Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Ili sinema ikamilike, hata kama ni part I lazima iwe na mwanzo wake na mwisho wake. Ikiendelea part II inakuwa ni season nyingine. Ni muvi za kitapeli kutoka Nigeria ndio huwa zinakatishwa katikati kwa kisingizio cha kumalizia katika part II. Sasa mheshimiwa Membe anaponyanyua bango na kushindwa kuwaweka hadharani anakuwa kama star wa muvi ya Nigeria. Kama hakuona ulazima wa kuwataja basi asingedokeza kwa sababu anatuachia sisi kazi ya ku-guess wakati majibu anayo. Kwa kusaidia kuimalizia hii muvi, adui mmoja ni Mudhihir ambaye hata ajali yake ilisemwa ni Membe alijaribu kumlimboka kwa teknolojia za jadi. Hii muvi kuimalizia mwenyewe ni ngumu, karibuni muongeze vipande ili tumalize kiu yetu