BASHADA
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 513
- 148
Ndugu wana jamvi, hivi majuzi nilisafiri na basi la Sumry lililokuwa linatoka Arusha kuja Mbeya. Tulipoondoka Morogoro, alipanda mtu mmoja aliyevaa nguo za Jeshi (bila shaka ni mwanajeshi yule),tulipofika usawa wa lile bwawa upande wa kushoto ukielekea Iringa (Sijui jina lake), na kabla ya kufikia walipo traffic, mara basi likasimama. Kuangalia upande wa kushoto wa barabara, tukaona gari dogo limepaki pembeni, watu watatu wako mle ndani, milango yote minne imefunguliwa. Walipoona basi limefika wale jamaa kwenye gari dogo walishuka kijeshi kijeshi fasta, wakafungua buti, wakatoa mabox fulani wakayaingiza kwenye buti la sumry kwa style ya haraka sana. Wakati wanamalizia kupakia yale maboksi, yule mwanajeshi aliyekuwa kwenye basi akashuka na kuingia kwenye gari dogo na kuondoka na hilo gari dogo, na basi likaendelea na safari.
Abiria tukaanza kushikwa na mshangao na kujiulizamaswali kibao. Mtu aliyekaa karibu na mimi akaniambia hii ni mara ya tatu anasafiri na hili basi na kuona wakifanya huu mchezo. Kuna kila dalili kuwa kuna magendo au mzigo haramu unasafirishwa, kwani waweza kujiuliza, kwa nini wasioakie stend? Kwa nini wakapakie maporini? Kwa nini yule mwanajeshi kapandia Morogoro na kushukia tuu pale mbele? Kumbe siyo msafiri? Na ana uhusiano gani na wale waliokuwa wametangulia na gari dogo?
Bila shaka kuna harufu ya ufisadi na utakuwa unafanywa na vigogo serikalini.
Abiria tukaanza kushikwa na mshangao na kujiulizamaswali kibao. Mtu aliyekaa karibu na mimi akaniambia hii ni mara ya tatu anasafiri na hili basi na kuona wakifanya huu mchezo. Kuna kila dalili kuwa kuna magendo au mzigo haramu unasafirishwa, kwani waweza kujiuliza, kwa nini wasioakie stend? Kwa nini wakapakie maporini? Kwa nini yule mwanajeshi kapandia Morogoro na kushukia tuu pale mbele? Kumbe siyo msafiri? Na ana uhusiano gani na wale waliokuwa wametangulia na gari dogo?
Bila shaka kuna harufu ya ufisadi na utakuwa unafanywa na vigogo serikalini.