Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Irine Uwoya agoma kuacha vimini
Irine UwoyaMWANDISHI WETU
IRINE Uwoya amesema hawezi kuacha kuvaa nguo fupi kwavile amezoea kufanya hivyo na hajaanza baada ya kuwa staa wa filamu.
Msanii huyo, ambaye ni miongoni mwa mastaa wanaofanya vizuri kwenye filamu za Tanzania amekwenda mbali zaidi na kusema haoni tatizo lolote la uvaaji wake, ambao baadhi ya watu wamekuwa wakidai hauendani na maadili.
Uwoya, ambaye ameigiza filamu kama 'Hazard', 'One Blood', 'Mid Night', 'Peace of Mind', 'Tanzanite', 'Kalunde' na 'The Dream'.
"Kusema kweli nimezoea kuvaa nguo fupi, ni kitu ambacho nimeanza muda mrefu, nafurahia wala sioni kama kuna athari kwa mtu mwingine,"anasema katika mahojiano maalum na kituo kimoja cha televisheni cha Dar es Salaam wiki hii.
"Ni mavazi yangu ambayo nimevaa kipindi kirefu na wala sifanyi hivyo kwavile ni staa, nimezoea ndio maisha yangu,"anasisitiza msanii huyo ambaye aliwahi kukiri kuwa mumewe Hamad Ndikumana, ambaye ni mwanasoka alimuona kwa mara ya kwanza kwenye filamu ya 'Oprah' ndiyo akaanza kumfuatilia.
Kuhusu dau analolipwa msanii huyo alisema kuwa; "Siwezi kusema kuna dau ambalo ni maalum, au kwamba siwezi kuigiza filamu labda mpaka nipewe milioni kadhaa.
"Haya mambo yanazingatia vitu vingi kwanza unaigiza kama nani nikimaanisha ule uhusika unaouvaa halafu unaigiza filamu ya aina gani na ina maudhui gani.
"Unaweza ukalipwa fedha nyingi ukaigiza filamu moja ikawa mbovu na ikakupoteza kabisa na kukuharibia soko, lakini tayari ulishapewa fedha. Ndio maana nasema fedha si kila kitu ni makubaliano baina ya msanii na maprodyuza husika.
"Lakini nikiigiza kama mhusika mkuu dau linakuwa kubwa na mara nyingi sipendi kuweka fedha mbele naangalia na kazi ninayofanya jamii itakubali vipi na itafaidikaje,"anasisitiza msanii huyo mwenye sura ya mvuto.
Msanii huyo ambaye mumewe anachezea klabu ya Daraja la Kwanza ya A. E. Lemesos ya Cyprus alifunga ndoa mwaka jana kwenye Kanisa la St. Joseph jijini Dar es Salaam na ni mtoto wa kwanza wa familia ya Naima Mrisho na Pacras Uwoya.
Uwoya alizaliwa Desemba 18, 1988 mjini Dodoma, na kuanza elimu ya msingi katika Shule ya Mlimwa na akiwa darasa la tatu alihamia Shule ya Msingi Bunge ya Dar es Salaam alikomalizia elimu yake hiyo na sekondari.
Alisoma Shule ya Greenville ya Kampala, Uganda na mwaka 2006 alitwaa taji la urembo la kitongoji cha Chang?ombe jijini Dar es Salaam na kushiriki Miss Temeke, alikoibuka nafasi ya pili ambayo ilimpa tiketi ya kushiriki Miss Tanzania na kuishia nafasi ya tano.
IRINE Uwoya amesema hawezi kuacha kuvaa nguo fupi kwavile amezoea kufanya hivyo na hajaanza baada ya kuwa staa wa filamu.
Msanii huyo, ambaye ni miongoni mwa mastaa wanaofanya vizuri kwenye filamu za Tanzania amekwenda mbali zaidi na kusema haoni tatizo lolote la uvaaji wake, ambao baadhi ya watu wamekuwa wakidai hauendani na maadili.
Uwoya, ambaye ameigiza filamu kama 'Hazard', 'One Blood', 'Mid Night', 'Peace of Mind', 'Tanzanite', 'Kalunde' na 'The Dream'.
"Kusema kweli nimezoea kuvaa nguo fupi, ni kitu ambacho nimeanza muda mrefu, nafurahia wala sioni kama kuna athari kwa mtu mwingine,"anasema katika mahojiano maalum na kituo kimoja cha televisheni cha Dar es Salaam wiki hii.
"Ni mavazi yangu ambayo nimevaa kipindi kirefu na wala sifanyi hivyo kwavile ni staa, nimezoea ndio maisha yangu,"anasisitiza msanii huyo ambaye aliwahi kukiri kuwa mumewe Hamad Ndikumana, ambaye ni mwanasoka alimuona kwa mara ya kwanza kwenye filamu ya 'Oprah' ndiyo akaanza kumfuatilia.
Kuhusu dau analolipwa msanii huyo alisema kuwa; "Siwezi kusema kuna dau ambalo ni maalum, au kwamba siwezi kuigiza filamu labda mpaka nipewe milioni kadhaa.
"Haya mambo yanazingatia vitu vingi kwanza unaigiza kama nani nikimaanisha ule uhusika unaouvaa halafu unaigiza filamu ya aina gani na ina maudhui gani.
"Unaweza ukalipwa fedha nyingi ukaigiza filamu moja ikawa mbovu na ikakupoteza kabisa na kukuharibia soko, lakini tayari ulishapewa fedha. Ndio maana nasema fedha si kila kitu ni makubaliano baina ya msanii na maprodyuza husika.
"Lakini nikiigiza kama mhusika mkuu dau linakuwa kubwa na mara nyingi sipendi kuweka fedha mbele naangalia na kazi ninayofanya jamii itakubali vipi na itafaidikaje,"anasisitiza msanii huyo mwenye sura ya mvuto.
Msanii huyo ambaye mumewe anachezea klabu ya Daraja la Kwanza ya A. E. Lemesos ya Cyprus alifunga ndoa mwaka jana kwenye Kanisa la St. Joseph jijini Dar es Salaam na ni mtoto wa kwanza wa familia ya Naima Mrisho na Pacras Uwoya.
Uwoya alizaliwa Desemba 18, 1988 mjini Dodoma, na kuanza elimu ya msingi katika Shule ya Mlimwa na akiwa darasa la tatu alihamia Shule ya Msingi Bunge ya Dar es Salaam alikomalizia elimu yake hiyo na sekondari.
Alisoma Shule ya Greenville ya Kampala, Uganda na mwaka 2006 alitwaa taji la urembo la kitongoji cha Chang?ombe jijini Dar es Salaam na kushiriki Miss Temeke, alikoibuka nafasi ya pili ambayo ilimpa tiketi ya kushiriki Miss Tanzania na kuishia nafasi ya tano.