano wa Sir Alex Ferguson
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom