Ndugu zangu hii barabara ya nyuma ya ikulu ambayo hufungwa saa 12 jioni hadi saa 12 alfajiri inatumika na walinzi kama mradi wa kuwatoa pesa. Kwa mgeni si rahisi kujua njia imefungwa na hawa jamaa wakikushika badala ya kukurudisha wanakutisha ili wafanikiwe kukutoa pesa za kutosha. Kama viongozi wa wangekuwa waungwana wangeweka kizuizi ikifika jioni kinafungwa badala ya kuendelea na hii fedheha inayoendelea karibu na makazi ya rais wa nchi yetu. Naomba maoni yenu jamani.