Benki ya CRDB yapunguza viwango vya riba ya mikopo na kuongeza muda wa marejesho kwa watumishi

Kwani ni lazima iwe miaka 7? Itakuaje endapo mtu achague yeye mwenyewe kwa miaka 2?
 
Kuna jambo huwa silielewi kuhusu hizi taasisi zinazotoa mikopo kwa wafanyakazi! Hivi wafanyakazi wa makampuni binafsi hawaruhusiwi kukopa?maana kila taasisi inatoa mikopo kwa watumishi wa umma/serikali tu!
 
Hongera JPM watakuelewa tu.
Bank zilikuwa zinatumia fedha ya Serikali kuikopesha Serikali
Mkuu! Hivi nikikukopa fedha ili nifungue biashara siku ukija kuhitaji huduma kwenye hiyo biashara yangu(ambayo mtaji nilikopa kwako) napaswa kukuhudumia bure?au ni wewe ndiye unayepaswa kufuata vigezo na masharti ya biashara yangu?
 
Hiyo riba ya 17% ni kwa mwaka au nusu mwaka?..... hapo kwenye hizo %ndio watu wanapokuja kujutia...calculation za riba kama unalipa kwa mwaka ni tofauti na miaka 2,3,4...sikwambii hiyo miaka 7.
 
Kuchukua mkopo wa muda mrefu ni sawa na kujitia kitanzi. Ukitaka kuona manufaa ya mkopo kama kipato ni kikubwa usichukue mkopo unaozidi miaka miwili
 
HAKUNA KILICHOPUNGUZWA HAPO... NI UHUNI TU.. MIAKA IMEONGEZWA 7 TOKA 6.. NA RIBA WAMEPUNGUZA TO 17% KITU NI KILE KILE.. FANYA MATHS UTAONA AT THE END UNALIPA KILE KILE AU ZAIDI. Riba bado kubwa mno mnoooo... mnoooooo... 17% kwa 7 yrs..? Banks zingeweza toa kwa 11% na kupata faida kubwa kwa sbb:

1: watapata wateja wengi sana wakishusha riba to 11%

2: kama BOT wamewashushia banks riba hadi 8% na banks binafsi ikamkopesha mwananchi kwa 11% ana faida ya 3%... Hiyo 3% ni kubwa sana sanaaaa sbb wakishusha to 11% watapata wateja wengi sana na faida yao ya 3% itakuwa kubwaa ..

17% bado kubwa mnoo mnoooooo... Hakuna kitu hapo
 
HAKUNA KILICHOPUNGUZWA HAPO... NI UHUNI TU.. MIAKA IMEONGEZWA 8 TOKA 7.. NA RIBA WAMEPUNGUZA TO 17% KITU NI KILE KILE.. FANYA MATHS UTAONA AT THE END UNALIPA KILE KKILE AU ZAIDI. Riba bado kubwa mno mnoooo... mnoooooo... 17% kwa 8 yrs..? Banks zingeweza toa kwa 11% na kupata faida kubwa sbb 1: watapata wateja wengi sana 2: kama BOT wamewashushia banks riba hadi 8% na banks binafsi ikamkopesha mwananchi kwa 11% ana faida ya 3%... Hiyo 3% ni kubwa sana sanaaaa sbb wakishusha to 11% watapata wateja wengi sana na faida yao ya 3% itakuwa kubwaa ..

17% bado kubwa mnoo mnoooooo... Hakuna kitu hapo
Mkuu unajua operational cost za hizi benki ?
 
Safiiii JPM.

Vipi wale waliokwisha kopa na hawajamaliza kulipa hili punguzo linawahusu au ndo waendelee kulia ?
 
pic+crdb.jpg



Kwa ufupi
  • Watumishi wa umma ambao awali walikuwa wanafanya marejesho mpaka miaka sita ambayo ni sawa na miezi 72, sasa wanaruhusiwa kufanya hivyo mpaka miezi 84.
By Mwandishi Wetu, Mwananchi mwananchipapers@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Benki ya CRDB imeongeza muda wa marejesho kutoka miezi 60 hadi 84 huku ikishusha riba kwa asilimia nne kwa wateja wake, hasa wafanyakazi.

Benki hiyo imeshusha riba kutoka asilimia 21 mpaka 17 huku muda wa marejesho ukitofautiana kati ya wafanyakazi wa sekta binafsi na watumishi wa umma.

Wateja wa benki hiyo wameanza kunufaika na punguzo hilo tangu wiki iliyopita pindi menejimenti iliporidhia kufanya mabadiliko hayo.

Akizungumza na Mcl Digital leo Mei 13, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk Charles Kimei amesema mabadiliko hayo yanalenga kumpa mteja unafuu wa kukamilisha malengo yake kwa wakati.

“Punguzo hili linatolewa kwenye matawi yetu yote. Tangu wiki iliyopita huduma hiyo imeanza kupatikana,” amesema Dk Kimei.

Watumishi wa umma ambao awali walikuwa wanafanya marejesho mpaka miaka sita ambayo ni sawa na miezi 72, sasa wanaruhusiwa kufanya hivyo mpaka miezi 84 au miaka saba wakati wafanyakazi wa sekta binafsi waliokuwa na miaka mitano wameongezewa mpaka miaka sita.

Hatua ya CRDB imekuja baada ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kushusha riba ya mikopo inayotoa kwa benki za biashara mara mbili mfululizo.

Machi mwaka jana, ilipunguza riba hiyo kwa asilimia nne kutoka asilimia 16 mpaka 12.

Mwaka mmoja baadaye, BOT ilipunguza tena kwa asilimia moja na kushusha kiwango cha akiba ambacho benki hizo zinatunza kwake kutoka asilimia 10 mpaka nane ili kuzipa uwezo zaidi wa kuikopesha sekta binafsi.

Je na limit ya kukopa kwa mtumishi wa umma inabakia 50 mil au wameongeza?
 
Back
Top Bottom