Basi la Hekima Laanguka na kuua Tanangozi

Mungu wangu!
Ajali kwa mara nyingine!!
mabasi ya Hekima nayafahamu na ni maarufu sana kwa kuwa na mwendo kasi mkali sana.
Imezoeleka ukitaka kufika mbeya mapema, panda Hekima, Mbeya express au happy Nation.
 
Mungu wangu!
Ajali kwa mara nyingine!!
mabasi ya Hekima nayafahamu na ni maarufu sana kwa kuwa na mwendo kasi mkali sana.
Imezoeleka ukitaka kufika mbeya mapema, panda Hekima, Mbeya express au happy Nation.

mdau mmoja amesema Hekima tangu waanze hakuna gari yao imewai kupata ajali.
 
mdau mmoja amesema Hekima tangu waanze hakuna gari yao imewai kupata ajali.

si kweli.
Mwaka 2008 ilipata ajali ingawa hakukuwa na abiria aliyepoteza maisha lakini majeruhi walikuwepo.
huyo mdau hakuwa na uhakika na alichokisema.
 
duh! sasa tukimbilie wapi?
Tunapigika na tunakufa kwa mambo yanayoweza kuepukika.
 
RIP marehemu wote. Unajua TZ tunatumia barabara kwa usafiri kwa asilimia zaidi ya 98. Sasa ajali nyingi lazima zitokee barabarani. Dunia nzima zinatokea ajali za barabarani. it is a dangerous means of transport!!
 
Terrible. Lakini why Tz things like these are daily on the increase?
Hata mimi napata kigugumizi, sijui tumeasi? I dont know kwakweli. MUNGU atusamehe tulipokosea jamani vinginevyo tutakwisha kabla ya wakati wetu!!! It pains once you think twice and deeply. Fikiria umekaa stendi unamsubiri mdogo wako anatoka safari halafu unasikia basi alilopanda limepata ajali
 
niliwahi panda hili basi toka mbeya mpaka dar,kwakweli ilikua ni hatari sishangai likipinduka na kuua wengi,spidi jamaa alikua anaenda nayo ni hatari,nasikia alitoka lusaka zambia saa 12 asubuhi,tumefika dar saa tisa na nusu likiwa ni basi la kwanza kuingia,nilishikilia roho toka mbeya hadi dar,maana hiyo spidi mmh,poleni majeruhi na marehemu.
 
niliwahi panda hili basi toka mbeya mpaka dar,kwakweli ilikua ni hatari sishangai likipinduka na kuua wengi,spidi jamaa alikua anaenda nayo ni hatari,nasikia alitoka lusaka zambia saa 12 asubuhi,tumefika dar saa tisa na nusu likiwa ni basi la kwanza kuingia,nilishikilia roho toka mbeya hadi dar,maana hiyo spidi mmh,poleni majeruhi na marehemu.
Kwanini hamuwashushii kichapo hao madereva?
 
Tuwaombee wahanga.
Haya ndiyo maisha yetu tuliyoyazoea. tukiamua pamoja kwa dhati tutabadilika
 
Nilisafiri hivi karibuni kwa njia ya barabara kwenda Mbeya. Kwa kweli hali niliyoiona inatisha. Madereva wengi wa ma-bus wanakwenda mwendo kasi na hu-overtake hata sehemu zisizopaswa ku-overtake. Nilijisemea moyoni "ndio maana ajali nyingi hutokea'. Ajali nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva na sio 'mapenzi ya Mungu' kama tunavyokimbilia kusema mara nyingi.
 
Inasikitisha sana... lakini ndani ya miezi mitatu tu, tumepata taarifa za ajali hizi nyingi, what's wrong?

Some thing is wrong? Yes! Kila mtu anakimbilia kujiwezesha kimaisha baada ya kuonekana kuwa sheria Tanzania hazina maana haswa pale ambapo una pesa. Leseni zinatolewa kama njugu! ukiikosa dar es salaam utaifuatilia kigoma n.k.

Usafiri wa ardhini uliosalama zaidi ni wa treni, lakini kwa kuwa serikali haina mpango madhubuti kuimarisha chochote nchini katika sheria zinazohusu usalama barabarani (kwa kuwa hii ni mitaji wa watu (polisi)), sasa inaelekea inaweka mikakati ya kuimarisha usafiri wa anga ambao pia nao ni salama kuliko barabara, ila yaliyotokea mwanza na ndege yenyewe moja! sijui mwendo ni upi!

Poleni sana majeruhi na walifariki katika hii ajali wapumzeike kwa amani.

Kutoka hapa sasa tunaelekea wapi? IGP, Waziri wa usalama wa raia na Rais wanatuambia nini katika hali hii? Tumewapa madaraka na masurufu manene ili washuhudia tunavyoangamia?
 
nilisafiri hivi karibuni kwa njia ya barabara kwenda mbeya. Kwa kweli hali niliyoiona inatisha. Madereva wengi wa ma-bus wanakwenda mwendo kasi na hu-overtake hata sehemu zisizopaswa ku-overtake. Nilijisemea moyoni "ndio maana ajali nyingi hutokea'. Ajali nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva na sio 'mapenzi ya mungu' kama tunavyokimbilia kusema mara nyingi.

yame nikumbusha yaliyotukuta kwenye basi la newforce tukitokea Dar mwanzoni wa mwaka huu.poleni sana majeruhi na mungu awalaze marehemu wote mahala pema peponi na majeruhi awabariki wapone mapema.
 
Wakuu hivi inawezekana abiria tujichukulie sheria mkononi tuwachape madereva wehu hawa?? nimesema hivyo kwa kuwa traffic wetu wanapewa mishiko ile ya Jerry Muro's camera na wanakaa kimya. Wakitokea wachache wakichapwa then watashika adabu. Je ni wazalendo wangapi tumepoteza na wengine kuachwa with permanent disability kwa kuanzia tu January 2010? Let us come up with solutions, tuanzie wapi jamani?
 
Mbona inasemekana hakuna aliyekufa mpaka sasa, rafiki yangu kapita eneo hilo mda mfupi, anasema imetokea tanangozi mita chache baada ya ile minara mingi ya simu, likiwa linatoka tunduma kwenda dar. Mungu awape faraja yake waliokutwa na tatizo hilo.

Ni habari njema kama roho za abiria zimesalimika.
 
Mbona inasemekana hakuna aliyekufa mpaka sasa, rafiki yangu kapita eneo hilo mda mfupi, anasema imetokea tanangozi mita chache baada ya ile minara mingi ya simu, likiwa linatoka tunduma kwenda dar. Mungu awape faraja yake waliokutwa na tatizo hilo.

Issue ni kufa au ajali kutokea.....hivi unajua mtu anaathirika kiasi gani kisaikolojia na ajali? na TZ hamna sehemu za kutoa ushauri/counselling? ila tushukuru Mungu kama hakuna kifo. Poleni wahanga na Mungu atawapa nguvu
 
Back
Top Bottom