Huitaji kujua yaliyomo ndani moyo wa mtu hadi uangalie matendo yake. Siku zote JK mlikuwa mnamuona rais legelege leo hii kwavile kawaumiza waislamu yaliyo moyoni mwao unasema ndio rahisi amekamilika kweli wajinga ndio waliwao. Let me see hii movie itaisha wapi kwani wakati wewe unafurahia ujue mwengine anaumia halafu unasema Tanzania kisiwa cha amani . St Augustine aliwahi kusema an unjust law or society is similar to no law or society of lawlessness wait and see.
<br />Ni kukosa vipaumbele, tatizo waislamu hata wakirudishiwa shule wanazodai..... kama zipo watazigeuza zote madrasa....
<br />iti is very clear sasa kila mtu atajua watu wa hapa JF na chadema ni watu waaina gani.<br />
ndo maana nilisema na narudia kusema kuwa uongozi wa JK umechukiwa kwa sababu ya hii mahakama ya kadhi, kujiunga na OIC na muafaka wa zenji. Sio hizi sababu zinazotolewa.<br />
kabla ya hapo hamna hata mmoja anayeweza kunithibitishia kinyume chake. ona leo mlivyofurahi. Sitaki kuwa bias, bias kwangu mwiko.
Kwa sisi waislam tunaona ametugeuka kwa kutoa majibu tofauti na alivyo tuahidi msikitini kipindi cha uchaguzi!! Kweli wanasiasa vigeugeu kikwete kigeugeu!!!
Amejivua gamba juu ya mahakama ya kadhi
<br />Shukrani ziende kwa KIGAGU wa Musoga!!
Nimefuatilia kwa karibu hotuba ya JK iliyorushwa LIVE na TBC katika baraza la Idd pale msikiti wa Gaddafi Dodoma. Nilikuwa natafuta tu channel yenye habari nzuri ila nilipofungua TBC nikamkuta Live na nikasema nisikilize angalau kwa DK 2 kwani siku nyingi nilikuwa sipotezi muda wangu kuangalia hotuba na mzee wa kaya.
Kwa mara ya kwanza tangu nianze kumsikia JK leo ameongea kwa ujasiri kama rais wa nchi kuwajibu sio waislam tu bali viongozi wengi wa dini including za Kikristo. JK ameonyesha tabia ambayo sijawahi iona tangu aingie madarakani kwa kuongea kwa ujasiri na msisitizo na serious huku akimwaangalia machoni Sheikh Mkuu kuhusu serikali kukataa kurudisha shule zilizokuwa za dini na suala la mahakama ya kadhi.
Issue hapa siyo mambo aliyoongea ila alivyoongea ameni bariki sana kwani nimejisikia nikilazimika kusikiliza hadi mwisho hotuba ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa na hadhi ya ki urais tofauti na hotuba zoote alizowahi kufanya.
Katiba hotuba hii JK hakuwa nacheka cheka kama ilivyo kawaida jambo ambalo limefanya niamini kwamba amepata mwana saikolojia wa kumpa shule ya essentials of public speech.
Issues hizi nzito ameongea kama rais bila kuzunguka, kutetereka wala kuuma maneno huku wakuu wa dini hiyo wakimwangalia kwa kutoonyesha kuridhika na wengine wakaanza kunongonezana.
Mzee wa Kaya usiishie hapo bali anza kwa usiriazi huo kupambana na mafisadi, majairo, kushughulikia umeme na masuala mengine yanayodidimiza taifa. Naamini kwa spidi hiyo hiyo mtazamo wetu kwako lazima utakuwa positive!!
Hasa Mwembechai; kwa sababu kwa kiasi kikubwa ameonesha kile ambacho serikali ya CCM haikutaka wananchi wakijue kuhusiana na uhusiano wake na masuala kadhaa ya Waislamu - na hapa nazungumza kwa ujumla tu. Nashukuru niliwahi kufanya naye mahojiano ya kina sana kuhusu kitabu chake hicho.
Lakini katika hili pia kuna suala la hekima. Sidhani - katika kufikiri kwangu - ilikuwa ni proper channel kuwateremshia Waislamu jambo hili siku ya Idi na kwa namna ya kisiasa jinsi ilivyotolewa.
1. Dodoma Secondary
2. Kizunguzi Secondary
3. Kondoa Secondary
4. Kwamire Girls
5. Hijra Secondary
6. Takwa Secondary
7. Jabal Hila Secondary