Belarus inaelekea kuwa kama Venezuela na baada ya hapo ni Tanzania?

S V Surovikin

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
13,653
32,890
Rais wa Belarus Alexander Lukashenko amesema kwamba wanapaswa kuandaa jeshi kwa ajili ya vita kwa sababu ya hatari zilizoelekezwa kwa nchi yake kutoka Magharibi,

"Lazima tufunge mipaka na Magharibi, haswa Poland na Lithuania." alisema.

Katika hotuba yake kwenye Mkutano wa Wanawake uliofanyika Minsk-Arena, Aleksandr Lukashenko amefanya tathmini juu ya maandamano dhidi ya uchaguzi wa Rais na shinikizo dhidi yao kutoka nchi jirani.

Akielezea kwamba baada ya uchaguzi, waandamanaji na uungwaji mkono wa kigeni walitumia kila aina ya mbinu ili kuleta machafuko nchini, lakini hawakufanikiwa, Lukashenko amesisitiza kuwa sasa shinikizo la kiuchumi na kidiplomasia kutoka nje limeanza.

Akikumbushia kwamba nchi jirani hazitambui matokeo ya uchaguzi nchini Belarus, Lukashenko amebainisha kuwa kilichofanywa Venezuela kinafanywa nchini mwake.

Lukashenko amedai kuwa uingiliaji wa nje dhidi ya Belarus unakuja kutoka Poland, Lithuania na Ukraine.

Lukashenko, ambaye pia amekosoa uamuzi uliochukuliwa na Bunge la Ulaya kwa kutotambua matokeo ya uchaguzi wa Rais nchini Belarus, amesema,

"Tulifanya uchaguzi katika nchi yetu kulingana na Katiba na Sheria. Hatuhitaji wewe kutambua uchaguzi. Uchaguzi ulifanywa kisheria."

Akisisitiza kuwa wale wanaoiingilia Belarus kutoka nje hawajui nini kinaweza kufanyika katika kipindi kijacho, Lukashenko ameendelea kwa kusema:

"Kabla hatujaanzisha vita, tunajua kwamba wana mbinu chache sana zilizobaki. Kwa hivyo tunapaswa kuandaa nusu ya jeshi kuwa tayari kwa vita. Tunapaswa kufunga mipaka na Magharibi, haswa Poland na Lithuania. Kwa huzuni kubwa, lazima tuimarishe usalama wa mipaka na ndugu zetu wa Ukraine. inatubidi. "

Akisisitiza kuwa anapinga vita , Lukashenko, amenukuliwa,

"Tunakaribia janga baya sana. Ikiwa wao (Ulaya) watakuja hapa itabidi tuwajibu. Hatutapiga magoti hata tukibaki peke yetu."

Baada ya Rais wa sasa Aleksandr Lukashenko kushinda uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 9 Agosti huko Belarus, maandamano yalianza na madai kwamba uchaguzi ulichakachuliwa.

5f2938f24ff9c.jpg
 
Marekani na washirika wake wa NATO wanachotaka ni kwamba nchi zote zilizokuwa ndani ya iliyokuwa Soviet Union zinapokonywa kutoka kwenye siasa zenye ushawishi wa Russia, na kuzifanya zifuate ushawishi wa kimagharibi. Dhumuni kubwa ni kuzifanya hizo zote ziwe mahasimu wa Russia kijeshi na kiuchumi kwa msaada wa NATO. Mwisho wa siku hizo nchi zitageuzwa kuwa military base za NATO kwa ajili ya kuidhibiti Russia kijeshi na kiuchumi.
 
Rais wa Belarus Alexander Lukashenko amesema kwamba wanapaswa kuandaa jeshi kwa ajili ya vita kwa sababu ya hatari zilizoelekezwa kwa nchi yake kutoka Magharibi,

"Lazima tufunge mipaka na Magharibi, haswa Poland na Lithuania." alisema.

Katika hotuba yake kwenye Mkutano wa Wanawake uliofanyika Minsk-Arena, Aleksandr Lukashenko amefanya tathmini juu ya maandamano dhidi ya uchaguzi wa Rais na shinikizo dhidi yao kutoka nchi jirani.

Akielezea kwamba baada ya uchaguzi, waandamanaji na uungwaji mkono wa kigeni walitumia kila aina ya mbinu ili kuleta machafuko nchini, lakini hawakufanikiwa, Lukashenko amesisitiza kuwa sasa shinikizo la kiuchumi na kidiplomasia kutoka nje limeanza.

Akikumbushia kwamba nchi jirani hazitambui matokeo ya uchaguzi nchini Belarus, Lukashenko amebainisha kuwa kilichofanywa Venezuela kinafanywa nchini mwake.

Lukashenko amedai kuwa uingiliaji wa nje dhidi ya Belarus unakuja kutoka Poland, Lithuania na Ukraine.

Lukashenko, ambaye pia amekosoa uamuzi uliochukuliwa na Bunge la Ulaya kwa kutotambua matokeo ya uchaguzi wa Rais nchini Belarus, amesema,

"Tulifanya uchaguzi katika nchi yetu kulingana na Katiba na Sheria. Hatuhitaji wewe kutambua uchaguzi. Uchaguzi ulifanywa kisheria."

Akisisitiza kuwa wale wanaoiingilia Belarus kutoka nje hawajui nini kinaweza kufanyika katika kipindi kijacho, Lukashenko ameendelea kwa kusema:

"Kabla hatujaanzisha vita, tunajua kwamba wana mbinu chache sana zilizobaki. Kwa hivyo tunapaswa kuandaa nusu ya jeshi kuwa tayari kwa vita. Tunapaswa kufunga mipaka na Magharibi, haswa Poland na Lithuania. Kwa huzuni kubwa, lazima tuimarishe usalama wa mipaka na ndugu zetu wa Ukraine. inatubidi. "

Akisisitiza kuwa anapinga vita , Lukashenko, amenukuliwa,

"Tunakaribia janga baya sana. Ikiwa wao (Ulaya) watakuja hapa itabidi tuwajibu. Hatutapiga magoti hata tukibaki peke yetu."

