S V Surovikin
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 13,700
- 33,071
- Thread starter
- #21
Hatari kutokea Ukraine kwenda Belarus sio kutoka maeneo yenye usalama hafifu bali ni kutokea moja kwa moja kwa serikali iliyo madarakani sababu ni serikali inayofuata sera za magharibi na kwa kiasi kikubwa iliwekwa na mataifa ya magharibi, hivyo majasusi wa maadui wa Belarus wapo huru kuamua kutumia nchi ya Ukraine kuhujumu serikali ya Bwana Alexander Lukashenko.Sawa Mkuu. Hata hivyo, maeneo yaliyoathirika na vita ni majimbo mawili ya 'Luhansk and Donetsk' i.e. Donbass regions mashariki mwa Ukraine. Maeneo haya yanaiunga mkono Russia. Binafsi, sidhani kama maeneo hayo yanaweza kuathiri Belarus inayoungwa mkono na Russia kupitia CSTO.
Mkuu, nitashukuru sana kama utafafanua namna maeneo haya ni 'kimeo' kwa mustakabli wa uwepo wa Belarus imara.
Karibu.
Lukashenko anaziona serikali za Lithuania, Poland na Ukraine kama zilizo tayari kusaidiana na mataifa ya magharibi kumng'oa madarakani ndio maana anataka kufunga mipaka ya nchi yake dhidi ya nchi hizo
Ni kama Marekani ilivyotaka kutumia Columbia kupenyeza mamluki wake kwenda kumng'oa Nicolaus Maduro wa Venezuela