Baraza la wawakilishi lafunguka: Tusilazimishane katika muungano huu. Watanganyika wanatuhadaa

Sasa raza kwa nini asilete mswada wa kura ya maoni ili Zanzibar ijitoe kwenye Muungano?
Ukiwasiliza wote hakuna anyesema muungano uvunjwe kila mmoja anazunguka zunguka.
Ili hoja za mtu ziwe na mashiko kule Zanzibar ni lazima uutaje ukristo. Vatican na muungano wapi na wapi?
Tunasubiri wabunge wa Bunge la JMT kutoka Zanzibar watamke kuwa hawataki muungano, tena wafanye hivyo wakati wa kujadili bajeti hii. Wakimaliza waondoke bungeni ili dunia ijue muungano umekufa na Wazanzibar wamedhamiria.

Tunasubiri Baraza la wawakilishi litoe tamko la kutomtambua Makamu wa Rais wa JMT aliyepatika kutokana na Uzanzibar wake.

Tunataka BLW lisitishe shughuli za barazani ili hoja ya kura ya maoni au kuvunja muungano ijadiliwe rasmi. Hii itasadia bajeti za nchi zote kuwa na uhalisia.

LET ZANZIBAR GO! GO ASAP
 
Hilo lina- justify ujinga wenu?


Ni bora ujinga wa kujitawala kuliko kutawaliwa, puuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!!!!!! Lazima muitoe Zenji ya watu, vinga'nga'nizi hamna hata haya, ondokeni wenyewe hawataki uamshoooooooooooooooooooo juuuuuuuuuuuuuuu.
 
Kweli wazanzibar hawafai kabisa! mpaka leo wanadha kuna wajomba wa kuwasaidia kuwapelekea maendeleo? wanaota OIC, UAE,sijui nani, nani kawambia kuna vya bure duniani? elimu bado inahitajika sana kuwakomboa wenzetu kifikra, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.
 
Nijuzeni wakuu, kati ya shia na suni nani wengi pale zinjibar,
najaribu kutafakari pale so-malia wale jamaa naambiwa ni waislamu karibu wote! Mbona serikali inashindikana? Nachelea kusema TAMAA MBELE. . . . . . . . . . . .
 
Jamuhuri Ya Watu Wa Zanzibar kwanza. Mkoloni Tanganyika mwisho Chumbe:nono:

TUNA HAMU SANA NA MAFUTA YA ZNZ!! Sijui yaanza kuchimbwa lini ili tuyauze kisha Wazanzibari tuwape makanzu na mabaibui wapendeze
 
mbona hakuuliza vipi wizara ya Afya ya Tanzania Bara kuongozwa na Dr Mwinyi Mzanzibar wakati wizara hiyo sio ya muungano? na waziri wao wa madini alikuwa wapi mpaka asishiriki huo mkutano?
 
Malumbano,

Ukitaka uonekane mwanasiasa mahiri Zanzibar kashifu waTanganyika[muungano] nakwambia hata kichaa atakuona wa maana.Bahati mbaya wanasiasa wa Zanzibar wameshindwa wameshindwa kutimiza matarajio ya wapiga kura wao kimbilio la kuwaadaa wananchi wa Zanzibar ni kuutukana muungano,kuukashifu muungano,kuukejeli muungano na kuchoma makanisa.

Zipo nchi kibao zilizojiunga na OIC lakini bado zinakabiliwa na matatizo ya miundombinu,elimu na nk.OIC sijawabu la matatizo ya Zanzibar.Matatizo ya Zanzibar yatatatuliwa na wazanzibar wenyewe kwa kufanyakazi kwa bidii na maarifa.Kuna watu wa ajabu sana huko Zanzibar wanadhani dunia ya leo maendeleo yataletwa na misaada ya mataifa ya nje.

CCM ni chama tawala ifike mahali wafanye maamuzi magumu ingawa kwangu naamini ni maamuzi mepesi sana wawape waZanzibar kisiwa chao hakuna haja ya kulazimishana hizi lawama na kejeli zimetosha tusiache hadi mambo yaharibike kabisa tufanye maamuzi sasa.

Ngogo,

Unachokisema ndiyo kilitakiwa kifanyike. Tatizo ni la hao magamba wenzenu. Wanajua muungano ukivunjika itabidi katiba mpya na TZ mpya kama ilvyokuwa USSR............ Sasa hawataki kupoteza the so called POWER!!! Ndiyo maana bajeti tu mbadala akina Ncheba inawatia wazimu na kudai wapinzani wana pepo za madaraka na wanasitahili kuombewa wakati wanasahau kuwa ni wao ndiyo wenye pepo wa madaraka!!
 
Kaka uliza uwambiwe usikurupuke au ndio usomi wetu watanganyika kuchangia tu japo uwongo.Dr.Mwinyi si mzanzibari ni mtaanganyika kwao ni mkuranga Baba yake Mzee Ali Hassan Mwinyi ni mtu wa mkuranga na wazazi wa mzee mwinyi wote wamezikwa mkuranga fanya utafiti kidogo tu utaupata ukweli na ndio maana kipindi cha mwanzo cha ubunge wake alikuwa ni mbunge wa mkuranga mbona umesahau.kugombea zanzibar alikwenda kwa mission maalum na kimsingi alilazimishwa yeye mwenyewe alikuwa hataki alipelekwa ili baadae aje agombee uraisi jambo ambalo haliwezekani kwani mzee mwinyi hakubaliki zanzibar anaonekana kama ni msaliti mkuu wa wazanzibari kaka usikurupuke Dr.Hussein ni ndugu yetu na ni mtanganyika halisi na hana nafasi yeyote zanzibar na hata ubunge hakushinda alipewa tu ubunge kwa mtutu wa bunduki .

baada ya hapo utasikia mpemba huyu muunguja. Mnashida nyinyi!
 
Bado kuna umuhimu mkubwa sana wa kuujadili huu muungano. Wazanzibar waachwe waujadili bila kuwekewa mipaka mpaka wafikie muafaka! Kimsingi mimi sioni tulichoungana zaidi ya ku 'sacrifice' tanganyika yetu kwa kuigawana na wanzanzibar wakati wao wakifaidi peke yao!! Chetu chao - chao chao
 
Akili nzuri ukiwa nayo. Hivi lini mlisikia Tanzania imepewa msaada na Vatican? Ubalozi si sawa na kujiunga na jumuiya ya dini. Tanzania ina ubalozi kwenye Jamhuri ya Kiislam ya Iran, hiyo inaongeza nini kwetu ukiondoa mahusiano ya kibalozi?

Kama kuna waarabu ambao hawawezi kuwasaidia mpk mjiunge na dini yao basi mnakubali utumwa. Tena utumwa mbaya unaoanzia kichwani. Imefikia sehemu leo Zanzibar inayojifanya inataka kuwa huru ikabidhiwe kwa OIC? Kwa hiyo mnataka Zanzibar huru au Zanzibar inayomilikiwa na OIC?

Mnapojenga hoja tumieni akili zenu. Vatican ni dola kama ilivyo Iran na Saudia, na mahusiano yake na Tanzania ni ya KIBALOZI na si kwamba Tanzania ni mwanachama wa UKATOLIKI.

Kuna mmoja wa hao wawakilishi amekiri kuwa hawana Elimu, naunga mkono. Utumbo kama huu uliobandikwa hapa hauwezi kusemwa na mtu aliyemaliza kidato cha pili, labda awe amesoma shule ya kata

Sasa naamini ukisha kuwa muislam unaandamwa na laana .Haya wacha walie na Vatican
 
BWANA YESU ANAOKOA, KWA NINI MNAUMIZA AKILI HIVI?KWA NINI MNASONONEKA?KWA NINI MNAHANGAIKA NA HII DUNIA? MPE BWANA YESU MAISHA YAKO NA KUHAKIKISHIA HUTA JUTA,roho ya hasira,chuki na mambo mabaya yataondoka nawe utakuwa mwenye furaha muda wote.KARIBU KANISA LOLOTE LILILOKARIBU NAWE LINALOAMINI WOKOVU.
AU TUWASILIANE KWA EMAIL :johnhella2007@yahoo.com hiyo email naitumia hata facebook ukisearch kwa email hiyo utanipata

Nje ya mada mkuu.
 