Baada ya Rais wa sasa Aleksandr Lukashenko kushinda uchaguzi wa Rais uliofanyika tarehe 9 Agosti huko Belarus, maandamano yalianza na madai kwamba uchaguzi ulichakachuliwa.

Hawa viongozi wa upinzani wa haya mataifa wana misimamo kama Tundu Lisu! Ni wapenda sera za mataifa ya mangaribi ambao ndio walioshika mpini kwenye hii dunia.
Lisu

View attachment 1573185
Marekani na washirika wake wa NATO wanachotaka ni kwamba nchi zote zilizokuwa ndani ya iliyokuwa Soviet Union zinapokonywa kutoka kwenye siasa zenye ushawishi wa Russia, na kuzifanya zifuate ushawishi wa kimagharibi. Dhumuni kubwa ni kuzifanya hizo zote ziwe mahasimu wa Russia kijeshi na kiuchumi kwa msaada wa NATO. Mwisho wa siku hizo nchi zitageuzwa kuwa military base za NATO kwa ajili ya kuidhibiti Russia kijeshi na kiuchumi.
Upo sahihi mkuu. Ila kwa Tanzania mataifa ya magharibi yanataka kupambana na China kwenye maswala ya kiuchumi na kidemokrasia.
Katika uchaguzi huu wanamtaka Lisu huku Uchina ikitaka ccm iendelee kutawala
 
Nikiangalia kitanzi wanachokipitia mataifa hayo kuna uwezekano Tanzania nayo itapitia kitanzi hichohicho kupitia kwa upinzani wa Lisu dhidi ya serikali isiyojali haki za binadamu na uhuru wa mtu mmoja mmoja
Tanzania kamwe haiwezi kupitia katika hali hii mtu mmoja tu amabaye ni lissu hana uwezo wa kutikisa amani ya nchi yetu hata kidogo
 
Nilifika Venezuela kikazi mwaka jana,nikakaa siku tisa Maracaibo,pamoja na matatizo yao yote hatuwezi kujifananisha nao,wanakula vizuri,wanavaa vizuri hata nyuso zao huwezi kuzifananisha na nyuso zetu za kinyonge. kwa kifupi wanafuraha kushinda EAST AFRICA yote kwa ujumla.
 
Nilifika Venezuela kikazi mwaka jana,nikakaa siku tisa Maracaibo,pamoja na matatizo yao yote hatuwezi kujifananisha nao,wanakula vizuri,wanavaa vizuri hata nyuso zao huwezi kuzifananisha na nyuso zetu za kinyonge. kwa kifupi wanafuraha kushinda EAST AFRICA yote kwa ujumla.
Sasa fikiria nguvu waliyotumia mataifa ya magharibi dhidi ya taifa hilo waielekeze Tanzania. Tutatoka salama kweli?
 
Marekani na washirika wake wa NATO wanachotaka ni kwamba nchi zote zilizokuwa ndani ya iliyokuwa Soviet Union zinapokonywa kutoka kwenye siasa zenye ushawishi wa Russia, na kuzifanya zifuate ushawishi wa kimagharibi. Dhumuni kubwa ni kuzifanya hizo zote ziwe mahasimu wa Russia kijeshi na kiuchumi kwa msaada wa NATO. Mwisho wa siku hizo nchi zitageuzwa kuwa military base za NATO kwa ajili ya kuidhibiti Russia kijeshi na kiuchumi.
At least wewe unaona yajayo! Ndio dunia tunaoishi.
 
Sio Ukraine yote kimeo mkuu ila ni yale maeneo ysliyoathiriwa na vita
Sawa Mkuu. Hata hivyo, maeneo yaliyoathirika na vita ni majimbo mawili ya 'Luhansk and Donetsk' i.e. Donbass regions mashariki mwa Ukraine. Maeneo haya yanaiunga mkono Russia. Binafsi, sidhani kama maeneo hayo yanaweza kuathiri Belarus inayoungwa mkono na Russia kupitia CSTO.

Mkuu, nitashukuru sana kama utafafanua namna maeneo haya ni 'kimeo' kwa mustakabli wa uwepo wa Belarus imara.

Karibu.
 
Upo sahihi mkuu. Ila kwa Tanzania mataifa ya magharibi yanataka kupambana na China kwenye maswala ya kiuchumi na kidemokrasia.
Katika uchaguzi huu wanamtaka Lisu huku Uchina ikitaka ccm iendelee kutawala
Sidhani kam una taarifa za kutosha. China ilikuwa karibu sana na Tanzania wakati wa Jakaya Kikwete. Baada ya kuingia Magufuli, na kuanza kufuta hata mikataba iliyosainiwa kati ya Tanzania na China, Wachina wamejiweka mbali na Tanzania, ndiyo maana uwekezaji wowote uliokusudiwa toka China umesimama.

Miradi ya Makaa ya mawe na chuma kule Liganga imesimama. Tangu aingie Magufuli hawajawahi kufanya chochote.

Kwa sasa kila mwekazaji ana wasiwasi sana na security ya investment yake Tanzania. Na hiyo ndiyo sababu kubwa ya kupungua ukuaji wa uwekezaji Tanzania. Tanzania jwa sasa haina ukaribu mkubwa na Taifa lolote, tofauti na vipindi vya awamu nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom