Mimi ninachojiuliza ni hivi mtu yeyote huko duniani akitunga wimbo wenye 'maudhui' yaliyo tofauti na Tanzania hairuhusiwi kuusikiliza hapa!? Tuchukulie uko katika lugha tofauti na kama tunavyojua wanamuziki ni wengi duniani na kila mmoja anatoa wimbo wake. Sasa Ney wa Mitego sijui akienda akarekodi wimbo tuseme Amerika, Ulaya, Asia nk wakaupenda alafu TZ na basata yetu tukaupinga, hao basata wataenda huko duniani kuwaambia wamiliki wa tv, maredio na mitandao kuwa "huo wimbo mnaupenda lakini sisi TZ tumeupiga marufuku na nyie hamruhusiwi kuusikiliza"!
Hawana uwezo wa kumzuiya Ney asifanye anachotaka kufanya, labda tu kama Nay atakuwa ni goigoi wa sheria.nimesikia pia kipindi cha XXL cha Clouds FM wakisema. siungi mkono hii kitu sababu Nay atakuwa na watu wengi wanamtegemea kwenye sanaa yake, ningemshauri Nay awaombe radhi basata au aende kwenye vyombo vya sheria,
basata pia watumie busara, inakuwaje nyimbo tu zinafanya msanii anafungiwa daima!