OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo waungwana , heshima kwenu ! Leo vijana makamanda (BAVICHA Mkoa Singida) watafanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Standi ya Zamani katikati ya mji wa Singida . Wazungumzaji watakuwa ni viongozi BAVICHA mkoa Singida na Viongozi wengine wa mkoa akiwemo Katibu wa mkoa, kamanda Msuta, mkutano huo utaanza saa 9 mchana. Lengo la mkutano huo ni mwendelezo wa vuguvugu la mabadiliko, maarufu M4C ambalo dhima yake kubwa ni kufikisha elimu ya ukombozi wa pili toka kwa mkoloni mweusi (CCM) .Pili mkutano huo unalenga kufuta na kukemea juhudi za makusudi zinazo ratibiwa na kufanywa na CCM kuhujumu vuguvugu la mabadiliko kwa kuwanunua vijana wa cdm wachumia matumbo na wapiga dili badala ya kununua dawa, vitanda hospitalini, kujenga madarasa, kununua madawati, kutoa mikopo kwa dada zetu wanaojiuza kwa mia tano sababu ya njaa, kununua vyakula kwani watanzani wanakufa njaa Ngorongoro n.k. My take :- Acha Mwigulu Nchemba a.k.a Lameck Mkumbo aendeleze matusi yasiyo na staha kwa umma dhidi ya Dr Slaa na Wabunge wa cdm badala ya kusimamia ilani ya ccm yenye kauli mbiu "MAISHA BORA KILA MTANZANIA ." Pia Nape endeleza Propaganda chini ya LUMUMBA PROPAGANDA FM ili CCM ife kibudu 2015. Naomba turejee Zaburi 15:2 " ULIMI WA MWENYE HEKIMA HUTAMKA MAARIFA VIZURI ,BALI VINYWA VYA WAPUMBAVU HUMWAGA UPUMBAVU ."