ephen_
JF-Expert Member
- Oct 28, 2022
- 6,079
- 21,983
Biashara inahitaji moyo kama unabisha muulize mshamba_hachekwi
KongoleKwa ambae hajawai kuwa na biashara hawezi elewa kwanini mtu ana duka kubwa ila mchana kikapu cha msosi kinakuja kutoka home.
kufika hiyo hatua sio rahisi kama unavyodhani, fikiria upya tena kiutu-uzima...Sio rafiki kivipi Mbona baadhi ya wafanyabiashara wanapiga pesa ndefu,kupitia biashara hizohizo?
Biashara matangazo.
Biashara ubunifu ...
Biashara Customer care ..
Biashara biashara biashara
Hata mentality ya viongozi wenyewe si ndio hiyo hiyo ? , mtu kama Mengi alipoomba vibali vya kuanza kuwekeza kwenye mradi wa gesi asilia ,alipewa dongo kwamba ,watanzania wana mitaji ya kuzalisha juice mambo ya gesi hawawezi .Pia hamna jipya mkuu.
Uchumi wa fremu yaani, kila mtu wazo lake ni kukodi fremu auze bidhaa/huduma fulani. Kuna nini?
Yote kwa yote usiombe hali hii ikukute ikiwa uliianzisha kwa kukopa hivyo una marejesho kila mwezi..
Unageuka tena hio hio ndio ya kulisha familia, hio hio kodi ya fremu na Pango..
Lazima upate moto, mteja akija asiponunua unaweza umkunje shati humo humo dukani.
Kaka upo kwenye biashra ganj mnk tumefananMimi ni graduate nilipata kazi nikafanya kwa muda wa miaka kama saba hivi kupata mtaji then nikaamua kuanzisha biashara,unajua biashara kuanzisha si kazi ukiwa na mtaji,kazi ngumu kwenye biashara ni kuifanya iendelee kuwepo.
Sasa wakati biashara inaanza mara nyingi inaanza vizuri but ukifika muda unakuta mambo hayaendi kabisa number ya wateja wako basic unakuta ghafla hawapo na hakuna wateja wapya wanaoingia dukani kwako aisee hii kitu usiombe unafanya kila kitu unachoweza kufanya kwa usahihi alafu matokeo hupati apa ndio nikajua kwa nini watu wanaenda kwa waganga.
Mashekhe au kwa wachungaji ili kuweza kupata msaada, kuna kipindi biashara inakua ngumu mpaka unaona bora urudi kwenye mshahara wa laki tano kwa mwezi big up sana kwa wafanya biashara walioweza kukuza mitaji hii kitu siyo rahisi mazee
Uko sahih sanaNa kitu kingine watu wengi biashara tunaanzisha Kwa mawazo yetu kichwani sasa na hii mitaji midogo downfall zikitokea biashara inakua kwenye risk ya kufilisika lakini ukiwa na familia ya watu wafanya biashara ni ngumu kupitia kwenye mashimo sababu waliotangulia washajua michoro yote ya biashara na kuipata faida
Hao Ni wakingaNdo maana wafanyabiashara welio wengi, chakula kinaletwa Toka nyumbani!Ili asiharibu droo ya hela kwa kununua hotelini
Mpe ukweliTulia wewe ,hujui kitu
We unaona hizo biashara zimesimama unadhani hizo biashara ndio zinagenerate faida si ndio ?
Watu wanafanya mambo yao meusi pembeni hizo biashara ni changa la macho tu
Watu wanafanya utakatishaji pesa , ukwepaji kodi , Rushwa , kuuza bidhaa feki , kupunja na kufanya Magumashi kibao
Mfumo wa nchi hii ni wa ovyo mno
Hairuhusu private sector na ujasiriamali kuthrive ,kama unaona hizi ni stories anzisha biashara halafu ulete mrejesho hapa
Ni kweli mkuu yaani hata ukipata mtaji kila unachofikiria kufanya unaona hapo mtaani kipo.Pia hamna jipya mkuu.
Uchumi wa fremu yaani, kila mtu wazo lake ni kukodi fremu auze bidhaa/huduma fulani. Kuna nini?
Kwa sababu hawana uwezo wa kufungua viwanda. Ndio maana wengi tunafanya uchuuzi .Pia hamna jipya mkuu.
Uchumi wa fremu yaani, kila mtu wazo lake ni kukodi fremu auze bidhaa/huduma fulani. Kuna nini?
Mimi mmachinga hapa Posta Dsm naishuhudia sana hii hali, maana karibia wote tunaffanana . Wote tunachuuza miwani, tai, mikanda, wallet ,chaja za simu na notebooks na peni. Yaani mtu akiwa na mteja full kutoleana macho, sometimes mpaka kushikana masharti.Matokeo yake ndio hayo sasa ,kuwa na taifa la wachuuzi badala ya uchumi ambao uko diversified
Unakuta clothing stores kumi sehemu moja , unategemea nini hapo ,ni mwendo wa kurogana tu na kupigana fitna + low purchasing power ya raia WA bongo
Hao wamejua ku "game the system"Sio rafiki kivipi Mbona baadhi ya wafanyabiashara wanapiga pesa ndefu,kupitia biashara hizohizo?
Mchina na bidhaa zake kaharibu chumi za nchi nyingi sana za Africa.Matokeo yake ndio hayo sasa ,kuwa na taifa la wachuuzi badala ya uchumi ambao uko diversified
Unakuta clothing stores kumi sehemu moja , unategemea nini hapo ,ni mwendo wa kurogana tu na kupigana fitna + low purchasing power ya raia WA bongo
Hapo bado watu wa tozo chungu zima na wengine wa mchango wa mwenge wanakusubiria.Wewe si unaleta nadharia zako za kwenye vitabu ,but ushawahi kufanya kila kitu Kwa usahihi na usione matunda,mimi kuna kipindi nilihisi kwenye biashara yangu labda watu wanaona giza tuu unafunga ofisi saa mbili asubuhi na kufunga saa tano hakuna prospect wala mteja aliyeingia dukani