Kuna maji2 humu hayana hoja. Nyinyi wakiristo kwanini munakuwa na chuki hivi na uislam? Acheni chuki zenu ,acheni ushabiki wenu.Ongeeni point za mcngi kama munataka kukipinga kinachoongewa hapo.Nyinyi maisha mutakuwa wajinga ivo.Kuweni na busara. Hapa 2nataka hoja za mcngi ,kama unapinga hoja pinga lakin acha kupinga kwa hoja za kidin chuki.
 
Shujaa ni yule anaepigania ardhi yake au nchi yake takatifu, kuwa na muungano/Tanzania ni bahati mbaya sana kwa Mzanzibari yyte, wacha aonekane shujaa kwa Wazanzibari na tena sio shujaa bali ni dhahabu/lulu.
Mnataka utwana na ubwana toka lini Mhindi Raza akatetea kuondoa ukoloni wa kiarabu? Leo tumeeleweshwa humuggumu jamvini JF kisa cha kuuvunja Muungano ni Jamsheed arudi na watu hao wapo Arabuni na UK
Hebu chukueni kisiwa chenu lakini msiwe ni waarabu au wahindi hapo sio kwenu
 
Wanataka hata muswada wa kura ya maoni uandaliwe na Tanganyika. Mbeleko mbeleko!
Historia itajirudia tu, hakutakuwa na jipya katika hilo. Ule mkataba wa kuunganisha baadhi ya mambo ya Tanganyika na Zanzibar uliandaliwa wapi?

Ni vyema pia katika kuuvunja mswada uandaliwe huku huku Tanganyika aka Bara.

Oyaa CCM watayarishieni "magaidi" "wachoma moto makanisa" mswada wa kura ya maoni ,mambo yaishe!
 
Ukiwasiliza wote hakuna anyesema muungano uvunjwe kila mmoja anazunguka zunguka.
Ili hoja za mtu ziwe na mashiko kule Zanzibar ni lazima uutaje ukristo. Vatican na muungano wapi na wapi?
Tunasubiri wabunge wa Bunge la JMT kutoka Zanzibar watamke kuwa hawataki muungano, tena wafanye hivyo wakati wa kujadili bajeti hii. Wakimaliza waondoke bungeni ili dunia ijue muungano umekufa na Wazanzibar wamedhamiria.

Tunasubiri Baraza la wawakilishi litoe tamko la kutomtambua Makamu wa Rais wa JMT aliyepatika kutokana na Uzanzibar wake.

Tunataka BLW lisitishe shughuli za barazani ili hoja ya kura ya maoni au kuvunja muungano ijadiliwe rasmi. Hii itasadia bajeti za nchi zote kuwa na uhalisia.

LET ZANZIBAR GO! GO ASAP

Huko kote unaenda mbali, ukianzia na Raza au KILAZA wakati anagombea uwakilishi si kuna wana ccm toka bara walikwenda kumpigia debe? kwa nini hakuwakataa na kusema yeye ni mgunya hahitaji nguvu na tarumbeta za bara?

Unakuja hizi kelele, ni kwa nini wameshindwa kuwambia wabunge wa zanzibar kuwa wasiende Dodoma kwani hawajawatuma kwenda huko? au wanatuambia kuwa hao wameenda kuiba hela za wabara bila ridhaa yao?

Kuvunja muungano kama wanavyodai kuwa wazanzibar wote wanataka sidhani kama ni kweli kwani ingekuwa hivyo, nini kimewafanya waende Dodoma?

Hilo BLW wanashindwa nini kujadili? kama hali ya nchi ni tete?
 
Back
Top Bottom