Baraza la mawaziri kutangazwa wakati wowote-Ikulu!!

I continue to be puzzled by myself coz though I hate it as much but I keep comment and arguing about it. I muzzle now.
 
Herald Hunter una hunt nini sasa? Badili heading yako mtu akija atadhani una tetesi za majina kumbe ni blah blah fulani hivi.
 
au kwa kumsaidia mleta mada, Invizibo au PAW au mod yeyote aunganishe huu uzi ni zingine zinazoongelea speculATION ya new baraza.
 
modes hizi threads za baraza jipya zimekuwa kero sasa. Napendekeza thread zote za baraza zifutwe (delete)
 
It always puzzles me! Kwa nini dogo hupenda sana kuteua? Akina Warioba & Co - mliangalie hili, Rais ajaye apokonywe hii, maana humuwezesha kujaza maswahiba na washikaji na hivyo mambo kurudi nyuma badala ya kwenda mbele.
 
Herald Hunter una hunt nini sasa? Badili heading yako mtu akija atadhani una tetesi za majina kumbe ni blah blah fulani hivi.

sio abadili naona mods wazuie thread yoyote ya baraza maana sasa imekinaisha!! kila mtu anapost anachojua!! hata kuna jamaa najua yupo south africa nae naona anasema ametoka ikulu !!
 
Hii inaweza kuwa thread dhaifu kuzidi zote zilizowahi kuletwa humu JF.

Kwani baba amekwambia atalitangaza lini baraza jipya la mawaziri au anakusubiri magogoni mkateue nyote maana urais huu si ni wa familia?
 
Hata mimi nina mtazamo huo huo, ni kweli asipofanya hivyo mambo yanaweza kumuwia magumu
 
Kikwete yuleyule, Pinda yule yule, uwezo wao ule ule, chama kile chenye wanamtandao walewale.

Kweli yataka moyo sana kutegemea kupata baraza jipya eti "lenye ubora"

Haya mabadiliko ambayo wanataka kuyafanya kwa msingi upi !!! Kiukweli sithani kama wanaweza kuleta mabadiliko kwa gafla kiasi hicho..!! Tuache kudanganyana hapa ni sawa na Kazi bure....
 
Mkuu Kilasara wabunge wakichaguliwa kazi ya kwanza ni kumchagua spika na kisha spika anawaapisha. Baada ya hapo Rais anateua PM ambaye jina lake linapelekwa Bungeni kwa ajili ya kupitishwa. Baada ya Waziri Mkuu kupitishwa ndio wanakaa na Rais ili kuteua mawaziri. Hivyo so lweli kwamba mawaziri wanateuliwa kabla ya kuapa. Unless kwenye wabunge wa kuteuliwa na rais labda kuna utaratibu mwingine wa kuapa.


Mhe. Kimbunga,

Ni s
ahihi kusema kwamba Wabunge wanapochaguliwa, kazi yao ya kwanza ni kumchagua Spika ambae anawalisha kiapo cha Ubunge.

Lakini uzoefu wangu (wa enzi za Nyerere) ni kuwa Rais anawalisha wateule wake kiapo cha uwaziri hata kabla ya kikao cha kwanza cha Bunge.

Pia huku kusema kuwa "Waziri Mkuu anakaa na Rais kuteua mawaziri" siyo sahihi sana. Mara nyingi utakuta huyo Waziri Mkuu atakuwa ameshtukiwa kupewa wadhifa huo, na hapo pia Rais atakuwa na watu wake ambao ameshaamua atawapa uwaziri. Ni kweli kuwa P.M. mwenye uzoefu anashauriana na Rais juu ya uteuzi wa mawaziri; lakini hii si wakati wa mwanzo wa kipindi au wakati ule yeye mwenyewe P.M. ndio anaanza kazi.
 
Ikulu imetoa taarifa rasmi kwamba baraza jipya la mawaziri liko jikoni na sasa litatangazwa muda wowote kuanzia sasa..

Taarifa hiyo imeongeza kwamba baraza hilo litakua lina ubora wa hali ya juu sana.

Chanzo:gazeti mwananchi.

Kinachoniuma sana roho hao watuhumiwa wote muda mfupi watapewa ubalozi nchi za watu
 
Mkuu Kilasara suala la Rais kushauriana na PM wakati wa kuteua baraza la mawaziri ni la Kikatiba kama Rais hashauriani na PM inakuwa ni kuvunja katiba. Enzi za Nyerere huenda mambo yalikuwa tofauti si unajua tena kwamba hii katiba ya sasa ya 1977 imefanyiwa mabadiliko kama 14 hivi. Wakati wa Nyerere kuna wakati PM alikuwa pia second VP ma wakati wa MWinyi PM alikuwa VP. Hii katiba tuliyonayo imejaribu kuingiza siasa za vyama vingi hivyo kuna mabadiliko mengi tu hapo (viraka). Hata akiwa PM ndio anateuliwa kwa mara ya kwanza anatakiwa ashirikishwe na hakuna Baraza ambalo limetangazwa sambamba na Kutangazwa PM (baada ya vyama vingi) anatangazwa PM kwanza anapitishwa na Bunge baadaye ndio baraza linatangazwa na kwa kuwa hii kazi ya kushauriana haifanyiki hadharani basi huwa tunaamini wameshauriana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom