Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi, kuna msemo wa Kiswahili usemao, " kizuri kula na nduguzo", hivyo nimeikuta hii imekaa vizuri, nikaona nilete tule na wana JF.
Kuna maonyesho ya bidhaa mbalimbali yanayoendelea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Hall tangu juzi, na yanatarajiwa kuisha kesho.
Jambo zuri nililolishuhudia kwenye bidhaa hizi za Uturuki ni kiwango cha ubora wa hali ya juu ukilinganisha na bidhaa za kutoka China zilizofurika maduka yetu.
Wale wenye nafasi, sio vibaya ikipita tuu na kujionea, ila nimedokezwa leo bei zimepoozwa karibu na bure na kesho kuna uwezekano baadhi ya bidhaa hizo zikagawiwa bure kabisa.
Dokezo hilo limefuatia Waturuki hao kuja kuonyesha bidhaa nyingi zenye ubora wa hali ya juu kwa viwango cha nchi za Ulaya, kwa matumaini ya kutosheleza kiu la soko la Tanzania kwa upande wa quality products, wamepigwa butaa kukuta Watanzania wameshaleweshwa na bidhaa za China sio kwa sababu ya poor quality, bali kwa sababu ni za bei chee, hivyo Waturuki kujikuta lazima hizo bidhaa zao, nao waziuze kwa bei chee.
Maonyesho hayo, yatamalizika kesho hivyo kupelekea baadhi ya bidhaa kugaiwa bure kutokana na gharama za kuzisafirisha kuzirudisha Uturuki ni kubwa kuliko kuzitelekeza hapa nchini.
Aina ya bidhaa hizo iko kwe attachment.
Asanteni
Kuna maonyesho ya bidhaa mbalimbali yanayoendelea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Hall tangu juzi, na yanatarajiwa kuisha kesho.
Jambo zuri nililolishuhudia kwenye bidhaa hizi za Uturuki ni kiwango cha ubora wa hali ya juu ukilinganisha na bidhaa za kutoka China zilizofurika maduka yetu.
Wale wenye nafasi, sio vibaya ikipita tuu na kujionea, ila nimedokezwa leo bei zimepoozwa karibu na bure na kesho kuna uwezekano baadhi ya bidhaa hizo zikagawiwa bure kabisa.
Dokezo hilo limefuatia Waturuki hao kuja kuonyesha bidhaa nyingi zenye ubora wa hali ya juu kwa viwango cha nchi za Ulaya, kwa matumaini ya kutosheleza kiu la soko la Tanzania kwa upande wa quality products, wamepigwa butaa kukuta Watanzania wameshaleweshwa na bidhaa za China sio kwa sababu ya poor quality, bali kwa sababu ni za bei chee, hivyo Waturuki kujikuta lazima hizo bidhaa zao, nao waziuze kwa bei chee.
Maonyesho hayo, yatamalizika kesho hivyo kupelekea baadhi ya bidhaa kugaiwa bure kutokana na gharama za kuzisafirisha kuzirudisha Uturuki ni kubwa kuliko kuzitelekeza hapa nchini.
Aina ya bidhaa hizo iko kwe attachment.
Asanteni